18 May 2011


He has been enjoying his freedom to travel back to the UK of late.

And upon his return to London Snoop Dogg looked right at home, conducting a press conference from a gold throne and surrounded by scantily-clad pole dancers.

The rapper played host to the UK media in a strip club yesterday to promote his new album Doggumentary during his second trip to the UK since the ban was lifted.

Snoop Dogg strolled in to the press conference in a sky blue Adidas tracksuit and sipped on tea from a Union Jack mug.



'I'm grateful for being here and proving to the authorities that I deserve to be here. I have had so much love and support from the UK,' The 39-year-old said told the Daily Star.

'When I was a young rapper I would dream of coming here, and when I came I didn't want it to end.'
Snoop Dogg, real name Calvin Cordozar Broadus Jr, was banned from entering the UK following a brawl between his entourage and security at Heathrow airport in 2006.

The following year the Home Office prevented him from obtaining a visa to enter the country with fellow rapper P Diddy, claiming allowing him in the UK could inspire violence and crime amongst fans, despite that his intention was to hold a seminar for youths against gun crime and gang violence.

A judge ruled in 2008 that Snoop had not been at fault during the incident and that he had actually cooperated fully with immigration officials - the ban was fully overturned last year in time for Snoop to play Glastonbury over the summer.

The What's My Name hitmaker is looking forward though, and yesterday announced plans to create his own X Factor-style show.

'X Factor is great but I need to do a show that goes straight to the hood,' he told reporters.

I want to find that raw untamed talent that hasn't been dressed up all nice for the TV. 'Any TV companies want to help me, then they know where I am,' he added.

The competition would feature artists 'with no money, just raw talent and natural ability.'
Snoop Dogg received a warm welcome from fans at a gig later that night before heading to Madame JoJo's and then The Box in Soho.

Earlier this week Snoop performed in Brighton as part of his promotional tour for Doggumentary.


The album features guest performances by Kanye West, David Guetta and also Willie Nelson. At the press conference the rapper named Sade as his ultimate collaborator.

He also defended a more controversial collaboration - his recent record with Charlie Sheen, 'Winning' which was released earlier this month.

'Sheen was my friend before all this happened so I do not judge him,' Snoop Dogg insisted. 'He called on me and I came through for him.

'He is conducting his business, living and functioning. But if the station (CBS, the network behind Two And A Half Men) wanted to put him in a box, then what would have been crazy is staying in that situation.'



Hasheem Thabeet afanya.....

Na Brighton Masalu

STAA wa mpira wa kikapu, duniani akicheza katika Ligi ya NBA nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka ‘Super Tall’ (pichani) amefanya kufuru ya fedha baada ya kumwaga fedha ukumbini na kuwaacha watu wagombanie, twende mstari kwa mstari.

Paparazi wa gazeti hili lenye heshima ya nyota tano kwa habari za mastaa Bongo, alishuhudia tukio hilo live wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Bilicanas uliopo Posta, jijini Dar es Salaam ambapo handsome boy anayecharaza fimbo katika muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ alikuwa akipiga shoo babkubwa.

Awali kasuku wa gazeti hili alimshuhudia Hasheem akikatiza kwa madaha ukumbini humo, akiwa ameongozana na wapambe wake waliokuwa wakimuandalia njia, kisha kukaa sehemu moja na kuanza kula bata kwa mtindo wa ‘tingisha kama imeisha, leta nyingine’.

Wakati shoo ikiendelea Hasheem aliinuka na wapambe wake kuongoza mbele kama kawa, kisha wakaelekea jukwaani alipochomoa burungutu moja la ‘nyekundu nyekundu’ tupu na kumkabidhi Dully Sykes ambaye aliongeza manjonjo baada ya kutuzwa na supastaa huyo.

Hakuishia hapo, aliposhuka jukwaani, alizama mfukoni na kutoa burungutu lingine kisha akalirusha juu na mashabiki kuanza kugombania.

Wakati watu wakiendelea kukanyagana wakigombea mkwanja huo wa ‘sadakalawe’ Hasheem na wapambe wake walitoka nje na kuingia kwenye gari aina ya Hummer na kuondoka kiwanjani hapo.

“Duh! Ebwana ee, jamaa huyu ni noma yaani minoti yote hiyo kaiachia watu wanyang’anyane? Hii ni kufuru, kweli mshkaji fedha imemkubali,” alisika jamaa mmoja akisema ukumbini hapo.

Hasheem Thabeet amerejea nchini hivi karibuni akitokea Marekani anapoishi, yupo kwa mapumziko mafupi. Ni Mtanzania pekee anayeipeperusha bendera ya Tanzania kwenye ligi ya NBA ya mpira wa kikapu nchini humo.

Na yafuatayo ni maoni ya wasomaji wa gazeti hilo

Comment by Eddie Mourice Junior 1 hour ago
Kwa hili umechemka hasheem even if ur money!
Comment by KUU LA MAADUI 7 hours ago
Dogo pesa ni zako lakini kwa hii ya leo umetimba ,sikujua kama na wewe bado mgeni na pesa aise kwa nini unafanya hivyo hujui kama anaweza kufa mtu katika kugombania minoti halafu wewe ukastakiwa kwa kusababisha vifo ,aise umeniuthi unakuwa mrefuuu 22222222 nje ndani mfupi acha ulimbukeni najua hata ndugu zako hawata fuhia upuuzi huo,kama unapesa unakuwasha utumie katika mambo mazuri mungu atakubariki sio kurushia walevi.
Comment by Minja Frank 7 hours ago
Ona mwenzio mwenye kipaji cha mpira wa kikapu kama wewe Dikembe Mutombo wa DRC kajenga Hospital kubwa tu Kinshasa. Wewe wamwaga pesa yako kwenye masanga. Saidia nchi yako!!!
Comment by Alphoncene Gerald 8 hours ago
Sina hata cha kuchangia
Nachoka kabisa
Comment by Miriam John Mndolanga 8 hours ago
Ulivyofanya ndivyo nafsi yako ilivyokutuma, kwa upande wako ni sawa tu ila ni vema hela unayoitolea jasho na kusumbuka sana hadi kuipata ungeiwekeza kwa makundi yenye mahitaji maalum na Mungu atakubarikia zaidi ya ulichotoa. Jifunze kupitie kwa waliofanya kama hivyo wameishia wapi?
Badilika Hasheem, usijijengee sifa mbaya kwa jamii yako.
Comment by julius manning 8 hours ago
huo ni ulimbukeni mkubwa akumbuke akina Tyson walikuwa na hela kuliko yeye lakini leo je
Comment by swalih/waziri 8 hours ago
huo niulimbukieni wakati familia nyengine pesa yakula mtihani wewe pesa unazigawa kwa walevi inshlwa mungu akulaani uje kuzikumbuka sikatowe misaada makanisani msikitini na mashuleni wewe unagawa kwa walevi ili upate jina kuwa umegawa pesa<.
Comment by Matu 8 hours ago
Pesa ni sabuni ya roho lakini pesa nazo zina upepo wake...wakati ukuta...pesa ni kama maua..huchanua na kusinyaaa kwa mtoto wa manka sasa zimechanua...!
Comment by anna [email protected] 8 hours ago
Ama kweli masikini akipata matako huria mbwata, hivi wewe umesahau tabu zote ulizopita, haya baba wakati wako hivi humuoni mwenzio yule modo anaitwa matata kila mwaka anatoa msaada kwa yatima wewe unagawa pesa kwa walevi, una akili nyingi sana mtoto wewe, ina maana hata kule kijijini kwenu huna wanaohitaji msaada, utakuja juta baadae na hao wapambe huta waona sana watakucheka, wapi nice??? unalewa sina
Comment by ikk 8 hours ago
Kweli minoti unaigawa kwa watu wenye ziada tele, tena Klabu? Wakati kuna watoto yatima huko makete wanalea wadogo zao, tena kwa kupika pombe za kienyeji?
Laana huanza polepole!
Comment by Sebastian Salatiel Shemhilu 9 hours ago
DUUH!! HII NI DHARAU YA FEDHA AU JEURI YA FEDHA? HASHEEM TOA PESA ZAKO KWA YATIMA KULIKO KUWAPA PESA WALEVI NAMNA HIYO.MUNGU ATAKUPA ZAIDI.

Comment by Mapresha Getebariadi 9 hours ago
Hela iko wapi wenye fedha hawafanyi hivyo hapo alikuwa anawachanganya warembo waanze kujimwaga kwake. Kama anahela si asomeshe hata yatima 2 tu.
Comment by edmas 9 hours ago

Haya bana, wakati wako huu. Alikuwepo Mr. Nice naye alifanya kufuru ya pesa, sasa yupo apeche alolo, kushnei.
Comment by furaha Tausi 9 hours ago
WEE HASHEEM WEWE KWANINI HIYO HELA USIWASAIDIE HATA WATOTO WA MITAANI JAMANI HATA WALE WATOTO WALIOKO OCEAN ROAD HOSPITAL WANAUMWA KANSA?? MUNGU ATAKULAANI SHAURI YAKO

16 May 2011



Wasaidizi wana nafuu kuliko rais?

Ansbert Ngurumo

BAADHI yetu hatujaelewa ari, nguvu na kasi ya Rais Jakaya Kikwete. Nina hakika naye ameiimba, lakini hajaielewa barabara.

Kaulimbiu hii iliyoasisiwa na kina Samuel Sitta mwaka 2005, ilitumika kumtafutia urais mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya.

Waliomjua vema uwezo na udhaifu wake walidokeza mapema kwamba maisha ya Watanzania chini ya CCM ya Kikwete yangedorora na kuwa magumu zaidi - kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Baadaye, sisi na baadhi ya watani wa CCM tuliifupisha kaulimbiu hiyo, tukaiita ANGUKA. Ni kweli! Miaka mitano baadaye, wameangukia pua.

CCM imeanguka. Rais Kikwete ameanguka. Mtandao wake umeanguka. Na kwa bahati mbaya, hata serikali yake imeanguka, ikaishia kuwa serikali kopa-kopa – hata mishahara ya watumishi – licha ya kodi kubwa tunazolipa.

Kuanguka huku, ndiko kumekuwa chanzo cha kura chache za mgombea urais wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kuanguka huku ndiko kumekuwa kichocheo cha vilio vya wananchi dhidi ya ufisadi. Kuanguka huku ndiko kumesababisha hata usanii mpya wa CCM wa ‘kujivua gamba.’

Kuanguka huku ndiko kumemkosanisha Rais Kikwete na maswahiba wake wa siku nyingi. Kuanguka huku ndiko kumemfanya Rais Kikwete aogope maandamano ya wananchi yanayoratibiwa na CHADEMA hata akalialia kwamba “wanataka kuniondoa kabla ya wakati.”

Kuanguka huku ndiko kumemwondoa Yusuf Makamba katika ukatibu mkuu wa CCM, yeye na sekretariati na Kamati Kuu. Kuanguka huku ndiko kumerutubisha na kukuza fitina na vita ya makundi ndani ya CCM.

Kuanguka huku ndiko kumewafanya Watanzania kuikataa CCM waziwazi kuliko wakati wote katika historia, na ndiko kumemwingiza Nape Nnauye (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM) katika migogoro mipya ndani ya makundi ya CCM na kumwandalia anguko lake huko tunakokwenda, hasa baada ya Rais Kikwete kuondoka madarakani.

Anguko hili la ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya limewagusa wananchi wenyewe. Sasa wanakabiliwa na ukali wa maisha usiofanana kabisa na ahadi kemkemu walizopewa na CCM mwaka 2005 na 2010.

Bahati mbaya waliosababisha anguko hili, bado wanajitapa kwamba wameleta maendeleo. Vipofu!

Na kwa sababu ya upofu huu, wanakosa mikakati mipya ya kujikwamua. Wanarudiarudia yale yale yaliyoshindwa kuwanusuru miaka mitano iliyopita.

Kwa mfano, mwaka 2006 mwanzoni, Rais Kikwete aliingia na mbinu ya kutembelea wizara moja moja, kutoa maelekezo na kupiga picha na watumishi wa wizara hizo. Ilikuwa propaganda na mapambo ya magazeti na televisheni.

Baadaye, aliwaita mawaziri na watumishi waandamizi wa serikali (mara mbili) katika semina elekezi kwenye Hoteli ya kifahari, Ngurdoto, Arusha.

Leo tunapotazama nyuma, ni nani anaweza kujivunia semina elekezi za Ngurdoto?

Lakini watu wasiojifunza hawafichiki. Mwaka jana, rais yule yule akagombea kwa kaulimbiu ya ari zaidi, kasi zaidi na nguvu zaidi. Yaani, hawa jamaa hawakuridhika na ’anguko jipya’ la 2006. Waliona hilo halitoshi, wakatuandaa “kuanguka zaidi” mwaka 2010!

Haikumwongezea kura mgombea wao. Haikuvuta hisia za vijana wala kina mama. Ili kupata watu wa kuhutubia ilibidi CCM itumie pesa nyingi kuchapisha na kugawa sare, kuwagawia watu na kuwapakia kwenye magari kuwapeleka kwenye mikutano ya mbali.

Haikuwaunganisha watawala wawe na sauti moja, hata baada ya kurejea madarakani. Haikuwasaidia kupata hekima ya kumaliza matatizo ya muda mrefu, kama ukosefu wa umeme ambao umezungumzwa tena na tena bila ufumbuzi.

Sasa kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, watawala wamerudi tena katika semina elekezi, chini ya mwelekezaji yule yule.

Walidhani zile zilishindikana kwa sababu zilifanyika Arusha. Sasa wamekimbilia Dodoma. Kwa wiki nzima, serikali iko Dodoma, imelala; inakula posho. Kazi zinakwama.

Rais naye, badala ya kuwaelekeza kwa hekima na ustadi, “akawananga” wasaidizi wake hadharani, kana kwamba huwa hapati fursa ya kukutana nao – wakati amekuwa akikutana nao kila mwezi katika vikao vya Baraza la Mawaziri. Ndio hao aliowatembelea na kuwasema wizarani kwao miezi miwili iliyopita, hata akawaamuru wengine waache ubabe.

Alitaka kuonewa huruma. Alitaka kuwashitaki kwa wananchi – waonekane wabaya, awe mzuri.

Rais anawasema mawaziri wake kama watoto wadogo wanaohangaika kuelewa kitu kidogo anachowafundisha. Anawaonyesha wananchi kwamba ana mawaziri mizigo, mbumbumbu – ambao kazi pekee wanayofanya ni “kumwangusha” rais.

Anataka turudi kwenye propaganda za kijinga walizoimba miaka mitano iliyopita, kwamba rais pekee ndiye anachapa kazi, bali mawaziri wake wanamwangusha.

Anawaambia mawaziri wake kuwa kama hawawezi kazi “waondoke,” kana kwamba hajui uwezo wao, hajui waliingiaje, wakati ndiye aliyewateua na ndiye ana mamlaka ya kuwaondoa.

Anataka “watoke” waende kwa wananchi kufafanua mafanikio ya serikali yake. Haamini kwamba wananchi wana uwezo wa kuona mazuri na mabaya ya serikali – bila kusubiri taarifa za mawaziri.

Haoni kwamba serikali inayofilisika na kulazimika kukopa hata mishahara ya watumishi wake, inahitaji kubana matumizi na kupunguza ziara na posho nono za viongozi hao waandamizi.

Lakini pia, tunapowatazama watu wenyewe aliokuwa anawapa somo, tunabaki kujiuliza: Rais amepata wapi hekima hii ya kudhani ana uelewa mpana kuliko mawaziri wake?

Amesomea wapi huko wasikojua wao, alikopata hicho cha kuwafunda? Tunapowatazama baadhi yao tunagundua kwamba kama rais angekuwa na busara ya kujifunza kutokana na miaka mitano iliyopita, asingewaita mawaziri kuwafunda, bali angewaita ili wakae kama timu, awaombe ushauri, awasikilize, wampe mang’amuzi yao na mipango mkakati; naye baada ya kuwasikiliza na kuongeza maono yake, awapangie kazi na kuwadai matokeo baada ya muda kadhaa.

Au basi angeunda kikosi kazi cha wasomi waliokubuhu kutoka taasisi mbalimbali zinazoheshimika, akawakutanisha na wasaidizi wake, wote pamoja wakavuna maarifa ya ziada katika kuboresha kazi zao na kukosoa kasoro za huko nyuma.

Angejenga mazingira ya kuambizana ukweli, naye akaambiwa kasoro zake; hasa kwamba serikali imekosa mipango mkakati mbadala na hata hiyo iliyopo imekosa msimamizi makini.

Kitendo cha rais kulialia mbele ya wateule wake na wananchi kupitia vyombo vya habari si ishara ya ushupavu anaostahili kuwa nao kiongozi mkuu wa nchi.

Ndiyo! Tuliona wameinama na kushika tama alipokuwa anafoka. Lakini ana uhakika gani kwamba walikubaliana naye? Ana uhakika gani kwamba walimwona shujaa?

Na kwa kiongozi ambaye ameongoza nchi kwa miaka mitano kwa hotuba na matamko yasiyotekelezeka, anadhani mawaziri wake watamwamini na kumheshimu baada ya kufokewa hadharani Dodoma?

Labda, watamshukuru kwa kuwatengenezea mazingira ya kula posho za safari. Lakini naamini mawaziri wenyewe wanajua fika kwamba hawana sababu ya kusafiri hadi vijijini kila mara, maana huko kuna watendaji wa ngazi za chini wanaopaswa kusimamia kazi na kuleta taarifa kwa ngazi za juu.

Sasa kama rais anaagiza mawaziri waende wenyewe vijijini, hao watendaji wa mikoani, wilayani na vijijini kwenyewe watafanya kazi gani?

Hivi waziri aliyekaa katika wizara ile ile kwa miaka mitatu au zaidi, ana kitu gani cha kujifunza kwa rais aliyekaa madarakani kwa miaka mitano bila maono na mafanikio yanayoshikika?

Rais Kikwete ana mfano gani wa utendaji uliotukuka anaoweza kuutumia kuwasuta mawaziri wake? Aliacha urithi gani katika wizara alizowahi kuongoza kabla hajawa rais?

Ni nani anayejua matatizo, changamoto, na suluhisho la matatizo yake, kati ya waziri aliye kwenye wizara hiyo hiyo, na rais “anayeishi kwenye ndege?”Baadhi yetu tunajua kwamba mkwamo mkubwa wa kiutendaji unatokana na madaraka makubwa ya rais, nidhamu ya woga ya wasaidizi wake na utovu wa uzalendo wa baadhi yao.

Zipo taarifa kwamba siku hizi wasaidizi wa rais wameamua kumwambia yale anayotaka kusikia, kwa sababu anawafokea hovyo hovyo wanapomweleza asiyotaka, au wanapompa mapendekezo magumu.

Wanadai rais hataki kuambiwa asichotaka; nao hawako tayari kupoteza kazi zao.

Kwa mantiki hii, haiwezekani kwamba baadhi ya wasaidizi wa rais wana nafuu kuliko yeye? Kwanini tusiamini, basi, kwamba rais ndiye anawaangusha wasaidizi wake?





Yanga wampa uchifu Manji 
Sunday, 15 May 2011 20:54

Clara Alponce
WAZEE wa klabu ya Yanga jana walimkabidhi Mkuki, Ngao na Kigoda kama alama ya cheo cha uchifu kwa aliyekuwa mfadhili wao Yussuf Manji.Manji alikabidhiwa heshima hiyo na kamati ya wazee ya muafaka wa Yanga chini ya kiongozi wake Mzee Yahaya Akilimali.

Akizungumza kwenye hafla hiyo mama Shadia Karume alisema Manji amejifunza mengi Yanga na amerejea rasmi kwa ajili ya kufanya kazi ya kuijenga Yanga mpya.Mama Karume alisema," Manji anatakiwa kujua hasira, jazba hazifai namtaka asahau yote yaliyopita."

Mama Karume aliongeza kuwa kuna watu wengi waliofanya mambo makubwa na mazuri Yanga huko nyuma na Manji ni moja wao."Mume wangu ndiye aliyejenga jengo la Yanga hapa Dar es Salaam, lakini angejisikia vibaya kama lingeachwa na kuharibika bila ya kufanyiwa ukarabati kama aliousimamia Manji,"alisema Mama Karume ambaye pia alimtaka Manji kujenga jengo lingine la Yanga huko Zanzibar kwa sababu uwanja umeshapatikana.

Tukio hilo lilishuhudiwa na viongozi wa serikali akiwemo Jamal Rwambo, Mbunge Mussa Zungu, Mudhihir Mudhihir pamoja na wachezaji wa Yanga huku burudani ikitolewa na bendi za Msondo, Sikinde na Tanzanite

CHANZO: Mwananchi.


Rais wetu mpendwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushangaa hajambo.Sasa anashangaa kwanini kuna utitiri wa mabango yenye ujumbe dhidi ya rushwa lakini rushwa inaendelea kutawala katika wizara mbalimbali bila uoga.

Tell you what Mr President,jibu la kinachokushangaza ni rahisi sana.Kama wewe mwenye kila nyenzo ya kukabiliana na rushwa,na ambaye ulitangaza hadharani kuwajua wala rushwa ila uliwapa muda wa kujirekebisha-na wakagoma kujirekebisha,lakini unaogopa kuwachukulia hatua-unasuasua katika kutekeleza ahadi uliztoa mwenyewe,unatarajia nini kutoka kwa watu wasio na uwezo wala mamlaka ya kupambana na rushwa?

Wewe unashangaa na sie tunakushangaa pia.One thing for sure,rushwa haiwezi kumalizwa kwa Rais kushangaa.Kinachohitajika ni vitendo na sio kubembelezana katika semina elekezi zinazozidi kuwatwisha mzigo walipa kodi masikini.

Jaribu kuwa mkali kidogo,punguza kushangaa,fanya vitendo.

Habari kamili ni hii hapa chini

Kikwete ataka vita vya rushwa kwa vitendo

na Danson Kaijage, Dodoma

RAIS Jakaya Kikwete, ameagiza mabango yote ya kupambana na rushwa yanayobandikwa katika wizara na taasisi za serikali na za umma yaendane na matendo yanayofanywa na maofisa katika ofisi husika.

Alitoa agizo hilo jana alipokuwa akifunga semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa serikali iliyofanyika mjini Dodoma kwa siku saba.

Alisema wananchi wangependa kuona ukusanyaji wa mapato unaimarika na nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma inakuwa bora zaidi badala ya kujaza mabango mengi yasiyokuwa na faida.

Alisema wananchi wanatarajia kuona juhudi za mapambano ya kweli kwa kudhibiti mianya ya rushwa badala ya kuona mabango mengi bila kuwepo na juhudi za makusudi.

Rais Kikwete alisema kinachoshangaza ni kuona wingi wa mabago katika kila kona wakati rushwa inaendelea kutawala ndani ya wizara mbalimbali bila woga.

Aidha, alisema kutokana na kuwepo kwa rushwa kuanzia ngazi ya juu ni wazi kuwa rushwa itaendelea kutendeka hadi ngazi ya chini kwa kuwa misingi ya rushwa inaanzia ngazi ya juu na kushuka ngazi ya chini.

Aliwataka vingozi na watendaji wakuu hao, kuonyesha ujasiri mkubwa juu ya kupiga vita masuala ya rushwa badala ya kuoneana aibu na kufichiana siri.

Rias Kikwete alisema semina hiyo ambayo ilikuwa na mikakati ya kuimarisha utendaji ndani ya serikali inapaswa kuzaa matunda hasa katika mapambano dhidi ya rushwa.

Hata hivyo, alisema wananchi wanatazamia kuona viongozi wa ngazi ya juu wakiwa mfano mzuri wa utawala bora, kuheshimu Katiba, utawala wa sheria na nidhamu ya kazi na uwajibikaji.

Naye Katibu Mkuu Kiongozi, Philimon Luhanjo, alisema waliazimia mazimio 14 ambayo viongozi hao wanatakiwa kuyatekeleza na kuyawasilisha katika ofisi yake kila baada ya miezi mitatu.

Semina hiyo iliwashirikisha mawaziri, makatibu wakuu, manaibu makatibu wakuu na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.





Hongera sana kwa mdau Godwin Habibu Meghji kwa kuhitimu Shahada ya Uzamili ya Sayansi Katika Mawasiliano ya Teknolojia iliyobobea katika uongozi wa miradi,aliyotunikiwa na Bodi ya wadhamini wa vyo vikuu vya Maryland,nchini Marekani.Kwa niaba ya wasomaji wa tovuti hii nakutakia kila la heri nikiamini kuwa shahada hiyo itakuwa chachu katika jitihada zetu za kizalendo za kuitumikia Tanzania yetu mahala popote pale (yes,nchi yetu inajengwa ndani na nje ya nchi)

15 May 2011



Mbele is a docudrama film about the journey of a music artist "Albino Fulani" as he links up with his fellow Tanzanian artist LBT for a USA benefit concert tour (S.A.P - Save Albinos Project). Being an Albino person himself, this show will take you behind the scenes where you will see dramatic episodes on how Albino Fulani associate and interrelate

The benefit concert takes place yearly to help raise funds which help children with albinism in Tanzania and also to raise awareness. The docudrama will show you how the two artists face and overcome professional and personal struggles and obstacles to raise funds and make the benefit concert a success.

The first season consists of 10 episodes which is expected to air in major Television Networks in Tanzania, Kenya and Uganda. Please join and “like” us on our Facebook page http://www.facebook.com/pages/Mbele/128019230601306 where as a member you will receive inside information and you will be able to watch the previews, behind the scene photographs and updates before the public does.

Stay tuned for the official trailer to be released on May 20th 2011. Please join the above facebook page to be the 1st to watch and comment.

Your support is very much needed and appreciated.

Sponsors and media please contact [email protected]

Thank you.


Wakati wenzetu mnasherehekea timu "zenu" kama Manchester United kuchukua ubingwa,akina sie bado tupo na Simba na Yanga zetu licha ya ubabaishaji wao wa hali ya juu.Kanuni nyepesi ya kumudu kuzipenda klabu hizi kongwe za Tanzania ni kuweka hisia mbele ya busara/akili (putting emotions in front of common sense).

Kwa bahati ya mtende,wana Msimbazi tumepata fursa ambayo laiti tukiitumia vema basi tutapiga hatua kubwa ya kushiriki Ligi ya Mabingwa.Kwa sasa sitaki hata kufikiria itakuwaje kwenye Ligi hiyo,iwapo tutafanikiwa,maana timu zilizopo huko ni hatari.Anyway,kwa muda huu ngoja tushangilie habari hizi njema (hata kama ni ushindi wa mezani)

Simba yawang’oa Mazembe Afrika
• Sasa kuwavaa Wamorocco jijini Khartoum

na Mwandishi wetu, CAIRO, Misri


WEKUNDU wa Msimbazi, Simba ya jijini Dar es Salaam, imeshinda rufaa yake iliyokata dhidi ya mabingwa mara mbili mfululizo wa Ligi ya Mabingwa Afrika 2009 na 2010, TP Mazembe ya DR Congo.

Sasa TP Mazembe imeondoshwa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa kwa kosa la kumchezesha mchezaji batili.

Huo ni uamuzi wa Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Soka (CAF), baada ya kupitia rufaa iliyokuwa imewasilishwa na Simba, kupinga TP Mazembe kumchezesha Janvier Besala Bokungu.

Bokungu (22), beki aliyezaliwa Kinshasa, akiwa mchezaji wa TP Mazembe mwaka 2007, alihamia Esperance ya Tunisia kabla ya kurejea mwaka huu.

Kwa mujibu wa CAF, Kamati ya Mashindano iliamua kushughulikia suala la nyota huyo baada ya Simba kuwasilisha pingamizi kwamba amechezeshwa isivyo halali.

Kamati hiyo imebaini kuwa kwa TP Mazembe kumchezesha Bokungu, ilifanya kosa kwa mujibu wa kifungu namba VIII kinachohusiana na ulaghai. Aidha, kifungu kingine kilichoipa Simba ushindi ni ibara ya 24 na 26 inayohusu uhalali wa mchezaji na ibara ya 29 ya kanuni za michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwamba TP Mazembe ilimchezesha Bokungu ambaye bado ni nyota wa Esperance, kwani mkataba wake na wakali hao wa Tunisia, utafikia ukomo Juni mwaka huu, ingawa TP Mazembe wanasisitiza ni mchezaji wao halali.

“Janvier alifuata taratibu zote kuvunja mkataba wake na si Esperance wala Mazembe yenye tatizo na mchezaji huyu, kwa sababu amejiunga nasi kwa maridhiano,” alisema Meneja Mkuu wa Mazembe, Frederic Kitengie.

Simba chini ya Mwenyekiti wake Ismail Aden Rage, ilimkatia rufaa Bokungu, licha ya kung’olewa katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 6-3.

Katika mechi ya kwanza ambayo ilichezwa mjini Lubumbashi, Simba ilifungwa mabao 2-1 kabla ya kupigwa 4-1 kwenye marudiano Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Kutokana na maamuzi hayo, sasa Simba itakipiga na mabingwa wa Morocco, Wydad Casablanca jijini Khartoum, Sudan, ambako itapigwa mechi moja tu ili kumpata atakayeingia katika kapu la timu nane bora, ambazo zitacheza ligi ndogo.

Tayari zilizotinga nane bora ni Ahly ya Misri, Raja Casablanca ya Morocco, Enyimba ya Nigeria, Esperance ya Tunisia, MC Alger ya Algeria, Al Hilal ya Sudan na Coton Sport ya Cameroon.

Wakati Simba wakifurahia kushinda rufaa, wakali hao wa Morocco, nao wanafurahia kurejea kwenye michuano hiyo kwani tayari walishang’olewa na TP Mazembe kwa jumla ya mabao 2-1.

Wakati hali ikiwa hivyo, leo Wekundu wa Msimbazi Simba, wanatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa mwaka kwenye bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mwaka mmoja tangu uongozi wa Mwenyekiti Ismail Aden Rage kuingia madarakani.

Kwa mujibu wa Rage, mkutano huo utakuwa na ajenda za mawasilisho ya mapato na matumizi ya fedha za mwaka, sambamba na kuwasilishwa kwa bajeti ya mwaka ya Kamati ya Utendaji na mengineyo.

Alisema ni mara ya kwanza Simba kuwasilisha taarifa za mahesabu ya mwaka mapema, jambo ambalo walijiandaa kabla ya uchaguzi mkuu, ikiwa ni mojawapo ya mapendekezo yaliyomo ndani ya katiba.

Uongozi wa Rage uliingia madarakani Mei 9 mwaka jana, baada ya uongozi wa mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Hassan Dalali, kumaliza miaka mitatu ya uongozi wake.

CHANZO: Tanzania Daima

14 May 2011


Victoria Climbié (RIGHT) and her killer aunt Marie Therese Kouao

Hundreds of children being accused of witchcraft 'as belief in demonic possession spreads across the UK'
By Rob Cooper

Last updated at 12:36 PM on 14th May 2011

Hundreds of witchcraft abuse cases are going unreported across the country each year, it has been revealed.

Officials believe child protection officers are only tipped off in the most extreme cases when a child's life has been put in danger.

Just 38 cases have been reported in the last five years - and it is feared that they represent just the tip of the iceberg.Hundreds of children may be left to starve, beaten and having chili rubbed into their eyes.

Youngsters born with physical and mental difficulties are most at risk from abuse.Relatives often believe that the children are 'possessed' and the torture is carried out as a form of exorcism.

Extreme evangelical Christian churches - most prevalent in the Democratic Republic of Congo - have grown significantly in recent years and their influence is thought to have spread to groups in the UK.

A decade ago the death of Victoria Climbie suffered appalling injuries at the hands of her aunt and boyfriend who believed she was possessed by the devil, sparking huge public anger.
Victoria

The eight-year-old had 128 injuries on her body in a case described by a pathologist as one of the worst ever child abuse cases.

She tied up, hit with bike chains and attacked with lighted cigarettes.

As officials try to combat the extreme beliefs, social services have been issued with a new set of guidelines to help them deal with youngsters from religious and ethnic minority backgrounds who could suffer abuse, The Times revealed.

The Metropolitan Police are working on their scheme to deal with religious-based child abuse to place extra emphasis on dealing with tackling witchcraft and abuse.

Witchcraft is most often found in the Democratic Republic of Congo and surrounding countries.

Romain Matondo, who works at the safeguarding children programme at the Congolese Family Centre, north London, said often it is not biological parents who are the abusers.

He told The Times: 'At first maybe it is swearing and shouting at the child, what we would call emotional abuse.

'But if there is church involvement, it sometimes means it doesn't stop there, but becomes physical and very violent as the church tries to get rid of the evil spirit.'

He added that children can be slapped, starved or beaten with spoons all to get the spirit out.

A report yesterday revealed that it is the poorest children that are most at risk of beind told they are 'possessed' because relatives are more likely to be influenced by faith leaders.

SOURCE: The Daily Mail

13 May 2011


Napenda kuwafahamisha badiliko la anwani ya blogu
Blog title: SAUTI YA MNYONGE:

Asante
Malkiory William Matiya,
B.Ed.(Hons) (UDSM); M.Sc, P/Health (UTA, Finland)
Mobile: +358404623776



11 May 2011




Africa here we come! Birmingham set to tour Tanzania ahead of new season

By Sportsmail Reporter

Last updated at 11:11 AM on 11th May 2011

Birmingham are planning a pre-season trip to Tanzania in July.

The details have not yet been finalised but first-team coach Andy Watson and chief medical officer Ian McGuinness have travelled to Africa to inspect facilities

Birmingham are expected to undertake a four-day trip, with Tanzanian top-flight sides Simba or Yanga, or possibly both, providing the opposition at the National Stadium in Dar-es-Salaam.

Watson told the club's website: 'The people of Tanzania that we have met have been very hospitable and kind, and from what we've seen of the country so far it looks an amazing place.
'We have been made aware of just how much the Tanzanian people love their football - especially the Barclays Premier League - and when everything is fully in place we look forward to coming back in July and playing.'

SOURCE: The Daily Mail

Mwangalie huyo kijana (well,may be mzee.You can't tell the difference,can you?) wa kwanza kulia.Sidhani kama anayoongea Nape yanamwingia akilini.Na wa tatu kutoka kulia,mwanamama aliyeshika tama,ni kama aliamrishwa kuhudhuria mkutano huo.Sio kashfa au dharau,lakini ni wazi kuwa sura za wahudhuriaji zinatia huzuni.Zimejaa mawazo,hazionyeshi matumaini....yet wamehudhuria.Ukiwaangalia akinamama hao hapo chini,japo kuna kijitabasabu cha kujipa matumaini,lakini hizo flana za njano na khanga zimeficha mengi...ngozi zao zinaonyesha waziwazi namna maisha yao ya kila siku yalivyo magumu katika harakati za kupeleka mkono kinywani.


Lakini bado wanahudhuria mikutano ya porojo.Wanajua wanadanganywa,kwani huhitaji kwenda shule kujua una njaa ilhali anayepiga porojo ameshiba.Mng'aro tu wa ngozi ya Nape as opposed to msinyao wa ngozi za wasikilizaji wake unaelezea mengi.Wanaambiwa kuwa CCM imejivua magamba,sasa itaendeshwa kisayansi,sijui imekuwa mpya...lakini hawaambiwi ni kwa namna gani ugumu wa maisha ya walalahoi hao utapungua...ni lini nao watapata fursa ya kunawiri kama akina Nape....

Lakini bado wanahudhuria mikutano hii ya porojo.Ndio maana katika kichwa cha habari nimehoji: WAMEROGWA?

Picha kwa hisani ya Jamii Forums

10 May 2011



Kwa walioamini usanii wa CCM kuwa imeamua kujivua magamba wahesabu wameliwa.Sio tu ukweli kwamba joka linalojivua magamba linakuwa hatari zaidi bali pia ufahamu wetu wengi kuwa joka likijivua magamba haligeuki kuwa mjusi.Na kama baadhi ya wanasiasa wa upinzani walivyoelezea suala hilo la magamba,tatizo la CCM ni mithili ya kansa ya damu.Dawa yake pekee ni kifo,and sure will CCM die,sio kwa vile kimezeeka vibaya bali kwa sababu ni mkusanyiko wa walafi,waroho,majambazi,matapeli na mabazazi wa kisiasa.Putting it bluntly,ushirika wa wachawi kamwe hauwezi kudumu.Let's wait and see!

VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Viongozi ambao waliotajwa kuwa wanatakiwa kujiondoa kwenye uongozi au chama ndani ya siku 90 kwa kuwa ni “mafisadi wanaochafua sura ya chama mbele ya jamii,” ni Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge.

Kinyume na majigambo ya viongozi wa juu wa chama hicho, kuwa sharti watuhumiwa hao waondolewe kwenye vikao vya maamuzi, hadi sasa chama kimeshindwa kuwapa barua za kuwajulisha juu ya suala hilo.

Katibu Mkuu Wilson Mukama, katibu wa itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, John Chiligati wamekuwa wakishindilia kuwa “mafisadi lazima waondoke.”

Hata hivyo, Mukama aliwaambia waandishi wa habari juzi Jumatatu, jijini Dar es Salaam, “…hakuna mahali popote katika maazimio ya NEC panapotaja siku 90.”

Alisema, “Kama ni muda basi ni pale mwenyekiti wetu aliposema NEC ijayo. NEC hukutana kila baada ya miezi minne na kwa hiyo kama ni siku, basi ni 120 na siyo 90,” alieleza Mukama akijibu swali la mmoja wa waandishi waliotaka kufahamu ni lini chama hicho kitaandika barua na kukabidhi watuhumiwa.

Kauli ya Mukama kwamba hakuna mahali ambapo NEC imeagiza Lowassa, Rostam na Chenge waondoke ndani ya chama katika muda wa siku 90 zijazo, imekuja wiki moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukutana kwa faragha na Lowassa.

Taarifa za ndani ya chama na kutoka baadhi ya viongozi wa CCM, zinasema mazungumzo ya viongozi hao wawili yalijikita katika kile kilichoitwa “kujivua gamba” na kwamba Lowassa anamtuhumu Nape kusambaratisha chama chao kwa kuendeleza tuhuma katika mikutano ya hadhara.

Lowassa na Kikwete walikutana ikulu jijini Dar es Salaam, 25 Aprili 2011 baada ya kushindwa kukutana mjini Dodoma, 3 Aprili 2011 kama ambavyo Kikwete alikuwa ameahidi.

Katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari, Mukama alisema, “NEC ilitoka na maazimio 26. Azimio mojawapo linasema chama kiendelee na mapambano yake dhidi ya ufisadi na kwamba watuhumiwa wakitafakari, wajipime na kuchukua hatua.”

Alisema, “Sehemu ya hotuba ya mwenyekiti wakati akifunga mkutano ilisema tunatambua athari ya kukosekana maadili katika chama na tuendelee kupambana; na katika hili hakuna ajizi. Viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajitafakari, wajipime na wachukue hatua,” alisema Mukama akinukuu kauli ya mweneykiti wa CCM, Rais Kikwete.

Alipoulizwa ni watuhumiwa gani wa ufisadi kwa kuwa chama hicho hakijawahi kuwa na orodha yake, badala yake orodha inayofahamika kwa wengi ni ile iliyotolewa na kiongozi mkuu wa upinzani nchini, Dk. Willibrod Slaa, Mukama alisema, “…CCM ni taasisi kubwa yenye mfumo wake na miongozo yake; hivyo haitegemei orodha ya CHADEMA.”

Mukama alikuwa akijibu swali la Manyerere Jackton wa New Habari House. Alitaka kufahamu vigezo vinavyotumika kutambua mafisadi; na iwapo wataweza kumwondoa Kikwete ndani ya chama hicho kwa vile naye ametajwa katika orodha ya Dk. Slaa ya tarehe 15 Septemba 2007.

Hata hivyo Mukama aliendelea kushikilia kuwa chama chake hakiwezi kufuata orodha za vyama vingine, hasa CHADEMA.

Kwa upande mwingine Lowassa amenukuliwa akimtaka Kikwete kumdhibiti Nape kwa kuwa “anakivuruga chama” kwa hatua yake ya kusisitiza kuwa NEC ilipitisha maamuzi ya kuwataka wajiuzulu, wakati akijua fika kwamba hilo si kweli.

“Mkutano kati ya Lowassa na rais ulikuwa mfupi sana. Lowassa alimueleza Bwana Mkubwa (rais Kikwete), jinsi asivyofurahishwa na mwenendo wa Nape hasa jinsi anavyowatuhumu ufisadi. Alimsihi Rais Kikwete kumweleza hilo katibu wake mwenezi, Nape…,” ameeleza mtoa taarifa.

Kikwete, taarifa zinasema, alimhakikishia Lowassa kuwa “…hakuna lolote litakalotokea,” kauli ambayo imethibitishwa na Mukama katika mazungumzo yake na wahariri.

“Yule bwana (Lowassa) alimuuliza Kikwete, mnataka kunipa barua kwa kosa lipi? Nimefanya nini? Nini ambacho wewe hukifahamu,” anasema mtoa taarifa wa MwanaHALISI.

Gazeti hili limejulishwa na vyanzo vyake vya ndani ya serikali kuwa uamuzi wowote utakaochukuliwa na Lowassa, unaweza kuzidisha mgawanyiko ndani ya CCM.

Mara baada ya Lowassa kukutana na Kikwete, taarifa zinasema mbunge huyo wa Monduli alikutana na kufanya mazungumzo marefu na Peter Kisumo, mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya chama hicho.

Katika mazungumzo yao, Lowassa alionya kuwa CCM kiko hatarini kupasuka kutokana na kauli za Nape na mwenzake John Chiligati juu ya ufisadi na watuhumiwa wake.

“Huyu bwana anaua chama. Nakuhakikishia mzee Kisumo, hawa watu wakiendelea kunishutumu bila sababu, nitatoka hadharani na kujibu mapigo,” anaeleza mtoa taarifa akimnukuu Lowassa katika mazungumzo yake na Kisumo.

Naye Kisumo anaripotiwa kumhoji Lowassa, “Mbona ninyi marafiki wawili mnataka kusambaratisha chama?” Naye Lowassa alijibu, “Kheri iwe hivyo…”

Mwandishi wa gazeti hili alimtafuta Lowassa ili kuthibitisha walichojadili na Kikwete, lakini simu yake iliita bila kupokelewa.





Leo ni tarehe 10/05/2011,na deadline aliyotoa Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete,kwa Katibu Mkuu wa Chadema,Dkt Willibroad Slaa,na Mwenyekiti wa DP,Mchungaji Christopher Mtikila,imemalizika jana.Ridhiwani alitoa dealine ya siku saba kuwataka Dkt Slaa na Mtikila wamwombe radhi kufuatia tuhuma zao dhidi yake kuwa amekuwa bilionea kwa njia za kutilia shaka.

Ni mapema mno kubashiri chochote lakini habari ifuatayo inaweza kutoa mwangaza kuhusu uwezekano wa Ridhiwani kwenda mahakamani kama livyotishia au kutokwenda (which would imply tuhuma hizo dhidi yake ni za kweli).Soma kwanza habari yenyewe


Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka

na Janet Josiah

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.



Pasipo nia ya kufanya hitimisho lolote,nashindwa kumwelewa Ridhiwani anaposema "jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lenu..."Hivi sio Ridhiwani huyuhuyu aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari,ambapo pamoja na mambo mengine alikanusha tuhuma zilizotolewa na wanasiasa hao,na akawataka wamwombe rahdi vinginevyom angewafikisha mahakamani?Sasa kama jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lao (wanahabari) kwanini basi aliitisha mkutano nao na kuwaelezea same thing anachodai hakiwahusu?

Waandishi wa habari wana kila sababu ya kumhoji kama atawafikisha Slaa na Mtikila mahakamani au la.Kwanini?Kwa sababu,kwanza,alitamka hayo mbele ya waandishi hao hao wa habari,na pili,yeye ni mtoto wa Rais na ametuhumiwa kuwa bilonea kwa mgongo wa baba yake.Sasa hakuna Mtanzania asiyependa kujua kama madai ya wanasiasa hao ni zushi mtupu au yana ukweli ndani yake.

Wito wangu kwa Ridhiwani ni huu:TIMIZA AHADI YAKO YA KWENDA MAHAKAMANI.Tuhuma za wanasiasa hao dhidi yako si ndogo,kwani licha ya kukugusa wewe binafsi zinamgusa pia baba yako ambaye ni Rais wetu (na ambaye siku za karibuni ametangaza kuwa anadhamiri kuukalia kooni ufisadi).Usipokwenda mahakamani itaonyesha kuwa tuhuma hizo zina ukweli.

And to make matter even worse,Dkt Slaa na Mtikila wanaweza kukufungulia kesi ya kuwakashifu,kwani ulidai ni wazushi tu.Sasa kama sio wazushi then go to the court as you promised,bearing in mind kwamba wewe ni mwanasheria.

Enewei,tunasikiliza WHAT'S NEXT!

Ngoma inogire!



Ama kweli chozi limepata mliaji.Kila mara tunasikia Rais wetu kalia na watendaji hawa,au kasikithswa na watendaji wale.Kichekesho ni kwamba watendaji hao hawakujiteua wenyewe kuwa madarakani bali waliteuliwa na huyhuyo anayelalama.

Binafsi,nadhani tatizo sio watendaji dhaifu wanaopelekea Rais "kulia" nao kila mara bali tatizo la msingi ni Rais mwenyewe.Kiongozi dhaifu haishiwi visingizio.Kiongozi dhaifu haishiwi lawama.Na kiongozi dhaifu hakawii kudai hili limeshindikana kwa vile yule hakufuata maagizo.Kwanini asiwatimue?

Hizi semina elekezi ni mzigo mwingine kwa Watanzania,ambao hawastahili kubebeshwa gharama za posho za waheshimiwa hao kwa ajili ya semina kama hizo ilhali aliyawateua ana kila sababu ya kuwatimua,lakini hana nia wala uwezo (wa kibinadamu,sio uwezo anaopewa na Katiba).

Yaani hadi tutapofika hapo 2015 sijui hali itakuwaje.Lakini moja ambalo tuna uhakika wa kulikumbuka kuhusu Kikwete ni hivi "vilio" vyake dhidi ya watendaji aliowateua yeye mwenyewe.

Enewei,soma habari husika hapo chini:

Kikwete alia na mawaziri mizigo 
Monday, 09 May 2011 21:54


Habel Chidawali, Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na makatibu wakuu kujiamini katika utendaji wao wa kazi badala ya kutegemea maelekezo ya mamlaka zilizo juu yao.Alisema hayo jana alipokuwa akifungua semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali iliyofanyika katika Ukumbi wa St Gasper nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma.“Hadi leo sijui kwa nini hasa watu (mawaziri) wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na Serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili (wapinzani) ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari. Sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” alisema Kikwete.

Kuna wakati waziri mmoja aliwahi kunipigia simu na kusema 'Mheshimiwa Rais habari hii tuikanushe?' Nilichokifanya nilimwambia pima wewe baada ya hapo nikakata simu,” alisema

Rais Kikwete alisema kitendo cha mawaziri kukataa kutoa habari na kuwafanya maofisa habari wa wizara kuwa kama waandishi wa habari ni hatari kwa serikali.

Katika hotuba yake, Rais Kikwete aliwataka watendaji hao kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu ili kukwepa hasara inayoweza kutokana na uamuzi usiofuata kanuni na kuiaibisha Serikali.
"Ni muhimu kwenu kama viongozi mkajielimisha juu ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi katika sehemu zenu za kazi. Uhalali wa maamuzi mtakaoyafanya hupimwa na sheria," alisema Kikwete na kuongeza:
"Ukifanya uamuzi unaokinzana na sheria utahojiwa wewe binafsi lakini pia utaibebesha Serikali mzigo wa hasara na fedheha itakayotokana na uamuzi huo. Uamuzi usiofuata sheria unaweza kuwa na madhara kwa wananchi.

"Heshimuni Katiba na fuateni sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika utekelezaji wa majukumu yenu. Katika semina hii masuala hayo yatafafanuliwa na kuzungumzwa. Kadhalika, uhusiano wa Serikali na mihimili mingine ya dola yaani, Bunge na Mahakama utafafanuliwa."

Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuepuka kauli na vitendo vinavyoweza kuwafarakanisha na kuleta mgawanyiko katika Serikali ili kulinda dhana ya uwajibikaji wa pamoja.

"Viongozi na watendaji wakuu wa wizara hamna budi kujenga uhusiano mzuri na uwajibikaji wa pamoja. Haifurahishi kuona waziri na katibu mkuu au waziri na naibu waziri; naibu waziri na katibu mkuu au katibu mkuu na naibu katibu mkuu hawaelewani."

"Wanasemana na hata wanapingana hadharani, yaani mbele ya wafanyakazi. Baya zaidi ni pale wanapopingana katika vyombo vya habari kuhusu uamuzi au utendaji wa wizara au serikali kwa jumla. Hayo si maadili mema katika taasisi yoyote.

"Kama unaona vigumu kuuafiki ni bora kutoka. Hairuhusiwi kupinga taasisi ambayo wewe umo ndani kama mmoja wa viongozi wake. Ni vyema hili likaeleweka. Msitupe tabu ya kuulizana maswali na kuwasemea."
Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuwa mstari wa mbele kuzungumzia mafanikio ya Serikali ili kuziba midomo ya wapinzani wanaopita kila kona nchini na kuwaeleza wananchi kuwa haijafanya chochote.

"Sijui kwa nini hatuwi wepesi kuyasemea mafanikio mengi tuliyoyapata tukaacha wasiotutakia heri wanaosema hatukufanya kitu wasikike mpaka waonekane wanasema kweli," alisema.

Alisema hajui na hana majibu mazuri ya kwa nini Serikali imekuwa ikishindwa kuzungumza mambo mazuri yaliyofanywa katika kipindi cha miaka mitano na hata wakati mwingine kushindwa kuzungumza jambo hadi wampigie simu, kitu ambacho ni aibu.

Alisema kuna udhaifu katika kujipanga kwa wasemaji kutokana na kuchelewa kutoa taarifa au kukanusha habari ambazo zimekuwa zikitolewa na upinzani, jambo linalowafanya wananchi waamini kuwa ni kweli, kwani uongo ukizungumzwa mara nyingi hugeuka na kuwa ukweli.

“Unajua mimi sijui hadi leo ni kwa nini hasa watu wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari huku sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” aliuliza Kikwete.

Alikanusha madai kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika habari za upinzani na kuacha habari nzuri za serikali na badala yake akasema woga na urasimu uliowajaa wasemaji katika serikali, ndilo tatizo hasa kwa kuwa hawajui kuwa vyombo vya habari vinatafuta habari na kama wao hawatoi habari ni lazima waandike zile zinazotolewa na upande wa pili.

Katika hatua nyingine, Kikwete alisema kuwa anategemea kuona Serikali yake ikifanya kazi kwa umoja na ushirikiano mkubwa katika kipindi hiki cha miaka mitano na kwamba kushirikishana na kupeana habari iwe ndiyo dira ya maendeleo yao.

Sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini
Aliwataka viongozi hao kuacha umangimeza, badala yake watoke ofisini kujionea matatizo ya wananchi.
"Mawaziri na makatibu wakuu lazima mtoke. Hiyo ndiyo njia bora zaidi ya kujua mambo yahusuyo wizara zenu na ndiyo njia bora ya kuongoza: kuona wenyewe na kutenda," alisema Rais Kikwete na kuongeza: "Hii itawafanya mjiamini kuelekeza na pia mnaposimama mbele za watu na kusema. Msiwe mamangimeza. Tokeni, tembeeni kuona shughuli zenu. Tembeleeni wananchi muwafahamu, wawafahamu, mjue shida zao muwatatulie."

Alikemea tabia ya viongozi hao kushinda kwenye mitandao kila siku na kusoma ujumbe badala ya kwenda kuwatumikia wananchi vijijini.Alisema tabia hiyo haipaswi kuvumiliwa hata kidogo na akaonya viongozi wa namna hiyo wataishia kuwa wababaishaji na hatakwenda nao katika kipindi chake cha uongozi.

Mimi sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini, bali niliteua watu wanaoweza kukimbizana kwa kasi zaidi, ari zaidi pamoja na nguvu zaidi, kwani nataka kuwasikia mkichakarika huko kwenye miradi mlikopeleka fedha, siyo kupokea taarifa ofisini bila ya kujua fedha za walipa kodi zinatumikaje huko.”

Dawa ya mawaziri hawa ipo jikoni
Rais Kikwete pia aliwatahadharisha mawaziri ambao wamekuwa wakipinga kauli na miswada ya mawaziri wenzao, huku wengine wakiwa wanatoa siri za Serikali.Alisema kuwa watu wa namna hiyo dawa yao iko jikoni kwa kuwa kitendo wanachokifanya si kizuri ndani ya Serikali.

Alisema anayo mamlaka ya kuchagua na ya kumwondoa waziri wakati wowote akiamua, hasa kama haoni umuhimu wa kuendelea na mtu wa aina hiyo.

“Katika hili nawaambia mapema kabisa kuwa waziri anayeishi kwa kupinga miswaada ya Serikali ajue kuwa anaipinga Serikali na hivyo sitakuwa tayari kufanya kazi na mtu wa aina hiyo. Sehemu kubwa ya kazi zenu mawaziri nataka ziwe za Serikali na zile za jimbo mtajua namna mtakavyojipanga bila ya kuharibu kazi za Serikali,” alisema.

Pato la Mtanzania litakua miaka mitatu ijayo
Rais Kikwete alisema kasi ya kukua kwa pato la Mtanzania ni ndogo na kwamba kunahitajika juhudi za makusudi katika kuongeza pato hilo. Hata hivyo, alitamba kuwa pato la Mtanzania litaongezeka katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa kutokana na baadhi ya nchi wahisani kuahidi kuongeza misaada kwa Tanzania.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, umaskini umepungua kwa asilimia mbili tu hivyo, akaahidi kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya awamu ya pili ya uongozi wake, umaskini utapungua kwa kiasi kikubwa.

Alisema mkakati uliopo hivi sasa serikalini ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025, Tanzania inakuwa nchi yenye uchumi wa kati pato la Mtanzania wa kawaida likitarajiwa kufikia Dola za Marekani 2,500 hadi 3,000. Sasa ni Dola 600. Kuhusu kipindi cha miaka mitatu, alisema kuwa, ipo mipango mizuri kutoka kwa wahisani, ikiwamo Benki ya Dunia ambayo imekubali kuisaidia Tanzania kiasi cha Dola 2.8 milioni ambazo zinaweza kusaidia katika kutengeneza ajira na kupambana na umaskini.

Semina hiyo ilihudhuriwa na watendaji wote wa Serikali wakiwamo Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, mawaziri na manaibu waziri, makatibu na naibu makatibu wakuu, Mwanasheria Mkuu na naibu wake, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na viongozi wastaafu, akiwamo Spika wa zamani na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya

CHANZO: Mwananchi

9 May 2011


Baada ya Rais Jakaya Kikwete kuonekana kituko kwa kupokea hundi yenye tarakimu zinazokinzana na thamani ya hundi hiyo kwa maandishi,na yeye kuonekana akitoa tabasamu la nguvu (trademark yake),sasa imekuwa zamu ya mkewe.

Ukiangalia hundi anayokabidhiwa Mama Salma Kikwete (pichani juu) utabaini kuwa thamani ya hundi kwa maandishi ni shilingi milioni tatu na laki nane,ambayo kwa tarakimu inapasa kuwa 3,800,000.Sasa sijui ni umaimuna au uzembe tu,tarakimu za hundi hiyo zimeandikwa kichakachuaji- TZS 3,800,00.Unaweza kudhani ni shilingi elfu tatu mia nane (3,800.00) lakini maelezo ya hundi yatakusuta kwani yametamka bayana kuwa ni SHILINGI MILIONI TATU NA LAKI NANE.

Na hapa chini tunamwona mtu tuliyemkabidhi dhamana ya kutuongoza Watanzania takriban milioni 50 akikenua meno kwa furaha huku hundi imeandikwa TWO HUNDRED THOUSAND lakini tarakimu ni 300,000



Hivi kabla ya hafla hizi, hao jamaa wa  PSU  hawakagui vitu anavyokabidhiwa Rais au mkewe?Au nao hadithi ni hiyohiyo?

Na haya ni madudu nadra tunayobahatika kuyaona hadharani.Je yanayofanyika kwa kwa faragha ua sirini inakuwaje?Npatwa na wasiwasi kuwa hadi Kikwete anaondoka madarakani hapo 2015 (kama hatoombwa na mafisadi kugombea tena ili aendelee kuwalinda) tunaweza kushtukia Tanzania ishauzwa zamani hizo.Unashangaa nchi inawezaje kuuzwa?Waulize "Zaire" (DRC Kinshasa)!!!!

Chanzo: Nimkutana na habari hii kwa ndugu yangu MPAYUKAJI MSEMAOVYO

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.