14 May 2010

Picha kwa Hisani ya SARAH wa Angalia Bongo.

Bila shaka ushaskia msemo wa Kiswahili 'Kufa Kufaana'.Nadhani kwa kimombo ndio tunachoita 'blessing in disguise'.Na ndivyo inavyoelekea kutokea katika sakata la 'ugomvi' kati ya msanii T.I.D na supastaa wa mpira wa kikapu,Mtanzania Hasheem Thabit,anayechezea timu ya Memphis Grizzliers kwenye ligi maarufu ya NBA huko Marekani.Katika pitapita yangu mtandaoni nimekuta habari hiyo imeshadakwa na vyombo vya habari vya kimataifa.Why not wakati Hasheem ni jina kubwa huko Marekani?

Sasa yayumkinika kusema kuwa sakata hilo limemnufaisha T.I.D 'kiaina' kwa vile katika kuripoti habari hiyo jina lake pia limekuwa likitajwa kama inavyoonekana katika habari ifuatayo kwenye mtandao wa kituo cha runinga cha FOX MEMPHIS cha huko Marekani:

MEMPHIS, Tenn. - The agent for Memphis Grizzlies center Hasheem Thabeet has told the team that an alleged incident involving Thabeet and R&B singer T.I.D never took place.


FOX13 Sports Director Matt Stark spoke with Ugo Udezue, Thabeet's agent, by phone Tuesday night, and Mr. Udezue said the allegations that Hasheem had knocked out the singer were completely false.


Udezue acknowledged that Thabeet was in a nightclub last weekend when an altercation broke out, but that the Grizzlies center was in a private section of the club and being protected by three bodyguards at the time, which is the norm for Thabeet when staying in Tanzania. Udezue says his client was immediately removed from the club, and was stunned later to hear the allegations that he had been involved.


Udezue said he believes the singer made the story up as a publicity stunt, and to get his music played on the radio.


Habari hiyo imekamata kasi kwenye mtandao kama inavyoonyesha HAPA.Japo natambua kuwa msanii T.I.D  'ana jina' kiasi chake katika anga za kimataifa,lakini ni dhahiri tukio hili linaweza kuwa limemtangaza zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

I just hope ugomvi huo haukuwa publicity stunt na publicity iliyojitokeza kwa T.I.D ni coincidental tu.Otherwise,mastaa wa kimataifa wataendelea kukutana na zahma kama hizo kwani zinaelekea kuwa na manufaa kwa upande mmoja wa wahusika wa tukio.

Ama kweli kufa kufaana!

Kuna wakati najiuliza kwanini sie masikini wa kutupwa ni hodari sana kwenye matumizi ya ovyo ovyo.Moja ya kumbukumbu za serikali ya awamu ya nne ilikuwa kuongeza mishahara ya wabunge licha ya hali yetu mbovu kabisa ya uchumi.Sambamba na hilo ni utitiri wa magari ya kifahari ambayo kimsingi si miongoni mwa vipaumbele kwa taifa masikini kama letu.

Wakati sie tunaendeleza matumizi ya kutapanya huku tukitembeza bakuli kwa wafadhili,serikali mpya ya hapa Uingereza chini ya David Cameron imetangaza kuwa mishahara ya mawaziri itapunguzwa kwa asilimia 5 na hakutakuwa na nyongeza katika mishahara hiyo (pay freeze) kwa miaka mitano.Mshahara wa sasa wa Waziri Mkuu Cameron utakuwa pungufu ukilinganisha na mishahara wanayolipwa meya wa manispaa mbalimbali 61 (kila manispaa hapa inajipangia kiwango cha mishahara ya viongozi wao kulingana na uwezo wa manispaa husika.Kukupa picha nzuri,alichofanya Cameron ni kama JK angeamua alipwe mshahara pungufu kulinganisha na meya wa manispaa ya Temeke au Kinondoni...ah,naota tu.Afanye hivyo achekwe!!!?)



Yah,unaweza kusema hizi ni mbwembwe tu za serikali mpya,au manjonjo tu,lakini ukweli ni kwamba serikali makini ni ile inayoonyesha kwa vitendo kuwa inatambua hali inayolikabili taifa.Cameron ameingia madarakani wakati Uingereza ikiwa kwenye msukosuko wa uchumi,na moja ya vipaumbele vya serikali yake ni kurekebisha uchumi mapema iwezekanavyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la hapa,mshahara wa Waziri Mkuu Cameron umepunguzwa kwa pauni 7,500 na kubaki pauni 142,500.Mishahara ya Naibu Waziri Mkuu Nick Clegg na mawaziri wengine waandamizi itakatwa pauni 7,082 na kubaki pauni 134,565 huku mawaziri wa kawaida wakikatwa pauni 5,197 na kubaki pauni 98,740.Mishahara ya mawaziri 'wadogo' itakatwa pauni 4,707 na kubaki 89,435.Hatua hiyo ya kukata mishahara kwa asilimia 5 itaokoa pauni milioni 3.

Wakati hayo yanatokea,gazeti la Mwananchi lina habari kuwa nchi wahisani wanaochangia bajeti ya serikali yetu wameamua kuunguza mchango wao kwenye bajeti ya serikali kwa mwaka 2010/2011 kwa sababu mbalimbali, ikiwamo ni pamoja na kasi ndogo ya serikali katika kutekeleza mageuzi kwenye sekta za umma.

Taarifa ya wahisani hao iliyotolewa jijini Dar es Salaam juzi, inaeleza kuwa mwaka huo wa fedha, watatoa dola za Marekani 534 milioni sawa na Sh721bilioni, ambazo ni pungufu kwa Dola za Marekani 220 milioni sawa na Sh297 bilioni walizotoa mwaka 2009/2010.

Wahisani wa bajeti ya serikali ni Benki ya Maendeleo Afrika (ADB), Canada, Denmark, Jumuiya ya Ulaya (EU), Finland, Ujerumani, Ireland, Japan, Uholanzi, Norway, Sweden, Uswisi, Uingereza na Benki ya Dunia (WB) mwaka jana walichangia Sh1.9 trilioni katika bajeti ya serikali kupitia miradi ya maendeleo na mifuko ya kisekta.

Taarifa hiyo ilitaja maeneo ambayo serikali ilishindwa kufikia malengo kuwa ni mabadiliko ya haraka katika menejimenti ya sekta ya fedha za umma, mategemeo ya kuboreka kwa hali ya mazingira ya uwekezaji na uboreshaji wa huduma kwa kutoka sekta za umma.

Hii ni mara ya nne kwa wahisani hao kuiwekea ngumu serikali katika kuchangia bajeti yake kila inapofikia mwisho wa mwaka, kwa kushindwa kutekeleza mambo wanayofikiria wao kuwa ni muhimu zaidi katika maendeleo ya nchi.

Mwaka juzi wahisani hao waligoma kutoa fedha baada ya serikali kusuasua kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wakiwemo wa fedha za EPA mpaka zilipofunguliwa kesi kadhaa ambazo mpaka sasa zinanguruma mahakamani.

Tatizo la viongozi wetu sie ni porojo nyingi na ulaghai mwingi wa kisiasa.Majukwaani wanahubiri kama watu wenye uchungu kweli na nchi yetu,lakini matendo yao tofauti kama kiza na mwanga.Tunapenda kuishi kifahari wakati uwezo wetu ni duni kabisa.Yani kuna wakati naangalia msafara wa Waziri Mkuu hapa,kisha nikikumbuka misafara ya viongozi wetu wakuu nabaki na maswali mengi kuliko majibu.Hebu angalia video hii hapo chini inayoonyesha msafara wa Gordon Brown siku alipokwenda makazi ya Malkia Elizabeth (Buckingham Palace) kuwasilisha ombi lake la kujiuzulu.

13 May 2010

Ndoa ya Mkeka.Haya ni mambo ya pwani zaidi kuliko 'bara'.Kule kwetu Ifakara hakuna vitu kama hivyo,lakini maeneo kama Tanga,Dar,Bagamoyo,nk ndoa za mkeka 'zinakula sahani moja' kwa umaarufu kama ndoa 'za kawaida'.Actually,ilikuwa almanusra 'nipigwe ndoa ya mkeka' wakati nilipoishi Tanga kwa takriban miaka 15 ilopita.Unajua tena mambo ya ujana...ukiyaangalia wakati huu wa utu uzima inabaki kichekesho.Anyway,kwa kifupi ndoa ya mkeka ni mithili ya fumanizi kati ya wanaovunja amri ya sita pasipo minajili ya kuwa wanandoa,na 'katika kuwapa one-stop fundisho na ufumbuzi' wanafungishwa ndoa ya chap-chap.It's like "si mnapenda kuvunja amri ya sita kisirisiri?Okay,sasa tunawahalalishia mtende manyotenda for the rest of your lives"...lol!Tatizo ni kwamba ni nadra kwa ndoa za mkeka kudumu kwa vile huwa ni'za kulazimisha'.Yani hazina tofauti na stori kama binti 'anayejiachia' na kupata ujauzito ili aolewe na mpenziwe.It rarely works!


Well,makala hii inazungumzia 'ndoa ya mkeka ya kisiasa' kati ya chama cha wahafidhina (Conservatives) na kile cha Waliberali (Liberal Democrats) ambao kwa pamoja wameunda serikali ya mseto hapa Uingereza. 

Uamuzi wa kiongozi wa Conservatives kuunda serikali ya mseto na Liberal Democrats umepokelewa kwa hisia tofauti huku watu wengi wakitabiri kuwa mseto huo hauna maisha marefu.Kikubwa kinachopelekea utabiri huo ni itikadi za vyama husika sambamba na tofauti zao katika sera zao.Japo tumeambiwa kuwa moja ya sababu zilizopelekea kufanikiwa kwa mseto huo ni kwa kila chama "kukubali matokeo" kwa aidha kuelegeza au kuachana kabisa na baadhi ya misimamo yao,hiyo haimaanishi kuwa misimamo hiyo imepotea 'vichwani' mwa wafuasi wa vyama hivyo.

Wakati wahafidhina wanafahamika kwa mrengo wao wa kulia na kati-kulia (right wing or centre-right politics) waliberali ni maarufu zaidi kwa mrengo wa kushoto na kidogo kati-kushoto (left wing or centre-left politics).Pengine hili sio rahisi sana kueleweka kama tukichukulia siasa zetu huko nyumbani kama mfano,kwani nadhani tunaweza kukubaliana kwamba nafasi ya mrengo katika siasa zetu huko Afrika ni ndogo sana.Yayumkinika kabisa kusema kuwa fedha za kukiwezesha chama au mgombea kununua kura ni muhimu zaidi kwenye siasa zetu kuliko mrengo wa chama au mgombea husika.Na hili ni tatizo kwa vile chama (au mgombea) kisicho na mrengo (au msimamo) ni sawa na bendera inayoweza kuelekea upande wowote ule kulingana na mvumo wa upepo.

Wenye hofu kuhusu 'ndoa ya mkeka' kati ya wahafidhina na waliberali wana sababu za msingi kwa vile mseto kati ya siasa za mrengo wa kulia na zile za mrengo wa kushoto hauko mbali sana na jitihada za kuchanganya maji na mafuta.Wakati chama cha Conservatives kinafahamika zaidi kwa siasa zake za kuwakumbatia matajiri huku zikiwakalia kooni 'walalahoi' kwa kudi kubwa (tayari kuna taarifa za 'kiama' cha kodi) waliberali wanafahamika zaidi kwa siasa za kuwa karibu na jamii huku vitu kama haki za binadamu,uvumulivu na ushirikiano vikiwa na umuhimu mkubwa.

Wakati Liberal Democrats walikuwa na sera ya msamaha (amnesty) kwa wahamiaji 'haramu' (illegal immigrants) huku wakisisitiza kuwa hatua kali dhidi ya wahamiaji hao si ufumbuzi kwa vile 'zinazidi kuwaficha msituni',chama cha Conservative kiliweka bayana msimamo wake wa kupunguza idadi ya wahamiaji kwa kuweka ukomo (cap) katika idadi ya wanaoingia/kuhamia Uingereza,sambamba na sheria kali za uhamiaji.Na katika hatua inayoweza kuwagharimu Liberal Democrats,chama hicho kimekubali kuachana na sera yake ya msamaha kwa 'wahamiaji haramu' na badala yake kimeafiki hatua ya Conservatives kuweka ukomo kwenye idadi ya wahamiaji wanaoingia nchini hapa.

Kuna tofauti ya kimtizamo kuhusu umoja na ushirikiano wa Ulaya.Wahafidhina wanasifika kwa upinzani wao dhidi ya suala hilo huku waliberali wakipendelea kuona ushirikiano huo ukisambaa zaidi ikiwa ni pamoja na wazo la Uingereza kutumia sarafu ya Euro badala ya Pound Sterling.Katika kufanikisha 'ndoa' yao,Liberal Democrats wamekubali kusitisha mipango yao kuhusu kukuza ushiriakiano wa Ulaya,jambo linaloweza kuwaudhi waumini wa siasa za chama hicho.

Lakini tayari kuna dalili za mpasuko kwenye 'ndoa hiyo ya mkeka' baada ya taarifa kwenye baadhi ya magazeti ya hapa kwamba 'Waziri' mpya wa fedha ((Kansela) George Osborne (wa Conservatives) amepinga vikali wazo kwamba 'Waziri' wa biashara (Business Secretary) Vince Cable (wa chama cha Liberal Democrats) ndiye atakayekuwa na dhamana ya kufanya mabadiiko kwenye mfumo wa mabenki (kwa minajili ya kudhibiti na kuzuwia uwezekano wa mtikisiko wa kifedha/kiuchumi kutokana na 'uzembe' wa mabenki katika utekelezaji wa sheria za fedha).Badala yake,hazina chini ya Osborne ndio itakayoshikilia dhamana ya utekelezaji wa sera ya mabenki na sekta ya fedha kwa ujumla.


Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kuna hofu kuwa chama cha Liberal Democrats kitakimbiwa na idadi kubwa tu ya wafuasi wake kufuatia uamuzi wake wa kushirikiana na Conservatives.Hali hiyo sio tofauti sana kwa upande wa wahafidhina kwani kuna idadi kubwa tu miongoni mwao wanaoona 'ndoa hiyo ya mkeka' kuwa jambo lisilofaa.Pengine tatizo kubwa kwa vyama vyote viwili ni wale walio 'mwisho wa upande' wa mrengo wa vyama hivyo,yaani wenye mrengo wa kulia kabisa kwa upande wa Conservatives na wa mrengo wa kushoto kabisa kwa upande wa waliberali.Hawa ni watu wanaoongozwa na imani na itikadi,na haiwaingii akilini kuona mambo hayo ya msingi yakiwekwa rehani kwa minajili tu ya kuunda serikali.

Lakini kuna wanaoona kuwa 'ndoa hii ya mkeka' kati ya David Cameron na Nick Clegg inaweza kudumu kwa vile kimsingi viongozi hao wawili wana mambo kadhaa yanayoshabihiana.Wote walisoma shule 'za bei mbaya',wanatoka familia zenye uwezo mkubwa kifedha na,kimsingi, wanaishi katika tabaka tawala.Kwa minajili hii,baadhi ya wachambuzi wanatabiri kuwa mfanano wa haiba za Cameron na Clegg,na sio tofauti katika itikadi zao,utafanikisha kudumu kwa serikali hiyo ya 'ajabu' kati chama chenye siasa za mrengo wa kulia (conservatives) na kile cha mrengo wa kushoto (Liberal Democrats).

Pamoja na yote hayo,siasa ni mchezo usiotabirika.Siku chache zilizopita ingekuwa jambo lisilofikirika kwa wahafidhana na waliberali kushirikiana katika uongozi wa serikali,lakini leo hii 'habari ndio hiyo'.Basi kwa minajili hiyohiyo,haitokuwa ajabu kwa 'ndoa hii ya mkeka' kudumu muda mrefu kuliko inavyotarajiwa.

Muda utatanabaisha (time will tell).

11 May 2010




Gordon Brown has just announced on live tv that he is stepping down as the Prime Minister.It's now clear that the next PM shall be David Cameron.

. http://goo.gl/5bKK.

Shamsi Vuai Nahodha.Huyu ni Waziri Kiongozi huko Zanzibar.Naomba kukiri hadharani kuwa kwa muda mrefu nimekuwa nikimuona mwanasiasa huyu kama 'yupo yupo' tu.Unajua kuwa mwanasiasa au kiongozi kunapaswa kuendana na mchango wa namna flani kifikra au kimatendo.Nyerere hakumbukwi kwa vile tu alikuwa mwanasiasa au kiongozi bali jitihada na mchango wake kwa umma,hata kama baadhi ya maeneo alikosea (hiyo ni makala nyingine: ALIPOKOSEA NYERERE).
Pasipo kutarajia,Nahodha kanipa 'surprise ya nguvu'.Ameongea maneno ya busara sana kuhusu fikra potofu zilizotawala akilini mwa viongozi wengi wa CCM kuwa chama hicho kitatawala milele.Japo si dhambi kwa chama kutawala milele (kama inawezekana na kama kinakidhi matakwa ya kinaowaongoza),ni uzembe wa tafakuri kuamini kuwa CCM itatawala daima hasa kutokana na uswahiba wake na ufisadi,kauli za kibabe hata kwenye mwaka wa uchaguzi na kupuuza watu waliokiweka chama hicho madarakani.Sasa,Waziri Kiongozi Nahodha amewatahadharisha wana-CCM wenzake kwamba KUNA SIKU CCM ITANG'OLEWA.Hebu msome hapa chini
Nahodha: Iko siku CCM itang'olewa


• AKUMBUSHA WAJIBU WA VIONGOZI KWA WANANCHI
na Mwandishi Maalum, Mererani
WAZIRI KIONGOZI wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha amewataka wana CCM kuacha kujidanganya kwamba chama chao kitaendelea kutawala milele.
Nahodha, mmoja wa viongozi wa juu wa CCM na serikali alitoa kauli hiyo jana wakati akiwahutubia wananchi katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Rafiki Child Care kilichoko Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.

Kiongozi huyo ambaye kimamlaka ni wa pili baada ya Rais Amani Karume katika SMZ aliwataka wana CCM kuachana na dhana kwamba chama chao hakiwezi kuondolewa madarakani na vyama vya upinzani.

“Ninatofautiana kimtazamo na watu wanaosema kwamba CCM itaendelea kutawala milele na milele, hapa kama hatutajipanga vizuri ipo siku chama chetu kitang’olewa madarakani…tusibweteke,” alisema Nahodha.

Waziri Kiongozi alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Katibu wa CCM wilaya ya Simanjiro, aliyetajwa kwa jina moja la Mujungu kuhutubia na kutamka kuwa, CCM haiwezi kuondolewa madarakani na vyama vya upinzani.

“Wapo wana CCM ambao kimtazamo wanaona sisi ndiyo wenyewe, kumbe wenye chama ni wananchi wanaowatawala. Tuna kila sababu ya kuwa makini katika utelezaji wa majukumu yetu… jambo hili nawaambia si kweli,” alisema Nahodha.

Akitoa mfano, Nahodha aliwataka wana CCM kujifunza kutoka katika nchi jirani ambako baadhi ya vyama vilivyopigania uhuru kama ilivyo CCM vimeng’olewa madarakani.

Alikitaja chama cha Kenya African National Union (KANU) ambacho kilipigania uhuru wa Kenya kuwa mmoja wa vyama vilivyopata kung’olewa madarakani.

“Kumbukeni namna ambavyo KANU ilisambaratika kule Kenya… leo hii imesahaulika kabisa. Lakini si huko tu, kule Zambia (UNIP) na Malawi (MCP) vyama tawala vilibwagwa vibaya na sasa vimesahaulika masikioni mwa wananchi,” alionya Nahodha.

Akiendelea, alisema ni wazi ipo siku wananchi wanaweza kukichoka CCM na kukibwaga iwapo viongozi watashindwa kutimiza ndoto za wananchi za kuwaletea maendeleo.

“Kuna mwanafalsafa mmoja mmoja anasema, msitafute uzuri wetu kwa kuangalia jinsi tulivyo, bali kwa kuangalia yale mema tuliofanya,” alisisitiza Nahodha.

Alisema uwajibikaji wa baadhi ya viongozi wanatokana na CCM ndani ya CCM unatia shaka inayoweza kuwafanya wananchi kukichukia chama hicho.

Alisema jukumu kubwa la viongozi wanaotokana na CCM ni kutekeleza majukumu yao kwa Watanzania kwa kuyafanya maisha yao yawe bora zaidi.

“Yuko mwanafalsafa mmoja wa zamani, aliwahi kusema maneno haya: ‘Tutakapokufa msitutafute katika makaburi yetu yaliyotengenezwa vizuri kwa chokaa bali mtutafute katika nyoyo za watu tuliowasaidia’. Ninawashauri viongozi wenzangu wa serikali na chama tuitumie sana busara ya mwana falsafa huyo,” alionya Vuai.

Katika hatua nyingine, Nahodha alieleza kusikitishwa na kuibuka kwa malumbano ya kisiasa miongoni mwa viongozi katika mkoa wa Manyara akisema hali hiyo haina faida kwa wananchi wanaowaongoza.

Kauli hiyo ya Nahodha iliyoonekana kuzungumzia na kukerwa na malumbano yaliyoibuka wiki iliyopita kati ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Henry Shekifu na Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka


Inaelekea habari kwamba raia mmoja wa India ameweza kuishi kimiujiza kwa kwa kutokula au kunywa chochote kwa miaka 70 sio fiksi bali ni kweli kabisa.Prahlad Jani ameimshangaza timu ya wanajeshi waliokuwa wakimchunguza kwa wiki 2 sasa kuthibitisha madai hayo.

Mtu huyo amekuwa chini ya uangalizi katika hospitali moja katika jimbo la Gujarat huku madaktari wakifuatilia kila jambo kwa kutumia kamera na CCTV.Kwa muda wote huo,hajawahi kula au kunywa chochote wala kwenda msalani.

"Bado hatufahamu ni namna gani anaweza kustahimili",anasema mtaalam wa mfumo wa fahamu Sudhir Shah alipoongea na waandishi wa habari baada ya uchunguzi huo."Bado ni muujiza usioweza kuelezeka kisayansi".

Prahlad,mwana-Yoga (Yogi) mwenye nywele ndefu na madevu aliwekwa hospitalini ili kuchunguzwa na taasisi ya utafiti na maendeleo ya ulinzi ya India (DRDO),ambapo ilitarajiwa kuwa matokeo ya uchunguzi huo yanaweza kusaidia kuwasaidia wanajeshi kumudu kuishi bila kula au kunywa chochote (kwa mfano wanapokuwa vitani),wanaanga na hata kuokoa maisha ya wengi yanapotokea majanga ya asili.

"Muda pekee Jani aligusa kimiminika ni wakati anasukutua na kuoga kwa vipindi maalum wakati wa uchunguzi huo",anasema G. Ilazavahagan,mkurugenzi wa taasisi ya ulinzi ya saikolojia na stadi shiriki (DIPAS).

Mtu huyo sasa amerejea kijijini kwake Ambaji,kaskazini mwa Gujarat,ambako ataendelea na taratibu zake za Yoga na uwazo (meditation).Anasema alipata karama alizonazo udogoni  kutoka kwa 'mungu wa kike' na tangu wakati huo amekuwa na uwezo wa ajabu.

Katika uchunguzi huo wa siku 15 uliohitimishwa Alhamisi iliyopita,madaktari walichukua vipimo (scans) vya viungo,ubongo na mishipa ya damu pamoja na vipimo (tests) vya moyo,mapafu na uwezo wake wa kufikiri.Matokeo zaidi ya uchunguzi wa vinasaba (DNA analysis),molekyuli za kibiolojia na vipimo vya homoni zake,enzymes na uzalishaji nishati mwilini (energy metabolism)  utatolewa hapo baadaye.

"Kama Jani hazalishi nishati ya mwili kutoka kwenye chakula na maji basi anapata nishati hiyo kutoka vyanzo vingine vinavyomzunguka kama vile mwanga wa jua",anaeleza Shah."Kama wataalam wa utabibu hatuwezi kufumbia macho uwezekano wa kuwepo vyanzo vingine vya nishati ya mwili zaidi ya kalori".

Habari hii imetafsiriwa kutoka AFP.

10 May 2010










Picha kwa Hisani ya Daily Mail

The British Prime Minister Gordon Brown has made a brief statement that he will stand down as Labour leader,and urged his party to start a process of electing his replacement.That means if the Conservative-Liberal Democrats power discussions on a possibility of  sharing deal bear no fruits,and the Liberal Democrats then agrees with Labour to form a a coalition government,the next PM might not be Gordon Brown,or David Cameron,for that matter.

Jambo moja nililojifunza kutoka kwa hawa wenzetu wa nchi zilizoendelea ni kile kinachoelezeka vizuri kwa kimombo kama not settling for less.Yaani,kwa tafsiri isiyo rasmi,ni kutokubali kuridhishwa na pungufu ya matarajio kamili.Kama ni mwanasiasa na wananachi wanaona 'unawazingua' basi usitarajie kuwa wataendelea 'kukulea'.Kama ni kwenye soka,wenye timu hawatarajii pungufu ya ushindi.

Baada ya matokeo yasiyoridhisha kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Alhamisi iliyopita,tayari 'bundi' mbaya ameshaanza kukiandama chama cha Labour.Baadhi ya wanasiasa ndani ya chama hicho wamejitokeza hadharani kutaka Gordon Brown atoswe kwa madai kuwa yeye ndio hasa chanzo cha matokeo mabaya kwenye uchaguzi huo ambapo Labour iliambulia nafasi ya pili nyuma ya chama cha wahafidhina (Conservative Party).

Japo hadi sasa Brown hajatamka kama ataachia ngazi uongozi wa chama hicho lakini dalili ni kwamba presha ikiendelea kuongezeka hatokuwa na jinsi zaidi ya kujiuzulu.Hapa sizungumzii u-waziri mkuu bali hali ya mambo ndani ya chama cha Labour.

Kukurejesha nyuma kidogo,Labour imekuwa na makundi mawili 'yasiyoiva' kwa kitambo kirefu sasa.Kwa upande mmoja ni wale wanaofahamika kama Blairites,ambao wanamhusudu Waziri Mkuu wa zamani Tony Blair,na kwa upande mwingine ni Brownites,ambao wanamhusudu Gordon Brown.Inasemekana kuwepo kwa makundi hayo kumechangia kwa kiasi flani matokeo mabaya ya chama hicho katika uchaguzi uliopita.Inadaiwa kwamba mmoja ya watu wenye nguvu kubwa ndani ya Labour,Lord Mandelson,alitumia kampeni za Brown na Labour kumuimarisha David Miliband,'Waziri' wa Mambo ya Nje wa Uingereza na chaguo la Blairites kumrithi Brown.Inaelezwa kwamba wakati Labour wanazindua kampeni zao kwa ajili ya uchaguzi huo,Mandelson (maarufu kama Malaika wa Giza-Angel of Darkness-ndani ya Labour)alifanikisha safari ya Miliband kwenda Marekani kwa mazungumzo na Rais Obama,fursa ambayo wachambuzi wa siasa wanaamini ingemwezesha Brown kuonekana kama kiongozi mwenye nguvu katika siasa za kimataifa.

Inadaiwa pia kuwa kampeni ya Brown iligeuzwa na Mandelson kuwa 'makao makuu ya Miliband' kwa maana kuwa ilikuwa ikitumika kwa namna flani kumpromoti mwanasiasa huyo (Miliband) ambaye bado ana ukaribu mkubwa na Blair.Hata meya wa zamani wa jiji la London,Ken Livingstone ameligusia hilo katika makala yake aliyoandika kwenye gazeti moja la Daily Mail.

Kwa sasa,harakati zinazoendelea chini chini ndani ya Labour ni za kumrithi Brown.Yani imekuwa kama ndugu za mgonjwa wanapoanza kugombania urithi kabla mgonjwa huyo hajaaaga dunia.Alosema siasa ni mchezo mchafu hakukosea.Baadhi ya majina yanayohusishwa na mpambano huo ni pamoja na akina Miliband,yaani David na mdogo wake Ed,ambaye ni waziri wa mazingira,Ed Ball- 'waziri' wa elimu na 'waziri' wa mambo ya ndani Alan Johnson.

Na akina Miliband  wanazua mvutano ambao unavuka anga za siasa kwa vile wakati David (pichani kushoto) ni Blairite,mdogo wake (kulia) ni Brownite.Inaelezwa kuwa tayari Ed ameshamfahamisha mama yao kuwa anadhamiria kupambana na kaka yake kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Labour.Hata hivyo,inaelezwa pia kuwa bado yuko njia panda kwa vile kwa upande mmoja Brownites wenzie wanamwona kama chaguo mwafaka kwa nafasi hiyo,lakini kwa upande mwingine 'damu ni nzito kuliko maji' na anatafakari kama pengine itakuwa jambo la busara kumsapoti kaka yake.

Tukiachana na mvutano huo wa kifamilia,'vita' kubwa inatarajiwa kuwa kati ya kaka yake (David) na (Ed) Balls.Wakati David anasifika kwa upeo na akili ya hali ya juu (ni Mwingireza mwenye asili ya Kiyahudi huyu) na ufahamu wake wa siasa za kimataifa hasa kutokana na wadhifa alionao sasa,Balls ana sapoti kubwa kwenye vyama vya wafanyakazi ambavyo kimsingi vina nguvu ya kutosha kwenye chama cha Labour.Kadhalika,wakati David anaonekana kama mtu wa 'tabaka la juu' Balls yuko karibu zaidi na wana-Labour wa ngazi za chini.

Tukiweka kando kidogo matatizo yaliyo ndani ya Labour kwa sasa,huko kwa wahafidhina nako mambo si shwari sana.Kuna wanaomuona mgombea wa chama hicho,David Cameron, kama amewaangushwa kwa kushindwa kwake kupata ushindi wa jumla (overall majority).Upinzani wa chini chini dhidi ya Camron haukuanza kwenye uchaguzi huu tu bali tangu alipoweka bayana dhamira yake ya kukibadilisha chama cha Conservative kutoka mwonekano wake kama 'chama kibaya' (nasty party) kwenda chama chenye kujumuisha makundi mbalimbali katika jamii.Kabla ya harakati za Cameron,chama hicho kimekuwa kikitafsiriwa kama 'cha Waingereza Weupe wa tabaka la juu' na kinachokumbatia zaidi mabwanyenye kuliko watu wa kawaida.

Cameron amefanikiwa kwa kiasi flani kubadili taswira hiyo japo si sana.Katika uchaguzi uliopita alihamasisha uteuzi wa baadhi ya wagombea kutoka makundi ambayo kimsingi 'hayamo kwenye akili za chama hicho' kwa mfano wagombea kutoka jamii ndogo za wasio weupe (ethnic minority),shoga na mabinti kadhaa.Japo baadhi ya wagombea hao wameshinda,wengi wao wamefanya vibaya na tayari baadhi ya wahafidhina wanamlaumu Cameron kwa uamuzi huo wa 'kuwapigia debe wageni wa tamaduni za chama hicho'.

Jingine linalomwandama Cameron ni mchango wa kundi dogo la washauri wake wanaofahamika kama 'wana-Eton wa zamani' (ex-Etonian),yaani marafiki zake wa karibu aliosoma nao katika shule ya Eton yenye hadhi ya juu kabisa na chaguo la 'wateule wachache' kwa hapa.Hao ni pamoja na Kansela ('waziri wa fedha') kivuli George Osborne na mwanamikakati anayesifika kwa akili nyingi Oliver Letwin (ambaye pia ni 'waziri' kivuli).Wengine wanaotuhumiwa 'kumshika akili' Cameron ni pamoja na kiongozi wa zamani wa Conservative,William Hague,na Mkurugenzi wa Mawasiliano,Andy Coulson (ambaye kabla ya kuchukua wadhifa huo alikuwa mhariri wa gazeti maarufu kwa udaku la News of The World).Coulson anafahamika kwa uwezo wake katika 'kutengeneza fitna,majungu na kummaliza mtu' (maeneo yanayolipa umaarufu News of the World).

Washauri hao wa Cameron wanatuhumiwa 'kumshauri vibaya' mgombea hasa katika wazo la 'jamii kubwa' (Big Society) ambalo inaelezwa kuwa liliasisiwa na Letwin.Wakosoaji wanadai kuwa wazo hilo halikueleweka kwa wapiga kura na wengine wanakwenda mbali zaidi na kulieleza kama 'wazo muflisi'.Vilevile,inaelezwa kuwa  Lord Ashcroft,'kibopa' aliyemwaga fedha nyingi kwa minajili ya Conservative kushinda uchaguzi huo,hajaridhishwa na matokeo ya uchaguzi huo,sambamba na 'kushindwa' kwa Cameron kusimama kidete kumtetea mhafidhina huyo tajiri (Ashcroft) alipoandamwa na skandali ya 'hadhi ya raia asiyelipa kodi kutokana na ukazi wake nje ya nchi' (non-domicile status).Lord Ashcroft anaamini kuwa suala hilo limechangia kupunguza kura za chama chao na anaamini kuwa Cameron angeweza kumtetea vizuri zaidi ya alivyofanya.Kadhalika,tajiri huyo anadaiwa kutopendezwa na wazo la Cameron kushiriki midahalo ya uchaguzi kwenye runinga,ambapo anaona kuwa ilisaidia kumuimarisha mgombea wa chama cha Waliberali (Liberal Democrats) Nick Clegg na hivyo 'kula' kura za Conservatives.

Nitaendelea kuwahabarisha kinachojiri kwenye anga za siasa za hapa kadri muda utavyoruhusu.

7 May 2010

Matokeo ya Uchaguzi Mkuu hapa Uingereza yametuacha baadhi yetu tukiwa na majonzi baada ya chama tawala cha Labour kuambulia nafasi ya pili (viti 258) huku chama cha wahafidhina (Conservatives) waikibuka mshindi kwa kupata viti 307 (japo ni pungufu ya viti 19 kwa viti 326 vinavyohitajika kuunda serikali ya peke yao).Chama cha kiliberali (Liberal Democrats) kimeshika nafasi ya tatu kwa kuambulia viti 57.

Kila mwenye majonzi kutokana na matokeo mabaya kwa Labour ana sababu zake binafsi.Zangu ni za kibinafsi zaidi (na mambo binafsi yanapaswa kubaki binafsi).Lililo bayana ni kwamba Labour haikushindwa kwa vile ni chama kibaya au kimeboronga wakati wa utawala wake.Hapana.Tofauti kati ya hawa wenzetu na akina sie na CCM yetu ni kwamba haitoshi kuwa umefanya vizuri tu bali watu wanataka vizuri zaidi kama sio vizuri kabisa.Bahati mbaya kwa Labour ni mtikisiko wa uchumi wa dunia ambao kama ulivyoathiri sehemu nyingine ulimwenguni,umepelekea idadi kubwa tu ya Waingereza wakiwa hawana ajira sambamba na ugumu wa wastani wa hali ya maisha.Kwa lugha nyingine,hali hiyo ya uchumi (ambayo kimsingi haikusababishwa na Labour) imechangia chama hicho kuangushwa na wahafidhina.

Hadi dakika hii haijafahamika nani atakuwa Waziri Mkuu kutokana na kanuni na taratibu za uchaguzi za hapa.Tofauti na huko nyumbani ambapo wingi wa kura unatafsiri ushindi wa moja kwa moja kwa chama husika,kwa hapa ili chama kiweze kuunda serikali kinapaswa kushinda viti 326.

Nitachambua zaidi baadaye kuhusu uchaguzi huu na namna Watanzania wanavyopaswa kujifunza kwa ajili ya uchaguzi wetu hapo Oktoba mwaka huu.Ila kuna habari ya 'kuliwaza' inayokihusu chama cha kibaguzi cha BRITISH NATIONAL PARTY (BNP) ambapo mwenyekiti wake Nick Griffin ameshindwa kumuangusha mgombea wa Labour,Margaret Hodge, katika eneo la Barking lililopo mashariki mwa jiji la London.

Habari njema zaidi ni kwamba BNP imepoteza viti vyote 12 ilivyokuwa inashikilia kwenye manispaa ya Barking and Dagenham jijini London.Pengine hili linaweza kutafsiriwa kama tamko la Waingereza dhidi ya siasa za kibaguzi.BNP ilitumia suala la uhamiaji kama ajenda yake kuu kwenye uchaguzi huo lakini ni dhahiri kuwa matokeo hayo yatafikisha ujumbe kwao kuwa watu wenye akili timamu hawaafikiani na ushenzi wa wabaguzi hao.

Mengi,baadaye.Kwa sasa tusubiri matokeo ya majadiliano ya simu katika ya mgombea wa wahafidhina,David Cameron na kiongozi wa waliberali Nick Clegg yanayotarajiwa baadaye leo kuangalia uwezekano wa ushirikianio kati ya vyama hivyo.Wakiafikiana,Cameron atafanikiwa kuwa Waziri Mkuu.Lakini kama Clegg ataamua kushirikiana na Labour basi Gordon Brown ataendelea kushikilia wadhifa wake.

6 May 2010

Leo ni siku ya uchaguzi mkuu hapa Uingereza.Vituo vya kupiga kura vilifunguliwa mapema asubuhi na inatarajiwa kuwa matokeo ya uchaguzi huo yatakuwa ya 'kukabana koo' kati ya vyama vikuu vya Labour,Conservative na Liberal Democrats.Hadi usiku wa jana,kura za maoni zilikuwa zikionyesha kwamba chama cha Conservative kingevuna viti vingi lakini visivyotosha kuunda serikali ZAIDI SOMA HAPA.

5 May 2010

Je una ndoto za kupata shahada ya juu?Basi jaribu shahada ya uzamifu (doctorate) ya ndoto,jambo linalotarajiwa kuwa halisi nchini Saudi Arabia. 

Yusuph al-Harthy,Msaudia mahiri katika kutafsiri ndoto,ana mpango wa kuanzisha taasisi ya kitaaluma itakayotoa shahada ya kwanza na ya uzalimi,na hata shahada ya uzamifu (PhD) katika ndoto na maono,kwa mujibu wa gazeti la Al-Hayat.

"Kutafsiri ndoto ni kwa asili yake ni njia ya kutoa ushauri nasaha,alisema Harthy ambaye anaendesha tovuti ya kufundisha namna ya kukokotoa maana ya ndoto.Taasisi anayotarajia kuanzisha kitashirikiana na chuo kikuu kimoja cha Uarabuni ambacho bado hakijatajwa.

Dini ya Kiislam ina historia ndefu ya kutafsiri ndoto,huku mwananzuoni wa aliyezaliwa karne ya 7,Muhammad Ibn Sirin,mwenyeji wa Basra katika Iraki ya leo,akitambulika kwa mchango wake wa kuhariri daftari (catalogue) za tafsiri za ndoto.

Harthy,ambaye hujadili ndoto kwenye vituo vya radio na shoo za runinga,haafikiani na mtizamo wa Wizara ya Saudia inayoshughulikia masuala ya Uislamu kwamba tafsiri ya ndoto sio sayansi inayoweza kufundishwa bali ni jambo linalotokana na hamasa (inspiration).

Imetafsiriwa kutoka tovuti ya Shirika la Habari la AFP


Latest voting intention 4th May

Tue, 04/05/2010 - 20:00
by Anthony Wells
Our latest daily polling figures for The Sun (fieldwork 3rd - 4th May; sample size 1,461) are:
Conservative 35%
Labour 30%
Liberal Democrat 24%
Others 11%

SOURCE: YouGov

Marc-Anotine Fortune, outjumps Steven Smith to head Celtic in front
Rangers' Maurice Edu is felled by Celtic's Andreas Hinkel


The airspace over Scotland and Ireland was closed last night because of an ash cloud in the atmosphere. Some ascribed that to the outpourings of a certain Icelandic volcano.




Those present in the east end of Glasgow on Tuesday night know better. It came from the dying embers of the Scottish season as they flared into life with the final Old Firm derby of the campaign.

This collision incorporated enough oddities for a lively quiz, although not Mastermind. The two goalkeepers who started did not finish, Allan McGregor departing the scene after only five minutes with a medial ligament injury and Artur Boruc leaving seven minutes after the break nursing two broken fingers.

David Weir, the Rangers captain, having won the first accolades of his career at the age of 40, capped an eventful passage by colliding with McGregor at the incident which saw the keeper stretchered off. After a lengthy stoppage, play resumed with a free kick awarded to Celtic for a foul committed by Kevin Thomson on Aiden McGeady.

The script called for Lee Naylor to test Neil Alexander with some form of direct effort from 25 yards, but the twist in the plot was that the Celtic full back kept his kick low and the Rangers defenders jumped, creating the gap through which the ball sped past McGregor's replacement, helped on by a deflection off the most unfortunate Weir.

Celtic Park erupted as it has rarely done in this dismal season for the club and the players responded by controlling proceedings with a passion and guile that has also been largely absent.
Neither Celtic nor Rangers, of course, can be sure who will be in charge of them when the new season opens, but the word on the pavement has been that Neil Lennon would emerge as prime contender to raise his status from caretaker manager if he could emerge from this fixture with the Parkhead side's first derby victory of the campaign.However, just when he was entitled to believe that his men would usher their narrow lead into the interval, the contest flipped.

In another peculiarity of the evening, each side fielded a makeshift centre back. Rangers had withdrawn Lee McCulloch from midfield to make up for the absences of Madjid Bougherra and Danny Wilson, the usual partners for Weir at the heart of the Ibrox back line. Celtic, meanwhile, had drafted Mark Wilson to cover for Josh Thompson, who made up the numbers on the bench.
It was Celtic's sticking plaster that peeled off first as Steven Whittaker made ground on the right to hang a cross into the box, where Kenny Miller beat Wilson to the jump for a glanced header between Boruc and his right hand post.

The Rangers forward then tempted fate and a caution – although he escaped censure from the referee – by making towards the Celtic support while kissing his badge – but it was the home support who savoured the last laugh within seconds as their team restored its lead with an identical strike.

In this case the overlapping full back was Naylor, the man on the end of the cross was Marc Antoine Fortune and the full back asked but unable to do a centre half's job was Steven Smith. Half time was enlivened by a repeated announcement declaring that an emergency had arisen within the stadium and instructing spectators to leave the stadium in an orderly fashion.

Having spent much of the season staying away from the place because of disdain at the fare on offer, the Celtic fans responded loudly that they had no intention of heading for the exits when their team had reached such a propitious juncture, thus providing proof that Bill Shankly might have been on the mark when he uttered his famous dictum about football and life and death.

The second half was almost inevitably an anti climax after what had gone before but there was still a slice of notoriety to be prised from the proceedings and it came when Lee McCulloch, who had been cautioned earlier, acquired another yellow card for a somewhat soft foul on McGeady. Off he went, on came members of the backroom staff on both sides to break up a mêlée.

Honour was eventually satisfied, the imbroglio calmed down and Celtic were able to celebrate their first triumph over Rangers in 15 months. Enough to earn Lennon the job? That's another tale for another time.


4 May 2010

Wiki moja baada ya kusherehekea mwaka wake wa 115 tangu azaliwe,binadamu mwenye umri mkubwa zaidi duniani amefariki katika kisiwa cha kaskazini mwa Japan cha Okinawa.Kama Chinen alizaliwa tarehe 10 ya mwezi Mei mwaka 1895 na kubahatika kushuhudia karne tatu tofauti,kwa mujibu wa wa taasisi ya utafiti wa vipengele (aspects) vya kijamii,saikolojia na baiolojia vya ukuaji wa binadamu (Gerontology Research Group)


Kikongwe huyo alifariki Jumapili iliyopita kwenye nyumba ya kutunza wazee/wagonjwa (care home)japokuwa taarifa za kifo chake hazijatolewa kwa nduguze ambao wamekuwa wakilinda faragha ya bibi hiyo kwa makini.

Kisiwa cha Okinawa kina sifa ya kuwa na wakazi wenye maisha marefu hali inayohusishwa na mlo wa asili wa mchaichai (green tea),supu ya 'miso',mbogamboga,wali na samaki.

Kama ameshikilia rekodi ya umri mkubwa duniani tangu mwezi Sptemba mwaka jana,baada ya kikongwe Gertrude Baines kufariki akiwa na umri wa miaka 115 huko Los Angeles nchini Marekani.Baada ya kifo cha Kama,rekodi yake sasa inabaki kwa bibi wa Kifaransa,Eugenie Blanchard,aliyezaliwa mwezi Februari mwaka 1896.Mwingereza Florence Emily Baldwin,wa Leeds,anashikilia nafasi ya pili akiwa na umri wa miaka 114 pia.Japo bibi huyo anasema kuwa kula sandiwichi ya mayai (egg sandwich)ndio siri ya kuishi kwake miaka yote hiyo,wataalam wanahisi maisha yasiyohusisha uvutaji sigara,unywaji pombe na kufanya kazi kwa bidii kumechangia zaidi.

Imetafsiriwa kutoka kituo cha runinga cha Sky


3 May 2010

Video courtesy of Michuzi Blog

Americans worry that illegal immigrants are putting a strain on schools, hospitals and the depressed job market but still are sympathetic to their plight.

Eight in 10 Americans, 84%, are very or somewhat concerned that illegal immigrants are burdening government services, and 77% worry that they are driving down wages, a USA TODAY/Gallup Poll finds.

Yet 77% are concerned that stricter immigration laws would mean illegal immigrants and their families who have lived productively in the United States for years would be forced to leave



"People seem to be more concerned about that than the hypothetical things like civil rights," Gallup pollster Jeffrey Jones said.

The seemingly contradictory sentiments reflect the difficulty in grappling with the immigration issue, said Tomas Jimenez, a fellow at the New America Foundation think tank and a sociology professor at Stanford University.

"On the one hand, they don't like the idea that people are breaking our immigration laws, that it appears we have a Southern border that is out of control," Jimenez said. "On the other hand, they think the people coming here who work hard, who have dreams of a better life, are really participating in an American tradition that is as old as this country."

The poll of 1,049 adults Saturday and Sunday has a margin of error of +/- 4 percentage points.

SOURCE: USAToday


.


Waziri Mkuu wa Australia,Kevin Rudd,amekuwa akifuatilia tovuti za ngono (porn sites),kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Sky. 


Rudd,hata hivyo,amekuwa 'mfuatiliaji' wa tovuti hizo kutokana na mapungufu katika nyenzo za usalama/udhibiti (setting) katika akaunti yake ya Twitter.Kutokana na mapungufu hayo,kiongozi huyo amekuwa akifuatilia watu kama bloga wa mambo ya ngono,duka linalouza bidhaa za ngono,mwanamama aliye kifua wazi huku amjifunga pingu,na kadhalika.

Msemaji wa Waziri Mkuu ameeleza kuwa tatizo hilo lilitokana na akaunti ya Twitter ya Rudd kufuata wale wote wanaomfuata (auto-follow those who follow him)."Japo Waziri Mkuu anajitahidi kutoa majibu kwa wale wanaosema chochote kwake,kazi hiyo ni ngumu ukizingatia idadi ya watu ni 900,000", alieleza msemaji huyo.

Japo inamhitaji mtumiaji wa Twitter kuangalia kwanza wasifu wa mtu anayeomba kukufuata,kuna kipengele kinachoiwezesha akaunti imkubali moja kwa moja mtu anayeomba kumfuata pasipo haja ya mwenye akaunti kufanya hivyo.Uwezo huo unaonekana kuwa muhimu kwa watumiaji wa Twitter wenye wafuasi (followers) wengi.Katika akaunti yake KevinRuddPM,Waziri Mkuu huyo ni mfuasi wa wana-twitter wengine 200,000.

Wataalam wa teknolojia wanatahadharisha kuwa nyenzo za habari kwa jamii (social media)zinaweza kuhatarisha usalama wa mtuamiaji kama hataokuwa makini."Kuna imani kwamba kwenye vitu kama Twitter unaweza tu kufungua akaunti na mambo yakaenda mwanana",anasema Handsley,makamu mwenyekiti wa kampuni ya Young Media Australia."Tunapaswa kufahamu kwa undani kuhusu usalama wa chanzo husika cha habari kwa jamii kabla ya kuamua kukitumia",aliongeza alipoongea na gazeti la Herald Sun.

Kwa mujibu wa gazeti hilo,baadhi ya wengine 'waliofuatiliwa' na Waziri Mkuu Rudd ni pamoja na tovuti ya kamera-mtandao (webcams) za ngono na mmiliki wa kiota cha watenda ngono wa jinsia moja (gay resort) cha Phuket,Thailand.

Rudd amekuwa mtumiaji mzuri wa teknolojia ya habari huku nyakati nyingine akitumia nyenzo kama Twitter kubainisha sera zake.

Imetafsiriwa kutoka Sky News

1 May 2010




Message from JESTINAI will be hosting a brand new talk show ALL ABOUT WOMEN.It explores issues and the progress made by women of Black origin who work and live in and outside London. The show is presented by Jestina George and Kayisha.On this show, the girls talk about everything from fashion to music and general gossip. The show will start showing on Sky Channel 184 BEN TV every monday 10:30 PM. The first show goes out on Monday the 3rd of May 2010. Also the show can be watched on AILTV just log on http://www.ailtv.com or you can purchase a set top box and watch the show and many other programs on a normal television set. For more info Please contact us [email protected] or call us on 07595040952

30 Apr 2010

Mtakatifu au mzushi?

Raia mmoja wa India amegusa hisia za jeshi la nchi hiyo kutokana na madai yake kwamba haitaji chakula wala maji kumudu kuishi.Prahlad Jani anadai yeye ni 'breatharia',yaani mtu anayeweza kuishi kwa kutumia nguvu za asili za kiimani.Anadai anapata nguvu hizo za asili kutoka kwa 'mungu wa kike' anayemmwagia kimiminika (elixir)cha miujiza katika paa la chini la mdomo wake (palate),kwa mujibu wa gazeti la Telegraph la London. 


Wakati baadhi ya watu wanamwona kama 'mzushi' flani,taasisi ya maendeleo ya utafiti wa ulinzi inasema Prahlad anaweza kutoa mwangaza katika kuwasaidia wanajeshi kumudu kukaa muda mrefu bila kula,au hata wahanga wa majanga mbalimbali.Hadi sasa amekaa siku sita bila kula au kunywa chochote katika hospitali iliyopo Hyderabad,na madaktari wanasema haonyeshi dalili yoyote ya kuathiriwa na njaa.

"Ikithibitika kuwa madai yakni sahihi,basi itakuwa hatua kubwa sana kwenye sayansi ya tiba",anasema Dkt G.Ilavazhagan,Mkurugenzi wa Taasisi ya Ulinzi ya Fiziolojia na Stadi Shiriki."Itatuwezesha kuokoa maisha ya wanadamu katika nyakati za majanga,kimo cha juu,safari za majini,na mazingira mengine magumu ya kibinadamu na ya asili.Tutaweza kuwaelimisha watu kuhusu namna ya kustahimili (surviving) mazingira magumu pasipo chakula na maji au chochote kile".

Madaktari wataendelea kumchunguza kwa siku 15 kipindi ambacho wanataraji kuona misuli yake ikisinyaa,upungufu mkubwa wa maji mwilini,kupungua uzito wa mwili na baadhi ya viungo vya mwili kushindwa kufanya kazi.

Binadamu wengi hawawezi kustahimili zaidi ya siku 3 hadi 5 pasipo kunywa maji.

Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily News la India.

29 Apr 2010

NEWSWEEK: Black blogs cover a far more diverse range of stories than the rest of the media. Just ask Sandra Bullock. While Sandra Bullock's post-Oscar split from husband Jesse James may be the biggest celebrity news in the last month (or two), it's probably not surprising it's the adopted brown baby that really got the African-American blog sites going. The funny thing is, black Web sites such as MediaTakeOut.com, Bossip, and Young, Black and Fabulous have been following Bullock for years. Part of the reason is her connection to the black community. "They know about her support for victims of Katrina and Haiti so they care about what happens to her, which we thought about when we gave her coverage," says Fred Mwangaguhunga, owner of the black entertainment site MediaTakeOut.com. But part of it is that black blogs look at the world differently than the often segregated mainstream.
. CLICK HERE TO READ THE FULL STORY

The US Army says that it is it is wasting far too much time preparing Powerpoint presentations and not enough time killing people.

For a while now the Army has been concerned that its officers are missing entire wars preparing Powerpoint slides and making presentations.

. TechEye has got its paws on the sort of slide they mean (see above). 

Last summer Gen Stanley McChrystal, the leader of US and Nato forces in Afghanistan, said when we understand that slide that “we’ll have won the war’.

Gen James Mattis of the Marine Corps, said: "Powerpoint makes us stupid". The Marines are not renowned for being that bright in the first place, which makes them some of the US's best soldiers, but Powerpoint sucks about the direction you want to point them.

Sam Nuxoll, a platoon leader in Iraq, seems to have shaken the Pentagon with a quote that said he was spending most of the war making Powerpoint slides. Instead of spending his time dodging bullets, he was making bullet points.

What is the problem is the fact that rather than encouraging making decisions PowerPoint sucks up the time of junior officers. The idea is that they can get crappy decisions blessed if it looks good in Powerpoint. However really good tactics which are dull on screen are being mothballed.

This has been noticed in business too with some companies thinking that Powerpoint presentations are a waste of time too.

.SOURCE: Tech Eye

JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.

. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.

Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.

Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.

Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.

Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.

Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.

Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda
kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.

Hata hivyo, Ustaadhi Ramadhan alisema anashangaa kuona idadi kubwa ya wanafunzi waliopata ajali, kwani aliowaruhusu kutoka chuoni hapo walikuwa 60 tu.

“Nashangaa sijui ni nini kimetokea, kwani niliowaruhusu kuondoka na gari
hilo ni wanachuo 60 tu, lakini idadi ya waliopata ajali imekuwa kubwa. Sijui walipandia wapi…,” alisema mwalimu huyo wa zamu.

Kanyinyi alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Raha Leo, Seleman Abdallah kwa kutoa dawa kwa ajili ya kuwatibu majeruhi wa ajali hiyo.

“Tunashukuru Mkurugenzi wa Raha leo, ametusaidia sana kwa kutoa dawa za
kuwatibu majeruhi na pia vifaa kwa ajili ya kusaidia kuhifadhia miili ya waliokufa,” alisema Kanyinyi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo alifika hospitalini hapo saa 5 .30 asubuhi na kuwapa pole ndugu wa wanafunzi waliokufa katika ajali hiyo.

Akiwa, akiwa katika wodi ya Galanosi Mkuu wa Mkoa huyo alimuagiza Kaimu Mganga Mkuu kuwaita waganga na wauguzi kutoka vituo vyote vya afya vya jijini hapa ili kuongeza nguvu, kwa vile waliopo katika Hospitali ya Bombo walikuwa wmezidiwa na kazi ya kuwahudumia majeruhi.

Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Riami alisema huo ni msiba
mkubwa uliwakumba Waislamu na Watanzania kwa ujumla, hivyo akaomba msaada wa hali na mali kuokoa maisha ya majeruhi waliopata ajali hiyo.

Ajali hii ni muendelezo wa ajali mbaya za barabarani zinazoendelea kutokea na kuua watu sehemu mbalimbali nchini hivi sasa.

Moja ya ajali hizo mbaya ni iliyotokea jijini Dar es Salaam mwezi uliopita na kuua watu zaidi ya 10 papo hapo baada ya lori la mafuta ya taa kuigonga na kulalia daladala maneo ya Kibamba katika Barabara ya Morogoro.

Katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri, daladala ilisagawa na kuwa kama chapati; na miongoni mwa waliokufa ni mama mjazito aliyekuwa anakwenda kujifungua hospitalini akiwa pamoja na mumewe.

CHANZO: Mwananchi
.

British National Party (BNP),chama cha kibaguzi cha hapa Uingereza,kimetangaza kwamba kitatoa paundi 50,000 kwa kila atakayeafiki kuhama Uingereza.Akiongea katika kipindi cha 'Today' cha kituo cha redio cha BBC4,mwenyekiti wa chama hicho,Nick Griffin (pichani) alisema kuwa mpango huo ni mahsusi kwa Waingereza wasio Weupe (non-White British) na wahamiaji wengine wasio weupe (non-White migrants).

Griffin alieleza kuwa kwa mujibu wa sera ya uhamiaji ya chama chake 'milango ya Uingereza itafungwa' kwa wageni isipokuwa tu kwa wale wenye ujuzi au taaluma maalum."Aidha unazungumzia fundi bomba wa ki-Polish au mkimbizi kutoka Afghanistan,milango ya Uingereza itafungwa kwa sababu nchi hii imejaa",aliongeza kiongozi huyo mbaguzi wa rangi.

Kiongozi huyo wa BNP alitanabaisha kuwa "Idadi ya watakaozuiwa kuingia nchi hii itakuwa yoyote na kutoka popote.Milango itafunguliwa tu pale itapokidhi mahitaji wa Waingereza na Uingereza".Akitolea mfano wa utekelezaji wa sera hiyo,Griffin alisema laiti Uingereza ikiwa na mahitaji ya wataalam wa nyukia basi chama hicho kitaruhusu,kwa mfano,mwanafikizia kutoka Japan.

Alipoulizwa kama sera hiyo itaambatana na kuvunja mikataba ya kimataifa,mbaguzi huyo alijibu: "Kabisa.Mikataba ya kimataifa haikidhi mahitaji ya Uingereza na watu wake.U-kimataifa (internationalism) ni miradi ya tabaka la wanasiasa".

Kuhusu kuwataka wasio weupe kuondoka Uingereza,Griffin alisema:"Tunasema tutatoa posho ya kuhama makazi (resettlement grants) na hili ni suala la hiari .Tunazungumzia takriban pauni 50,000 kwa kwa mtu".Alipoulizwa ni watu wangapi wanaotarajiwa kuhama Uingereza kwa mujibu wa sera hiyo alisema: "180,000 kwa mwaka,kama wataondoka katika nchi hii iliyojaa kupindukia".

Imetafsiriwa kutoka Yahoo! News


Judges are set to rule whether to remove the story of the intrepid explorer's first African adventure after a Congolese man claimed it is racist.

. Bienvenu Mbutu Mondondo wants Tintin in the Congo - the second in the celebrated children's series - to be axed for its ignorant depiction of native Africans.


Creator Hergé defended his book, first published in 1930, in later life and said any stereotypes merely reflected contemporary colonialist views.

The Belgian courts may follow a recent compromise decision in Britain and place a sticker warning of offensive content instead.

That was the result when the UK's Commission for Racial Equality called for the comic to be banned in 2007.

Mr Mondondo has put his case to Belgian and French judges before, but his latest legal challenge faces some scepticism.

Online comic magazine actubd.com accused him of lying about his profession, amid other doubts that he will be unable to pay his own lawyers.

SOURCE: Skynews

28 Apr 2010

China has revoked a ban on people with HIV/AIDS entering the country, softening a decades-old policy that drew sharp criticism this year when an Australian writer was blocked after declaring himself HIV-positive. Until now, China's regulations formally banned foreigners entering the country with "psychiatric illness, leprosy, AIDS, sexually-transmitted diseases, active pulmonary tuberculosis or other infectious diseases."


The State Council, China's cabinet, issued amended rules late Tuesday removing the explicit ban on people who have developed AIDS or are infected with the HIV retrovirus, as well as anyone with leprosy, while leaving authorities leeway to decide which diseases could trigger an entry ban.

The United Nations welcomed the decision as an important step towards ending discrimination against people living with HIV.

"I commend President Hu Jintao for China's decision to remove travel restrictions based on HIV status," U.N. Secretary-General Ban Ki-moon said in a statement.

"Punitive policies and practices only hamper the global AIDS response. I urge all other countries with such restrictions to remove them as a matter of priority and urgency."

Travel restrictions, which are imposed in some form by dozens of countries worldwide, do not prevent transmission of the disease or protect public health, the statement added.

China's new rules, posted on the central government website (www.gov.cn), still block foreigners "with serious psychiatric illness, infectious pulmonary tuberculosis or other infectious diseases that may constitute a major threat to public health."

The amended regulations did not say whether AIDS/HIV would be among the infectious diseases that people seeking Chinese visas must declare when applying, possibly leaving officials some leeway on how to apply the rule.

But an unnamed legal affairs official for the State Council indicated that AIDS/HIV would not be a bar to entry.

"Restricting foreigners with these diseases from entering the country has played an extremely limited role in our country's disease prevention and control work, and instead has repeatedly become an impediment to our hosting a variety of international events," the official told the Legal Daily.

In March, more than 90 Australian authors signed a letter decrying China's refusal to grant a visa to one of the country's most celebrated writers, Robert Dessaix, who is HIV-positive.

Friday, Shanghai opens its World Expo, a multi-billion dollar exhibition that is China's latest effort to promote an image as a forward-looking and open country.

The HIV virus can be spread through unprotected sex, sharing of infected needles and blood, and -- without preventive drugs -- to children in the womb of infected mothers or who take milk from an infected woman.

If untreated, the virus attacks the immune system, leading to full-blown AIDS, a deadly condition.

China has 560,000 to 920,000 people infected with the HIV virus and 97,000 to 112,000 AIDS patients, according to 2009 Ministry of Health and United Nations estimates.

SOURCE: Reuters

.

Matokeo ya utafiti uliofanywa na Mradi wa Utafiti na Elimu na Demokrasia Tanzania (REDET) yanaonyesha kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni mchapakazi zaidi ya 'bosi' zake,Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Ali Mohammed Shein. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa katika gazeti la Mwananchi,asilimia 61.2 ya wananchi waliohojiwa wameonyesha kuridhishwa na utendaji wa Pinda huku Kikwete akipata asilimia 58.8 na Dkt Shein akiwa na asilimia 46.8Kwa habari kamili soma HAPA.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.