5 Sept 2010

By Guy Adams

She tells lies. She's a lousy tipper. She billed the Republican Party more than $3,000 for the underwear she bought during the last Presidential election, including dozens of Spanx girdles. Oh, and for all the cutesy charm that Sarah Palin projects in public, she's got a nasty habit of bullying staff, losing her temper with friends and family, and, when particularly upset, throwing tin cans at her husband, Todd.

Fresh from a week that seemed to cement her status as the most valuable brand in American conservatism, and saw her both receive top billing at a vast "tea party" rally in Washington, and almost single-handedly alter the direction of a Senate race in her native Alaska, Palin is on the receiving end of a brace of vintage journalistic hatchet jobs from the left and right sides of the political spectrum.

The first, a vast profile of the self-proclaimed "Mamma Grizzly," which covers 18 pages of next month's Vanity Fair, devotes more than 10,000 words to a mixture of revelation, allegation and innuendo regarding both her public and private persona, detailing what it calls her "erratic behaviour," her "pattern of lying," and what the magazine's reporter Michael Gross describes as the "sad, mouldering strangeness" of her everyday existence.

The second comes courtesy of Meghan McCain, the daughter of Palin's former running mate John, whose new book Dirty, Sexy Politics, describes the former Governor of Alaska as a "a time bomb" who is addicted to attention and whose eccentric behaviour brought "drama, stress, complications, panic, and loads of uncertainty," to the 2008 campaign trail.

Like almost everything else that involves Palin – who, despite her habit of avoiding interviews in what she calls the "lamestream media," has still not ruled out a run for the 2012 Presidency – the broadsides are receiving endless attention. As befits an increasingly polarised nation, they are sparking outrage in conservative circles and a mixture of mirth and disbelief in liberal ones. Palin takes issue with the allegation and has responded with an attack on Vanity Fair, calling into question its facts and reporting standards.

In truth, Vanity Fair's article is a curious mixture of un-sourced innuendo and minor revelation which was mostly staggering for its sheer scale. The magazine spent four months trailing the former Alaska governor on the various speaking engagements that have helped her earn $13m since quitting last year.

It alleges she is "warm and effusive in public, and angry in private," that she is paranoid and vindictive towards former friends, and it revels the details of the occasional sense-of-humour failures which inspired the headline: "The Sound and the Fury."

The piece quotes a "friend" of Palin and her husband Todd, who once witnessed a domestic dispute. "They took all the canned goods out of the pantry, then proceeded to throw them at each other," recalls the friend. "As soon as she enters her property and the door closes, even the insects in that house cringe. She has a horrible temper, but she has gotten away with it because she is a pretty woman."

During the campaign, an un-named "aide" is quoted as claiming that Palin "lashed out" at the slightest provocation, sometimes screaming at staff and throwing objects. Asked about her temper, Todd told a staffer: "You just got to let her go through it... Half the stuff that comes out of her mouth she doesn't even mean."

Vanity Fair also claims that Palin signs the autographs in her books with an autopen, requires three hairstylists and make-up artists before public appearances, and despite her principled opposition to immigration, employs an Hispanic housekeeper.

She is also a bad tipper, the article claims. During a recent stay at the Hyatt in Wichita, she gave the bellboy just $5 for seven bags, making her the "all time worst tipper" of the famous people who have stayed there. She also failed to leave money for the maids who cleaned her room.

As suggested by Levi Johnston, the estranged father of her teenage daughter Bristol's child, the magazine also claims that Palin is a lousy and only occasional angler, who exaggerates her interest in fieldsports to win support in conservative circles.

"This whole hunter thing, for Sarah? That is the biggest fallacy," a friend of the family was quoted as saying. "That woman has never hunted. She never helps with the fishing either. It's all a joke." Bristol, by the by, has made several hundred thousand dollars from media appearances, and was this week unveiled as a contestant on the popular US television programme Dancing With the Stars.

The Vanity Fair article wasn't all tittle tattle. It also explored Palin's links to extremist Christians – the "prayer warriors" she often cites in speeches – and explored her somewhat opaque finances. It revealed that Timothy Crawford, treasurer of Sarah-PAC, her political action committee, is being investigated in Ohio for alleged campaign finance misdemeanours, and has refused to respond to a subpoena issued by the state's investigators.

Meanwhile, Palin's famously scant general knowledge may be even more flaky than originally thought. When McCain aides prepared her for television interviews in 2008, they allegedly found that – besides thinking Africa was a country rather than a continent – she had never heard of Margaret Thatcher. Palin now cites Thatcher as one of her all-time heroines.

Responding yesterday, Douglas McMarlin, a spokesman for Sarah-PAC, said: "The article is a collection of lies cobbled together by an outlet without standards. As the message continues to succeed, the messenger will continue to be attacked by yellow journalists seeking to increase sales."

Miss McCain, for her part, has attempted to put a marginally more sympathetic gloss on things. Her book reveals that the Republican inner circle was "waiting for her [Palin] to explode" during the 2008 campaign. She adds: "There was a fine line between genius and insanity, they say, and choosing her as the running mate was starting to seem like a definition of that line."


The policeman who found the body of MI6 codebreaker Gareth Williams said it was submerged in ‘fluid’, The Mail on Sunday has learned.An inquest heard last week that the 31-year-old spy was padlocked in a sports hold-all and left in the bath of his two-bedroom flat in Pimlico, Central London.But the disclosure that he was also covered by liquid – not thought to be blood or water – has raised fears that a substance was used to accelerate decay and complicate toxicology tests.

The revelation came as new details emerged of the highly sensitive nature of Mr Williams’s work.A source said he had the highest security clearance available to an intelligence officer and was part of a secretive ‘cell’ that created devices that can steal data from mobiles and laptops.

Now, nearly two weeks after cycling enthusiast Mr Williams was found in his flat, police are apparently no nearer to learning how or when he died.This is despite a post-mortem, a second examination and toxicology tests, the results of which might not be available for weeks.

Sources close to the inquiry say the PC who found the body described it as being in ‘fluid’ when he radioed for assistance. Detectives at the scene are understood to have used the same word in their reports.Immediately after making the discovery at the flat, the PC said: ‘This is a murder scene.’

Mr Williams, from Anglesey, North Wales, worked as a cipher and codes expert for the Government’s eavesdropping centre GCHQ in Cheltenham.He was on a year-long secondment to MI6 which was due to end days after he was found dead.Police and security sources have indicated that the explanation for his death is more likely to be found in his personal life rather than his work.

But speculation that he was the victim of a professional ‘hit’ was given credence last night after further details of his work were disclosed.‘He was involved in some very sensitive projects, known as codeword protected,’ said a security expert.‘This meant that only the people in his cell would know what he was working on, and nobody else in his organisation.

‘You are signed in to these projects and once you finish one you are signed out and you no longer have access to any data or news about what is happening in the project.’Mr Williams – a child prodigy who had a degree in maths at 17 and then a PhD in the subject – was part of a team that created devices which ‘hook’ on to mobiles and laptops. ‘It is an aggressive form of Bluetooth or similar wireless technology,’ said the security expert.

He said such devices would be used by spies on the ground to steal data from the handsets of unsuspecting terrorists, organised criminals or officers from rival intelligence agencies.‘Traditionally, there has been a separation of MI6 and GCHQ,’ said the expert. ‘MI6 has been full of the James Bond types working on the ground and GCHQ is filled with boffins with beards who are doing their scientific stuff. ‘But recently there has been a merger of these agencies’ work and Williams was at the forefront of that. This was why he was on secondment to MI6.’

He added that Mr Williams did similar work when he had stints at the National Security Agency in America.The NSA is the equivalent of GCHQ and has been leading the West’s attempts to intercept communication between Al Qaeda cells. Mr Williams worked for the Special Delivery Team, a unit set up in the NSA to create advanced bugging and intercepting devices.

‘If you just look at Williams’s CV, you know he has worked in some of the most important data-mining centres in the UK and US. His salary is no indication of his rank,’ said the expert.

It has also emerged that before his secondment to MI6, Mr Williams worked briefly for MI5, the domestic security agency. As part of that work, he was sent to Bulgaria on a secret mission.A source close to the investigation said that on August 23 police were asked to check on Mr Williams’s flat as he had not shown up for work. Just before 6pm, a PC went to the Georgian townhouse in Alderney Street, which has been converted into four flats on four floors. Mr Williams had the top one.

The PC could not get into the house so the letting agent, W.  A. Ellis, was called and a woman employee arrived with keys.She hovered at Mr Williams’s door as the PC went inside. Within minutes he emerged quickly from the en suite bathroom and escorted the woman back downstairs. He then told her: ‘You stay here. This is now a murder scene.’

This weekend, staff at W. A. Ellis, of Knightsbridge, refused to confirm details.A spokeswoman said: ‘36 Alderney Street is owned by a private company, New Rodina.‘There has been speculation that it is linked to MI6 or that it is a front for MI6. Our clients do not have any links to MI6 whatsoever and are distressed by the death of Mr Williams.’

SOURCE: Daily Mail


Inaudhi na kukasirisha kuona gazeti la serikali,Habari Leo,likijipachika jukumu la kumuua kisiasa mgombea wa Chadema Dokta Wilbroad Slaa kama ambavyo imekuwa ikifanywa na magazeti ya Habari Corporation na Changamoto,na mengineyo yanayofadhiliwa na mafisadi.

Gazeti hilo limeandika kwa kirefu kuhusu anayedaiwa kuwa mume wa mwenza wa sasa wa Dkt Slaa,Josephine Mushumbusi.Ungetegemea gazeti hilo linaloendeshwa kwa fedha za walipa kodi wa Kitanzania pasipo kujali itikadi zao za kisiasa,lingetafakari kwa makini madhara ya habari hiyo.Wanajua sana wanachofanya,na yayumkinika kuamini kuwa serikali inayoongozwa na mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,imeridhia uchapishaji wa habari za aina hiyo.

Kuna msemo wa busara unaoasa "WANAOISHI KWENYE NYUMBA ZA VIOO WASIRUSHE MAWE".Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una wasifu wenye mawaa ya aina moja au nyingine then si wazo jema kuwachafua watu wengine.Wengi wetu tunafahamu "ishu binafsi" za viongozi wa CCM ikiwa ni pamoja na Kikwete mwenyewe.Hazizungumzwi hadharani kwa kuwatunzia heshima viongozi hao lakini inaelekea katika kutapatapa kwao baada ya kugundua hawamwezi Dokta Slaa kwa hoja,wameamua kuhamia kwenye character assassination.

Majukwaani,Kikwete na CCM yake wanajifanya kuhubiri umuhimu wa kampeni za kistaarabu lakini pembeni wanaruhusu raslimali za umma zitumike kumchafua Dokta Slaa.Kikwete alichukua hatua za haraka pale mtandao maarufu wa Ze Utamu ulipochapisha picha zinazomhusu lakini anaruhusu gazeti la serikali litumike kumwandama Dkt Slaa.

Na kwa kuonyesha unazi,kuna mahala katika habari hiyo ambapo pasi aibu wameandika (nanukuu) "Na wakati Mahimbo akiwa njia panda akishindwa kujua hatima ya ndoa yake, Dk. Slaa, Padri msomi `amelitangazia’ taifa mbele ya mikutano ya kampeni ya chama chake cha Chadema kuwa Josephine ndiye mke wake mtarajiwa..." 

Hivi Mhariri wa Habari Leo hafahamu kuwa Dkt Slaa sio Padri bali aliwahi kushika nafasi hiyo na kuiacha?

Blogu hii inamshauri Kikwete akemee mkakati huu mufilisi wa character assassination.Wengi wanafahamu kwa undani maisha ya Kikwete tangu akiwa Waziri,na wanajua vema maisha yake binafsi ndani na nje ya nchi.Asijivunie vyombo vya dola kumlinda pindi kibao kitapogeuzwa upande wake.Ni bora Dokta Slaa anayetangaza hadharani kuhusu uhusiano wake na Josephine kuliko kashfa lukuki zinazohifadhiwa kuhusu viongozi wa CCM kwa vile tu tunawaheshimu na tuna mambo muhimu zaidi ya kuzungumzia kuliko maisha binafsi ya viongozi wetu.

I repeat: Those who live in glass houses shouldn't throw stones!!!





Those who live in glass houses shouldn't throw stones.

4 Sept 2010

Dr_Slaa

TAFADHALI UKISHASOMA SAMBAZA KWA MWENZIO.BONYEZA HAPO JUU KULIA PALIPOANDIKWA "<>SHARE" KISHA CHAGUA NJIA YA KUSAMBAZA.

Kibonzo kwa hisani ya FEDE

Tunafahamu kuwa mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,ni mahiri sana katika kutoa ahadi.Wakati wa kampeni zake za kuwania urais kwa mara ya kwanza mwaka 2005 alitoa rundo la ahadi ambazo hata angekuwa na uwezo wa kutekeleza basi ingebidi awe rais wa milele.Kwa makusudi,badala ya kufanya marejeo ya ahadi zake lukuki za 2005,Kikwete ameendelea kutoa ahadi zaidi akijaribu kuwaghilibu Watanzania kuwa safari hii akipewa madaraka atazitekeleza.Swali la msingi ni kipi kilichomzuia kuzitekeleza katika kipindi hiki (2005-2010) na kipi kitamwezesha kutekeleza ahadi hizo katika awamu ijayo (2010-2015).

Alipokuwa kwenye kampeni zake huko mikoani aliahidi (bila aibu) kuwa tatizo la umeme sasa litakuwa historia.Last time aliposema hayo,walikuja matapeli wa Richmond.Sijui safari hii watakuja wasanii gani "kuvuna wasichopanda".Angekuwa na busara,angewaeleza Watanzania kwanini umeme umeendelea kuwa tatizo sugu nchini.Ufumbuzi wa tatizo hilo hauwezi kupatikana kwa ahadi zaidi ya zilizokwishatolewa.Kikwazo kikubwa katika upatikanaji wa ufumbuzi wa tatizo la umeme ni maslahi binafsi na ufisadi.Kuna watu wanaoombea Tanzania iwe kizani kila siku ili wauze jenereta zao.Kuna wengine wanaotaka umeme uendelee kuwa tatizo ili wapate fursa ya kutengeneza dili za kifisadi kama za IPTL,Richmond na Dowans.Na Kikwete anawajua sana watu hao lakini hana nia wa kuwachukulia hatua.Ikumbukwe kabla ya kuukwaa urais,Kikwete alishawahi kuwa Waziri wa Nishati!!!

Kadhalika,katika mwendelezo wa ahadi,Kikwete ameahidi kuleta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la maji jijini Dar es Salaam.Utadhani kwamba tatizo hilo halikuwepo wakati wa utawala wake,au limeanza majuzi.Na kama hiyo haijatosha,akaahidi tena kuwa daraja la Kigamboni litajengwa kwa vile zabuni ya kumpata mkandarasi imeshakamilika.Kwanini iwe baada ya kumchangua tena na sio alipochaguliwa 2005?Haihitaji hata elimu ya chekechea kutambua kuwa ahadi hizi ni hewa.ZITAENDELEA KUWA AHADI TU.

Ukimsikiliza kwa makini utagundua kuwa Kikwete hayuko serious na anachoongea.Pengine ni kwa vile anafahamu kuwa hahitaji kuwa serious kupata tena nafasi ya urais.Pengine ni tatixo la upeo tu.Hata hivyo,kumlaumu JK ni kumwonea kwa vile kama ilivyokuwa Desemba 2005,come Oktoba this year HATAJICHAGUA MWENYEWE KUWA RAIS BALI ATATEGEMEA KURA ZA WATANZANIA.Mwaka 2005 waliompigia kura na kumpa ushindi wa kishindo wanaweza kuwa na excuse kwa kudai walikuwa HAWAMJUI VEMA.Five years later,naamini kila Mtanzania anafahamu udhaifu wa kiongozi huyu.Kumrejesha tena Ikulu kwa miaka mingine mitano ni kosa ambalo litawagharimu sana Watanzania.

Ikumbukwe kuwa kama atarejea tena madarakani,kuna uwezekano mkubwa wa kuendesha nchi kwa mtindo wa BORA LIENDE kwa vile hiyo itakuwa awamu yake ya mwisho kwa mujibu wa Katiba.Kama ameweza kuwapuuza Watanzania katika kipindi hiki cha miaka mitano inayoisha huku akielewa fika kuwa itambidi awabembeleze tena wampigie kura mwaka huu,kwanini basi asiwapuuze zaidi kwa vile hatagombea tena urais hapo 2015?

Ni muhimu kwa Watanzania kutambua kuwa tusipoziba ufa tutajenga ukuta.Ufa wetu kwa sasa ni Kikwete na CCM yake.Tukiwarejesha tena madarakani hapo Oktoba tutakuwa tumejichimbia kaburi refu.Tuweke kando ushabiki wa vyama vya siasa na tuangalie maisha yetu na hatma ya taifa letu.Tusifanye mzaha kwa kuendekeza kauli "JINI LIKUJUALO HALIKULI LIKAKWISHA" (i.e. Bora Kikwete na CCM kwa vile tunawajua kuliko hao akina Dkt Slaa na Chadema tusiowajua).Problem is,jini hili safari hii litatumaliza na kutukomba kila kitu.Wameiba mabilioni ya EPA,wametutapeli na Richmond,Dowans,IPTL,Kiwira,Meremeta,Tangold,nk na hawajatosheka.Tukiwarejesha tena madarakani watatukomba kila kitu.

Bahati nzuri Mungu si Athumani.Ametuonea huruma na kumwibua mkombozi Dokta Wilbroad Slaa.Hii ni nafasi adimu,na ndio maana nguvu za giza zimekuwa zikimwandama.CCM wanajua bayana kuwa Dkt Slaa ana dhamira ya dhati kuwatumikia Watanzania.Hawampingi kwa vile ni mwanasiasa wa upinzani bali wanahofia atawafungua macho waliolala,na pia atawapora mtaji wao- yaani masikini wanaonunuliwa kwa pishi za mchele na sukari huku wakiahidi maisha bora "hewa".

Kama wewe si fisadi basi unapaswa kuwa na NIA,SABABU na UWEZO wa kumtosa JK na CCM yake hapo Oktoba.Maisha Bora ya Kweli (na sio ya kuzugana) Yanawezeka,Ila tu sio kwa wazushi hawa waliopo madarakani bali kupitia kwa Dokta Slaa na CHADEMA.

Kwa mujibu wa blogu ya Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua (mwanahabari mahiri Ansbert Ngurumo),Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa alionekana Ikulu siku ya Alhamisi majira ya saa 9 alasiri ambapo inaelezwa alikutana na Rais Jakaya Kikwete,mgombea wa CCM ambaye amelalamikiwa na Chadema kwa kukiuka Sheria y Gharama za Uchaguzi.Awali,Tendwa alisema kuwa angetoa "hukumu" keshokutwa (Jumatatu).

Kwa hakika,haihitaji utaalam wowote kuhusisha tukio hilo (la Tendwa kukutana na Kikwete) na pingamiz la Chadema.Na haihitaji ujuzi wa sheria kubashiri matokeo ya "hakimu kukutana faragha na mshtakiwa" siku chache kabla ya hukumu.

Wengi wetu tunafahamu Tendwa atasema nini hiyo Jumatatu.Most likely,ameshafanya maamuzi ila kinachoshughulikiwa sasa ni usanii wa lugha ya utoaji wa maamuzi hayo.Na ni katika hilo ndio maana inamlazimu awasiliane na JK ili "ajenge mazingira ya hukumu ya haki".Katika mazingira tuliyonayo ambapo Msajili wa vyama vya siasa ni kama kibaraka wa CCM,haiwezekani kabisa kiongozi huyo kutoa maamuzi ya haki yatakayokiathiri chama hicho.

Na dalili za "usanii" zimeonekana tangu Chadema wawasilishe malalamiko yao.Hivi Tendwa anaweza kuwaambia Watanzania kwanini imchukue takriban wiki nzima kutoa maamuzi kuhusu malalamiko ya Chadema?Je hiyo pekee sio dalili ya uzembe na kutowajibika ipasavyo?Awali aliwaeleza waandishi wa habari kuwa angetoa maamuzi Jumatatu lakini hakueleza kwanini itachukua muda wote huo kutoa maamuzi hayo muhimu kwa mustakabali wa demokrasia nchini mwetu.Jibu jepesi ni kwamba hana ubavu wa kutoa maamuzi kabla ya kupata ridhaa ya CCM.Na kwa vile CCM ndio watuhumiwa,ni dhahiri maamuzi ya Tendwa yataelemea kuipendelea CCM.

Nafahamu kuna wataosema "aah,sasa kelele za nini wakati maamuzi hayajatolewa?" Wana haki ya kusema hivyo lakini wanapaswa pia kutambua vema mapungufu ya Katiba yetu yanayomfanya mgombea wa chama tawala kuwa na advantage kubwa dhidi ya wagombea wengine kutokana na ukweli kwamba Katiba inampa rais nguvu kubwa mno.

Kikwete ameendelea kupuuza malalamiko ya Chadema kwa kuzidi kutoa rushwa ya ahadi katika mikutano yake ya kampeni.Sote tumemsikia akiwazuga wapigakura huko Mbagala kuhusu daraja la Kigamboni na ahadi nyingine hewa ya huduma ya uhakika kwa maji jijini Dar es Salaam.Huyu mtu hana aibu kwa sababu ahadi anazotoa sasa zinatoa picha ya mgombea anayeomba idhini ya kuingia madarakani kwa mara ya kwanza na sio aliyekuwa rais wetu kwa miaka mitano iliyopita.Kama tangu 2005 hadi leo ameshindwa kuwezesha ujenzi wa daraja hilo la Kigamboni,kwanini tumwamini kuwa ataweza katika mhula wake wa mwisho (2010-2015) hasa ikizingatiwa kuwa kipindi hicho cha pili kitatumika zaidi kwa yeye kujitengenezea mazingira ya "kustaafu kwa amani"?

Jeuri ya Kikwete inasababishwa na ufahamu kuwa Chadema,na vyama vingine vya upinzani,havina mahala pa kukimbilia pindi wasiporidhishwa na mwenendo wa kampeni za Kikwete na CCM kwa ujumla.Anafahamu kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Mahakama na taasisi nyingine za kusimamia uchaguzi na sheria nza nchi kwa ujumla,ziko mikononi mwa CCM.Hata hivyo,wapinzani hawapaswi kukata tamaa kwa vile nchi yetu kama masikini wa kutupwa inategemea sana misaada ya wafadhili.Japo kuwapigia magoti wafadhili kunaweza kutafsiriwa kama "kuegemea kwenye ukoloni" lakini tufanyeje kama nchi yetu inaendeshwa kiholela.Binafsi,nina matumaini makubwa kuwa nchi wafadhili zinafuatilia kwa karibu mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa nchini na hazitasita kuchukua hatua mwafaka pale CCM itakapotumia ubabe wake kulazimisha ushindi.

Hata hivyo,wakati we keep on hoping for the best and expecting the worst,Tendwa afahamu kuwa he wont get away with this issue as easily as he might think.Blogu hii inaamini kuwa Chadema ni chama makini na chenye rekodi nzuri ya ufuatiliaji mambo.Ni katika mantiki hiyo basi blogu hii inatarajia kuwa Chadema hawatamruhusu Tendwa kufanya uhuni wa aina yoyote ile katika maamuzi yake.Ni heri uchaguzi uvurugike lakini haki ipatikane.Kutoa fursa ya sheria za nchi kupindishwa kwa namna watawala wanavyotaka ni hatari sana hasa tukizingatia ulevi wa madaraka unaowakabili viongozi wengi wa "dunia ya tatu".

Kama alivyoandika Ngurumo katika blogu yake,nami narejea kumkumbusha Tendwa kuwa HATUDANGANYIKI!




Brought to you by Urban Pulse Creative

3 Sept 2010


CHANZO: Jamii Forums

Wenye busara zao wanatuusia kuwa pindi ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo then sio wazo jema ku-entertain kurusha mawe.Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una ishu zenye utata katika maisha yako then sio wazo jema kuanza kushupalia ishu za watu wengi lest flani akakugeuzia kibao.

Lakini usemi huo umeonekana hauna maana kwa Katibu Mkuu wa CCM,Yusuph Makamba,ambaye kwa siku kadhaa sasa ameamua "kuvalia njuga maisha binafsi ya Dokta Wilbroad Slaa" na kuligeuza suala la ndoa ya mgombea huyo wa Chadema kuwa ajenda ya uchaguzi.

Pengine ni dharau au ujinga,Makamba alijisahau kuwa wakati anamnyooshea kidole Dkt Slaa,yeye mwenyewe (Makamba) alikuwa na doa linaloweza kabisa kumpeleka jela.Kwa mujibu wa taarifa zilizozagaa mtandaoni,Makamba anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi wakati akiwa mwalimu mkuu wa shule moja na hatimaye kufukuzwa ualimu.

Hizi ni tuhuma nzito sana kwani licha ya kumtia doa Makamba kama mwanasiasa,ni suala linaloweza kumpeleka jela endapo victim wake atajitokeza hadharani,na kupatiwa msaada wa kisheria.Lakini tukiweka ishu za kisiasa kando,hapa kuna suala la binti asiye na hatia ambaye inadaiwa alibakwa na mtu aliyekabidhiwa dhamana ya kumpatia elimu na mwongozo katika maisha yake,mwalimu wake,lakini akaishi kubakwa.

Blogu hii inatoa ombi maalum kwa yeyote yule anayeweza kuipatia taarifa za uhakika kuhusu binti huyo anayedaiwa kubakwa na Makamba.Lengo si kumkomoa mtuhumiwa bali kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake as well as kutoa reminder kwa watu wengine wanaotumia vibaya dhamana walizokabidhiwa,iwe mashuleni,makazini au hata katika ngazi ya familia.

Je unamfahamu binti anayedaiwa kubakwa na Makamba?Kama jibu ni ndiyo basi tafadhali sana tuwasiliane kwa barua pepe kwa anuani hii [email protected].

1 Sept 2010

Kama waliweza kuchakachua kadi zao wenyewe kwenye kura za maoni watashindwaje kufoji za Chadema?Na wameshamgeuza sehemu ya kufanyia mazoezi kuzuga kama anavyotabasamu hapo chini kwa kupewa "two hundred thousand USD za $300,000/="!!!!


31 Aug 2010





Mwezi Juni mwaka huu tuzo maarufu ya kimataifa iitwayo Ashden Awards iilitolewa kwa wahusika kadhaa duniani zikiwepo nchi za Afrika Mashariki. Tuzo hiyo hutolewa na shirika maalum lililoundwa na duka maarufu la matajiri wa Uingereza yaani Sainsbury Kutoka katika Ashden Trust Charity ambapo mlezi wake akiwa ni Prince Charles. Lengo lake ni kusaidia kurekebisha na kuboresha mazingira duniani . Tuzo ya mwaka huu ilitolewa kwa watafiti na wabunifu waliotengeneza zana za kutengeneza umeme kutokana na nguvu asilia za jua yaaani Solar Energy.
Ingawa wabunifu walitoka mataifa mbalimbali ya Marekani, Asia na Afrika washindi pia walihusisha Kenya, Uganda na Tanzania.
Umeme Jua, Bio gas( Gas Itokayo kwenye kinyesi cha ng'ombe) ni zana ambayo itawasaidia watu maskini hasa wanaotoka nchi kama yetu Bongo vijijini.
Baada Ya Mafanikio makubwa la movie ya £ovely Gamble Urban Pulse wakishirikiana na Msanii/ Mhariri Freddy Macha Wamepewa mzigo mwingine wa kutengeneza documentary ambayo itakuwa hewani tarehe 2 sept 2010 na kurushwa katika tv za hapa ukerewe na mabara mengine ya ulaya.
Hivyo basi utawala wa Urban Pulse Unawaletea trailer ya documentary hiyo hapo juu.

Baada ya uzinduzi tutawapatia kipindi chote
Asanteni sana
Urban Pulse Creative

30 Aug 2010

Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimewasilisha rasmi pingamizi dhidi ya mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Jakaya Kikwete kwa madai ya kukiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi (iliyosainiwa na Kikwete kama Rais).Imedaiwa kuwa Kikwete amenongeza mishahara ya watumishi wa umma kinyume cha taratibu,na inatafsiriwa kuwa ni rushwa.

Stay tuned!

Kwa mujibu wa mwana-Jamii Forums

Nimekutana na habari hii huko Jamii Forums,nami naiwasilisha kama ilivyo:

Dola kuishughulikia CHADEMA
DAWATI LA HATUDANGANYIKI limepokea taarifa za kuaminika kutoka vyanzo vyake kuwa kuwa mara tu baada ya mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi tarehe 28 Agosti 2010 wakuu wa Idara ya intelejensia walikutana na timu ya Kampeni ya CCM kwa ajili ya kutoa mlisho nyuma, na kupanga mikakati ya kuikabili CHADEMA, na yafuatayo yalijiri:-
a)Idara ililazimika kutolea ufafanuzi sababu zilizopelekea shauri wake wa kutaka matangazo ya TBC ya mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CHADEMA kurejeshwa mara moja baada ya kukatizwa. Walieleza kuwa ilitokana na maelfu ya wananchi waliohudhuruia mkutano huo kuwa wa kwanza kugundua kukatishwa kwa matangazo hayo na kuamua wenyewe, bila ya kushawishiwa na kiongozi yeyote kuchukua hatua kali sana dhidi ya TBC. Viongozi wa CHADEMA walistukia tuu mkutano ukitaka kuvurugika kwa wananchi kudai vikali kurejeshwa kwa matangazo hayo. Ilielezwa kuwa kuvurugika kwa mkutano ikwa sababu ya kukatishwa kwa matangazo ya chombo cha umaa kama TBC iimeelezwa kuwa ingekuwa ni aibu kubwa kwa Serikali na TBC.
b)Idara ilitoa taarifa kuwa licha ya umati wa watu waliohudhuria kutofikia ule wa mkutano wa uzinduzi wa CCM, lakini kwa kuwa umati huo kila mtu alijinyanyua kutoka atokako na kuja Jangwani kwa ajili ya CHADEMA tofauti na maandalizi makubwa ya usafiri, fedha, burudani za kila aina, viburudisho n.k yaliyofanywa na CCM kuwafikisha watu kwa maelfu Jangwani. Hizo ni dalili mabaya na ni tishio kubwa kwa CCM. Na ikaamuliwa kuwa iandaliwe mikakati ya kuwakatisha tamma wananchi wenye mapenzi na CHADEMA.
Mkakati :- Ilamuliwa kuwa upandikizwe mgogoro baina ya viongozi wa CHADEMA na mgombea wake Dr W. Slaa; na kuwachonganisha na wapiga debe wao akina Marando, Shibuda, Mpendazoe n.k kwa nia ya kuwakatisha tamaa wenye mapenzi na CHADEMA na wote wanaotarajia kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA.
Iliamualiwa kwa kuwa wananchi wanampenda sana Dr W Slaa, zisambazwe habari kuwa aelewani na Mwenyekiti wake Ndg Freeman Mbowe kwa sababu Dr Slaa sio kutoka kabila la wachagga. Ilikubaliwa kuwa taarifa hizo zianze kusambazwa wiki inayoanzia Jumatatu ya tarehe 30 Agosti 2010. Na tathmini ifanyike kujua mafanikio yake wakati zinatungwa mbinu mpya.
Iliamuliwa kuwa magazeti ya New Habari Corporation ikiwemo Mtanzania, Rai n.k yaanze kutumika kwa kazi hiyo wakati waandishi zaidi wa kufanya kzai hiyo wakitafutwa.
Ili wananchi wenye mapenzi mema na CHADEMA waweze kusadiki taarifa zitakazosambazwa ilikubaliwa kuwa magazeti yatakayotumika yaanze kwanza kwa kipindi kifupi kuandika habari njema kuhusu CHADEMA na wagombea wake; na baada ya mashabiki wake kuyaamini magazeti na vyombo hivyo vya habari ndipo kazi ya kuisamabaratisha CHADEMA ianze rasmi.
Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.
Vyombo vya habari vya Serikali ya ikiwemo magazeti ya Daily News na Habari Leo na TBC na redio za TBC vilielekezwa kuanza mara moja kazi ya kuipamba CHADEMA kama chama na watu wa fujo mbele ya jamii makakati amabo unadaiwa kufanikiwa sana kuisambaratisha CUF mwaka 2005, wakati Mkuu wa chombo kimoja cha dola alipodai siku moja kabla ya upigaji kura wamekamata shehena ya majambia yenye rangi za bendera za CUF
c)Pingamzi la CHADEMA dhidi ya Jakaya Kikwete mkutano ulikubaliana kuwa kuaniza sasa idara ihakikishe kuwa inamgeuzia kibao Dr Slaa na kusambaza habari kwa wafanyakazi na umma kuwa DR Slaa anapinga wafanyakazi kuongezwa mishahara ndio maana CHADEMA inamuwekea pingamizi mgombe wa CCM Jakaya Kikwete kwa kitendo cha kuwaongezea mishahara watumishi wa umma katika kipindi hiki cha kampeni.
Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!

If it's true,hivi hii sio local version yetu ya Watergate?

From Lt. Gen. Peter Olu
From:

NATIONAL SECURITY ADVISER 
Add to Contacts
OFFICE OF THE NATIONAL SECURITY ADVISER
TO THE PRESIDENT FEDERAL REPUBLIC OF NIGERIA
GET BACK TO ME AT YOUR EARLIEST CONVENIENCE

Dear Sir/Madam,

I am Lt. Gen. Peter Olu, National Security Adviser to the New President Dr Goodluck Jonathan Federal Republic of Nigeria. I decided to contact you because of the prevailing security report reaching my office and the intense nature of policy in Nigeria. This is to inform you about our plan to send your fund to you via cash delivery. This system will be easier for you and for us. We are going to send your contract part payment of US4.1 Million to you via diplomatic courier service.

Note: The money is coming on two security proof boxes. The boxes are sealed with synthetic nylon seal and padded with machine. This fund was brought to us from America; it was meant for our Local AFEM market. But since the money was not used, I will use my position as the National Security Adviser to the President to send this fund to you.

The boxes are coming with a Diplomatic agent who will accompany the boxes to your house address. All you need to do now is to send to me

Your full name
Your house address
Your age
Your marital statue
Your identity such as, international passport or driver license
Your contact phone and fax numbers,

The Diplomatic attached will travel with it. He will call you immediately he arrives your airport. I hope you understand me.

I will let you know by the special grace of God when the boxes are airlifted.

Note: The diplomatic does not know the original contents of the boxes. What l declared to them as the contents is Sensitive Photographic Film Material. I did not declare money to them please. If they call you and ask you the contents please tell them the same thing OK, I will let you know how far I have gone with the arrangement. I will secure the Diplomatic immunity clearance certificate that will be tagged on the boxes to make it stand as a diplomatic consignment.

This clearance will make it pass every custom checkpoint all over the world without hitch. Confirm the receipt of this message and send the requirements to me immediately you receive this message. If you need more information about this, I will give you the details how to contact the diplomat for more information on how to carry out the plan.

I need you response because the boxes are schedule to leave as soon as we hear from you. Reply me immediately you receive this message via Email ([email protected]) Call me on my direct phone: (+234-8063619571) or Fax: (234-8029402741)

Best Regards,
Lt. Gen. Peter Olu

28 Aug 2010

Bonyeza HAPA kupata up-to-the-minute updates za uzinduzi wa kampeni za Chadema katika viwanja vya Jangwani.

CAUTION:Some videos contains swearing











27 Aug 2010

Rais wa Rwanda Paul Kagame amechaguliwa tena kuongoza nchi hiyo baada ya kushinda kwa asilimia 93 katika uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni,lakini kulikuwa na taarifa zilizosambaa kuwa waandishi wa habari na wanasiasa wa vyama vya upinzani wameuawa au kuwekwa jela.Sasa,ripoti iliyovuja (leaked) ya Umoja wa Mataifa inaashiria kuwa jeshi la Rwanda linaweza kuwa limetenda uhalifu wa kivita na kuua makumi ya maelfu ya watu mwishoni mwa miaka ya 90 (late 1990s).

Kagame anaheshimika sana kwa kuleta maendeleo na amani kwa nchi hiyo iliyotiwa kovu na mauaji ya kimbari mwaka 1994 ambapo Wahutu (kabila kubwa nchini humo) waliwaua Watutsi (kabila dogo nchini humo)-na Wahutu wenye msimamo wa wastani- takriban milioni moja.Chini ya Kagame,ambaye ni Mtutsi na kamanda wa zamani wa jeshi,Rwanda sasa ni salama,huku ikitajwa kuwa miongoni mwa zenye rushwakidogo zaidi barani Afrika.Matokeo yake,nchi hiyo imekuwa ikipokea mamilioni ya dola katika misaada ya kimataifa na inaendelea kujijenga.

Lakini,kwa mujibu wa gazeti la New York Times,mmoja wa wapinzani wa Kagame alikutwa amekufa kabla ya uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 mwezi huu,huku kichwa chake kikikaribia kutenganishwa na kiwiliwili.Na wapinzani wengine "maarufu ambao waliongea hadharani kumpinga Kagame na pengine kuuweka majaribuni umaarufu wa Rais huyo walizuiliwa kushiriki katika uchaguzi",kwa sababu za kiufundi.Kagame amehalalisha hatua kali alizowahi kuchukua huko nyuma,kwa mujibu wa gazeti hilo,akidai kuwa Rwanda bado haijatulia vya kutosha.

Kwa jinsi gani hali nchi humo haijatulia inabainishwa na katika ripoti ya kamishna wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia haki za binadamu,iliyopatikana na gazeti la Le Monde la Ufaransa kabla haijachapishwa.Ripoti hiyo inabainisha,kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Uingereza,mwaka 1996 wakati vikosi vya Watutsi vikiwakimbiza Wahutu kuelekea Jamhuri ya Kimekrasia ya Kongo (wakati huo Zaire),na mwaka 1998 katika uvamizi wa kudhibiti waasi wa Kihutu,jeshi la Rwanda na washirika wake liliwazingira mamia ya wanaume,wanawake na watoto na kuwachinja kwa kutumia majembe na mashoka.Nyakati nyingine,"wakimbizi wa Kihutu walichinjwa kwa kutumia sime za bunduki,kuchomwa moto au kupigwa nyundo".Matukio hayo,inaeleza ripoti hiyo,ni sawa na mauami ya kimbari.

Serikali ya Rwanda amepinga madai ya ripoti hiyo,na inadaiwa imetishia kuondoa askari wake katika jeshi la kulinda amani huko Darfur na kwingineko,iwapo ripoti hiyo itawekwa hadharani rasmi.Umoja wa Mataifa unaeleza kuwa ripoti ililyovuja ni rasimu (draft) tu.Inasubiriwa kuonwa kama jumuiya ya kimataifa itasalimu amri kwa shinikizo kutoka serikali ya Kagame kuondoa mpambano na kupunguza makali ya lugha katika chapisho timilifu (final version).

Imetafsiriwa kutoka Jarida la Newsweek



Ilani ya Uchaguzi CHADEMA 2010-2015

Sheria ni msumeno: Rais Kikwete akisaini kwa mbwembe Sheria ya Gharama za Uchaguzi,ambayo Chadema wanamtuhumu kuikiuka na hivyo wanamwekea pingamizi.
Geofrey Nyang'oro na Lilian Mazula

SHERIA ni msumeno na sasa imgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete atalazimika kufanya kazi ya ziada isimdhuru baada ya Chadema kumwekea pingamizi rais huyo wa serikali ya awamu ya nne.Kikwete alisaini Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa mbwembwe mapema mwaka huu akitaka itumike mwaka huu, lakini Chadema imeitumia sheria hiyo kumwekea pingamizi, ikidai kuwa mgombea huyo wa CCM ameikiuka.

Katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Kikwete amekiuka sheria hiyo kwa kwa kutangaza ongezeko la mishahara ya wafanyakazi wa sekta ya umma akiwa kwenye mikutano ya kampeni.

"Wanasheria wetu wanashughulikia suala hilo kwa kusaidiana na naibu katibu mkuu, John Mnyika kukamilisha pingamizi hilo na kesho (leo) asubuhi tutawasilisha pingamizi letu kwa msajili wa vyama vya siasa,"alisema Dk Slaa ambaye pia ni mgombea urais kwa tiketi ya Chadema.

Dk Slaa alidai kuwa Kikwete alikiuka kipengele cha 6, sehemu ya 21 (1) cha sheria hiyo inayotoa tafsiri ya mambo yanayokatazwa wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea na kampeni za uchaguzi.

Alisema Kikwete amekiuka kifungu hicho kwa kutangaza ongezeko la mishahara ya wafanyakazi akiwa katika majukwaa ya kampeni, jambo ambalo linaweza kutafsiriwa na sheria hiyo kuwa ni rushwa ya uchaguzi.

Alieleza kuwa Kikwete amekiuka sheria hiyo kwa kuwa yeye kama mgombea, hana mamlaka ya kuongeza mshahara wa wafanyakazi katika kipindi hiki cha kampeni.
Dokta Slaa

"Kwa kutungwa kwa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na kusainiwa Julai 17 mwaka huu pamoja na marekebisho yake, tulitegemea kungesaidia kuleta mabadiliko," alisema Dk Slaa ambaye kitaaluma amebobea kwenye sheria.

"Kitendo cha Kikwete kukiuka sheria hiyo kimenishtua sana.

Watanzania tungependa kupewa ufafanuzi; fedha hizo za (mishahara) zimetoka wapi na kwa mamlaka ya nani kwa kuwa wenye mamlaka ya kuidhinisha matumzi ya fedha za umma ni Bunge," alisema Dk Slaa.
Alifafanua kuwa kwa mujibu wa katiba, Bunge ndilo lenye mamlaka ya kuidhinisha matumizi ya fedha ikiwa ni pamoja na ongezeko la mishara kwa wafanyakazi wa umma.

"Kitendo cha serikali kuamuru ongezeko hilo nje ya vikao vya bunge, ni ukiukwaji wa sheria za nchi na ndio mwanya uliosababisha kutoweka kwa fedha za Akaunti ya Madeni ya nje(EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT)," alisema Dk Slaa.

"Sehemu ya tano ya sheria hiyo sura ya 21.-(1) inaweka bayana vitendo vinavyokatazwa wakati wa uteuzi wakati wa kampeni za uchaguzi na inasomeka:

"(a)Kila mtu ambaye kabla au wakati wa kipindi cha kampeni, moja kwa moja au kwa namna nyingine yoyote, kupitia kwa mtu mwingine yeyote au kwa niaba yake, anatoa, anakopesha au anakubali kutoa au kukopesha, au anatoa, anaahidi au kumpatia au anajaribu kumpatia fedha yoyote au kitu chochote chenye thamani,

mpiga kura au kwa ajili ya mtu yeyote kwa niaba ya mpiga kura yeyote au kwa ajili ya mtu mwingine yeyote kwa nia ya kumshawishi kupiga kura, au kuacha kupiga kura au kumrubuni mtu yeyote kutendo hicho kwa niaba ya mpiga kura huyo kupiga kura au kuacha kupiga kura katika kura za maoni au uchaguzi wowote;

"Kikwete alisema yeye mwenyewe hahitaji kura za wafanyakazi, na akasisitiza katika hotuba yake iliyoitoa kwa wazee wa Dar es Salaam kuwa serikali haina uwezo wa kulipa mishahara hiyo na kama wanafanya hivyo kwa kushinikiza kigezo cha kura, yeye hazitaki; leo mishahara imeongezeka, fedha hizo zimetoka wapi?Tunataka utueleze matumizi hayo ya fedha za umma kinyume na utaratibu."

Kwa mujibu wa Dk Slaa mgombea urais anapaswa kulinda katiba na sheria zilizopo, ili kulifanya taifa liendelee kuwa katika hali ya amani na utulivu katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.

Dk Slaa alisema kuwa kitendo cha rais kutumia nafasi hiyo kutangaza mishahara kwenye kampeni ni kujipa upendeleo kwa kushawishi watu kumpigia kura kwa kutumia nafasi aliyonayo.

Dk Slaa pia alitumia fursa hiyo kukemea kitendo cha kufanya maamuzi kwa kukiuka sheria zilizopo akieleza kuwa kufanya hivyo kunaweza kuhatarisha usalama wa nchi.

Dk Slaa pia alienda mbali zaidi na kuituhumu CCM kwamba imekiuka taratibu za uchaguzi kwa kutengeneza mabango yake ya mgombea nchini Canada.

"CCM wametumia Sh1.5 bilioni kutengeneza mabango nje ya nchi kwa kutumia fedha za serikali pia ankara ya malipo "invoice" inaonyesha imeandikwa 'VAT INVOICE' kitu ambacho hakieleweki," alisema Dk Slaa.
Alisema kuwa ni muhimu CCM kutoa ufafanuzi juu ya hilo kwa kuwa ushahidi upo na unaonyesha kuwa kuna mchezo mchafu umeanza kufanywa.

CHANZO: Mwananchi

Inaelezwa kuwa vita vya mtandao (cyber war) ni tishio kubwa kwa Marekani kama ilivyo ugaidi.Na katika kujipanga vema kupambana na maadui wa nchi hiyo wanauweza kutumia mtandao kufanya mashambuli,Makao Makuu ya "Wizara" ya Ulinzi,Pentagon,imeanzisha mkakati wa kuajiri vijana wadogo wenye kipaji cha hali ya juu katika kuhujumu mtandao na kuufanya utekeleze matakwa ya mhujumu husika (hacking).


Katika kufanikisha zoezi hilo la kupata makuruta mwafaka,Pentagon ilisimamia shindano la uhujumu huo wa mtandao ambapo hackers vijana kadhaa walishiriki.Kichekesho ni kwamba katika kuonyesha uhodari wake katika fani hiyo,mmoj wa hackers hao alifanikiwa kuhujumu alama alizopewa na wasimamizi wa shindano hilo kabla matokeo hayajatangazwa.

Habari hii imenikumbusha kauli ya mwalimu wangu mmoja pale Mlimani,Profesa Ngware,aliyetupa "ukweli mchungu" kwamba "hivi kama wakati watoto wenu wanachezea vifuu ilhali wanangu wanacheza na kompyuta,mnatarajia watapokuwa wakubwa watakuwa na uwezo sawa wa akili?"









26 Aug 2010

Rostam Aziz
Katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005,mfanyabiashara controversial Rostam Aziz alitumia raslimali zake nyingi kuhakikisha mgombea wa nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete,anashinda kwa gharama yoyote ile.Na kutokana na utajiri mkubwa alionao pamoja na mbinu zake mbalimbali,mchango wake ulimsaidia sana Kikwete kuingia Ikulu,na sasa ni Rais wetu anayeomba tena ridhaa ya kutuongoza kwa miaka mitano ijayo.

Kati ya mwaka 2005 (baada ya Kikwete kuingia Ikulu) na sasa,Rostam ameibuka kuwa kiumbe mwenye nguvu za kutisha sio tu ndani ya CCM bali kwenye siasa za Tanzania kwa ujumla.Lakini kubwa zaidi katika kipindi hicho ni kwa mfanyabiashara huyo kuhusishwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi na Kikwete na serikali yake kushindwa kuwaridhisha Watanzania kwamba "hamkumbatii swahiba wake huyo".Haihitaji kurejea namna Rostam alivyohusishwa na ufisadi wa EPA (Kagoda) na ujambazi wa Richmond.
Jakaya Kikwete

Mwaka 2010,yaani mwaka huu,Rostam anaelekea kurejea tena ulingoni japo si kwa wazi sana.Ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuhusika kwa mfanyabiashara huyo katika kampeni za Kikwete.Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Rostam vimekuwa vikiendesha kampeni ya chuki dhidi ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa,mwanasiasa anayeonekana kuwa  tishio kwa mfanyabiashara huyo na vitendo vyake dhidi ya maslahi ya taifa.
Magazeti yanayomilikiwa na Rostam

Na kama hilo la vyombo vya habari vya Rostam kumuandama Dkt Slaa halitoi mwangaza wa kutosha basi taarifa kwamba mwandishi mwandamizi wa kampuni ya Habari Corporation (inayomilikiwa na Rostam),Muhingo Rweyemamu,anatajwa kuwa mratibu wa kampeni za Kikwete.Itakumbukwa kuwa mwaka 2005,waliokuwa waandishi waandamizi wa Habari Corporation,Salva Rweyemamu na Dokta Gideon Shoo walitumika sana kwenye kampeni hizo.Baada ya kuingia Ikulu,Kikwete "alimzawadia" Salva ukurugenzi wa habari wa Ikulu,nafasi anayoshikilia hadi sasa.
Muhingo Rweyemamu

Kama alivyo Salva,Muhingo anasifika kwa uwezo wake wa hali ya juu wa kujenga hoja.Kwa bahati mbaya au makusudi,uwezo huo pia unatumika ipasavyo kutengeneza fitna.Wengi watakumbuka namna Dokta Salim Ahmed Salim,mmoja wa wana-CCM waliokuwa wanawania kuchuana na Kikwete,alivyoundiwa zengwe kubwa na kumhusisha na kundi la Hizbu la huko Zanzibar.Inaelekea kuwa mbinu hizohizo zimeanza kutumika dhidi ya Dokta Slaa,na kuna kila sababu ya kuamini kuwa kuna mengi yatakayoibuliwa dhidi yake.
Salva Rweyemamu  (kushoto) na Gideon Shoo

Yayumkinika kuamini kuwa waandishi wa habari wanaotumiwa kumchafua Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanafanya hivyo kwa minajili ya "kupeleka mkono kinywani".Kubwa zaidi ni sapoti ya Rostam kwa Kikwete.Wakati mwaka 2005 alijibidiisha ili kufanikisha maslahi yake binafsi ya kibiashara (na amenufaika kweli-kwa kuangalia ishu za Kagoda na Richmond/Dowans) safari hii Rostam anahaha kumzuia Dokta Slaa kwa vile anafahamu fika kwamba laiti mwanasiasa huyo wa Chadema anayesifika kwa msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi akiingia Ikulu,zama za mafisadi kutumia jeuri yao ya fedha "kuendesha serikali kwa remote control" itakuwa imefikia kikomo.

Kwahiyo,Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanapaswa kuelewa kuwa safari hii Rostam ana "special mission" ya kuhakikisha "survival (kusalimika) yake.Atatumia kila raslimali aliyonayo kuhakikisha Dokta Slaa haingii Ikulu.Anafanya hivyo akifahamu wazi kuwa rais yeyote mwenye kujali maslahi ya nchi yake "atamkalia kooni" mfanyabisahara huyo na washirika wake.

Hata hivyo,kwa vile si fedha za Rostam au wanahabari wake zitakazopiga kura kwenye uchaguzi mkuu,bali mimi na wewe pamoja na kila Mtanzania aliyechoshwa kuona nchi yetu ikigeuzwa "shamba la bibi",ni muhimu kwa wapiga kura kusema HAPANA.Tusitoe fursa kwa watu wenye maslahi binafsi kuipeleka nchi yetu kwenye maangamizi.Na ni muhimu zaidi kutambua kuwa baadhi ya watu hao wana utata wa kutosha tu kuhusu asili ya mahali walipozaliwa.Hiyo inamaanisha kuwa "wakishaiingiza Tanzania kwenye mtaro",watakuwa na sehemu ya kukimbilia.

KILA MTANZANIA MWENYE KUITAKIA MEMA NCHI YETU ANAPASWA KUPAMBANA NA WAHUNI WA KISIASA WANAOTAKA KUTUWEKEA MADARAKANI VIONGOZI WANAOWAMUDU NA HIVYO KUENDELEA KUTUFISADI KAMA ILIVYOKUWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ILIYOPITA.


INAWEZEKANA,TIMIZA WAJIBU WAKO

Na Frederick Katulanda, Mwanza na Sadick Mtuly

LICHA ya sheria na kanuni za Uchaguzi kuzuia matumizi ya magari ya serikali, msafara wa mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete umetumia magari kadhaa ya serikali katika mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera.

Mbali na magari hayo, wakuu wa wilaya waliokuwa wameshiriki msafara wa mwenyekiti huyo wa CCM, walitumia magari yao ya kazi yakiwa yamewekwa namba binafsi huku wakivalia sare za chama hicho.

Ukiondoa magari maalumu ya walinzi wa mgombea huyo ambaye pia ni rais, magari mengine ya wakuu wa wilaya na wakuu wa idara mbalimbali za serikali, yalitumika na kuwekwa namba binafsi.

Kwa mujibu wa habari tulizozipata kutoka vyanzo vyetu zinaeleza kuwa hivi sasa Ikulu ya Dar es Salaam ina upungufu kwa kuwa wafanyakazi wa Ikulu hasa madereva pamoja na wapishi na wagawa vinywaji (waandazi), wanatumika katika kampeni za Rais Kikwete.

Wapishi na waandazi hao wamepelekwa mikoani kulingana na ziara za kampeni.

“Cha ajabu ni kuwa baadhi ya wafanyakazi wa Ikulu hasa madereva, wapishi na waandazi wanatumika katika kampeni za CCM kupitia Rais Kikwete.

“Wamegawanywa katika mikoa tofauti kulingana na ratiba za ziara za kampeni za rais,’’ kilisema chanzo chetu.

Juzi jijini Mwanza Mkuu wa wilaya Ilemela, Serenge Mrengo ambaye alifika majira ya saa 4:35 asubuhi uwanja wa ndege na gari lenye namba za STK 3551 huku wote wawili na dereva wake wakiwa wamevalia sare za CCM, lakini baada ya kusalimiana na viongozi wenzake, aliondoka.

Akiwa wilayani Geita, Mkuu wa wilaya hiyo Philemon Shelutete alitumia gari lake la serikali ambalo lilikuwa limebandikwa namba T 804 BCZ huku akiwa amevalia sare za CCM. Pia gari la Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Benson Katala lilitolewa namba za serikali na kubandikwa namba T 180 BKW.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro alitetea hatua hiyo akisema sio kosa kwa kuwa Kikwete bado ni rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanania.

Kandoro, alikiri kutumika kwa magari hayo ya serikali na kusema kuwa viongozi hao waliyatumia kumpokea na baadhi yao waliambatana naye katika ziara hiyo kwa kuwa mbali na kuwa mgombea wa CCM pia anayo hadhi ya urais.

“Huyu ni Rais, amekuja kama kiongozi licha ya kwamba anagombea, bado hajavuliwa urais, sasa ma-DC walikuja kama viongozi wa serikali kumpokea rais. Kama kuna mkuu wa wilaya alivaa shati la CCM alivaa kwa sababu ya mapenzi yake kwa chama,” alifafanua Kandoro ambaye alitumia gari binafsi la kiongozi mmoja wa CCM Kanda ya Ziwa.

"Makosa ni kiongozi wa serikali kufanya kazi za chama na sioni kama kuna kiongozi wa serikali ambaye alifanya kazi za chama,"alisema

Msafara wa Kikwete kuambatana na magari ya serikali haukuishia Mwanza na Geita pekee bali pia hata mkoani Kagera ambako magari mengi yalikuwa na namba za STK.

Katika hatua nyingine, uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando umetoa ufafanuzi kwamba uamuzi wake wa kutoa gari la kubebea wagonjwa katika msafara wa mgombea urais wa CCM kuhakikisha usalama wa mgombea huyo.

Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk Charles Majinge alisema kwa kawaida jukumu la kutoa magari huwa lipo mikononi mwa uongozi wa mkoa ambao uliomba gari kwao na wao waliamua kutoa gari hilo la wagonjwa namba T 848 AWN.

“Sisi hatutoi ambulance kwa wagombea, ila tulitoa kwa Kikwete kutokana na kuwa ni kiongozi wa nchi. Kutoa magari huwa ni kazi ya uongozi wa mkoa, lakini sisi kama watalaamu wa matibabu tulichukua tahadhari na kuweka gari hilo,” alieleza Dk Majinge.

Alisema kwa vile akiwa jijini Mwanza aliwahi kuanguka, basi waliamua kuchukua tahadhari kuepuka kukosa huduma haraka iwapo jambo hilo lingejirudia akiwa mbali na hospitali ya rufaa.

Akizungumzia gari hilo, Kandoro alisema uwapo wake ni utaratibu wa kawaida katika misafara ya viongozi wa serikali.

“Huu ni utaratibu wa kawaida katika misafara ya viongozi, tumetoa kama utaratibu wa kawaida….unajua huyu ni kiongozi wa nchi, sasa unataka wakija na wagombea wengine wa upinzani nao tuwapatie magari ya wagonjwa, wao ni akina nani?” alieleza na kuhoji Kandoro ambaye pia aligombea kura za maoni kuwania kuteuliwa na CCM kuwa mgombea ubunge Jimbo la Kalenga na kushindwa.

Akizungumza kwa sharti la kutotaja jina gazetini mmoja wa viongozi ambao walikuwa wakishughulika na kuratibu msafara huo alieleza kuwa gari hilo la wagonjwa ni lile ambalo lilitolewa na serikali ya Ujerumani chini ya ushirikiano wa Jiji la Mwanza na Wurzburg.

“Gari hili liliandaliwa kutokana na maofisa wa usalama kuliomba na hili agizo limetolewa katika mikoa yote ambako atafika, kwani katika kampeni anakuwa amekwenda hadi katika wilaya ambazo haina hospitali na ikitokea dharura akimbizwe haraka hospitali huku akiendelea kupatiwa matibabu” alieleza kiongozi huyo wa chama.

Hata hivyo, alisema gari hilo wao kama chama hawakuambiwa wala kuelekezwa kulilipia kwa vile ofisi ya mkoa ilisema watachukua wao katika hospitali ya Bugando, baada ya kuwasiliana na ofisi ya mganga mkuu wa mkoa.

CHANZO: Mwananchi

USHAURI: Imefika wakati sasa kukomesha uhuni huu wa CCM dhidi ya Watanzania hususan wale wasio wanachama wa chama hicho tawala.Matumizi yoyote ya mali za umma zinazogharamiwa na walipakodi pasipo kujali itikadi za vyama zao ni ubadhirifu wa wazi.Haitowezekana kuwa na uchaguzi huru na wa haki iwapo raslimali za taifa zinatumika kwa manufaa ya chama tawala,tena pasipo ridhaa ya walipakodi.Wito wa blogu hii kwa kila mpenda haki na usawa ni kuuweka wazi uhuni huu kwa dunia ili ifahamike mapema kuwa CCM inatengeneza mazingira ya kuhujumu uchaguzi mkuu ujao.

TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA


25 Aug 2010


Hongera nyingi kwako Mzee wa Changamoto Yetu kwa blogu yako kutimiza umri wa miaka miwili.Ama kwa hakika blogu yako ni miongoni mwa sehemu zinazofanya kuweko mtandaoni kuwa ni jambo la muhimu katika maisha yetu ya kila siku.Hekima na filosofia zako zinaamsha tafakuru kubwa,huku ukihakikisha tunamwayamwaya na burudani ya miziki mbalimbali.Kwa hakika,Changamoto Yetu ni miongoni mwa sababu zinazonifanya niendelee kupenda fani ya kublogu.

Kila andiko lililowekwa kwenye blogu yako katka kipindi hiki cha miaka miwili kimekuwa na manufaa makubwa kwa jamii.Ni dhahiri kuwa kila unapoandaa andiko la kuweka bloguni hapo unakuwa na picha ya sie wasomaji wako akilini na hivyo kufahamu maswali,kiu,mshawasha,na matamanio au mahitaji yetu mengine.

Kukupa sifa unazostahili inahitaji chapisho kubwa zaidi ya thesis ya PhD.Naomba pongezi hizi fupi ziwakilishe stahili zako zote kutokana na kazi mwanana unayoifanya kwa jamii.

Again,Hongera Sana na Happy Birthday.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.