28 Apr 2009

NKWAZI MHANGO
St John’s NL, Canada


AT last names are openly named! When Hon. Harrison Mwakyembe named Rostam Aziz as a suspect behind Kagoda profligacy, many scratched their heads. Some thought it was just politics. Others said: there must be something truly fishy. Others thought the government would wake up and bring him to book. Mwakyembe is a lawyer and an MP who knows what he is doing.

Before long, Reginald Mengi, the Executive Chairman of IPP, massively and openly weighed in with more damning allegations. He minced no words. He averred: Rostam, Yusuf Manji, Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel) who is facing EPA charges, Tanil Somaiya, and Subash Patel are the most corrupt people in Tanzania.

Today I’ll specifically look at two -Rostam and Manji. They’ve been stealing thunder when it comes to corruption save the government has pretended not to hear or see!
No doubt. The two are CCM bigwigs just like Mengi himself.

What makes things worse is the fact that the duo has been mentioned, though not openly, in almost all multi-million scams. I still remember how Manji was alleged to have swindled wananchi’s money, thanks to his business connections with NSSF. Though this was swept under the carpet, we still have more questions than answers.

Manji also tried hand in politics when he vied for Kigamboni Constituency backed by Yusuf Makamba - CCM’s secretary general who is said to have thick but suspicious bond with the duo.

As for Rostam, it’s an open secret. �He has been cowering before allegations connecting him with EPA theft thanks to being the mind behind Kagoda. Refer to the recent revelations by Bhyidinka Michael Sanze, a lawyer who presided over EPA authorization by Benjamin Mkapa - former president engrossed in many scams.

Also Rostam was linked with Richmond, thanks to his Caspian Company’s address being used by Richmond. He too was named by Ibrahim Msabaha as PM Edward Lowassa’s Arab in Richmond scam.

What damns so as to create doubts is the fact that, the duo, despite being mentioned in many scandals, still has much influence in CCM. They are awarded many lucrative tenders and other projects. They, too, are CCM’s financiers or donors. And this is the reason that forced the Father of the Nation Mwl. Julius Nyerere to sarcastically aver that CCM has been taken by corrupt business people. Who can step in Nyerere’s shoes.
Given that the government has been dragging feet in dealing with the buggers behind Kagoda, now it is aware who those buggers are. Will it go on keeping mum and acting indifferently as it sits on the same.

Silence is gold. But sometimes, it is admission of guilt. When Rostam was confronted by the media to shed light onto Mengi’s allegations, he’s quoted as thus. ’’Mengi is full of jealousy, hatred and what not. There is no way I can help him except to pray God and ignore all, for it is enough a punishment for him. Due to how I was brought up, I cannot quarrel with an old man.’’

Do such gimmicks address the allegations really. Let’s call shorts to white washing and be serious especially when allegations are damningly serious like these.

Though it can be lightly and wrongly perceived as racism and hatred for Mengi to name five Tanzanians of Asian decent as the most corrupt in the country, there is truth in this. Why should it be racism or hatred to aver they are corrupt but not when it comes to owning our economy Why not when they’re given tenders and other preferential treatments.

As Rostam once said that those alleging he is corrupt are labouring under racism, petty jealousy and hatred, but again, is it racism really or corruption.

Suspects should mount reasonable defence in lieu of taking camouflage under the colour of their skin. For example, if someone says Indians own a big chunk of national housing, will this be referred to as racism? If one avers that Indians own over 75% of commerce in the country, will it be branded hatred. If one avers that Indian and Chinese illegal immigrants and hawkers are favoured by authorities, will this be jealousy.

Indians own almost every lucrative business. And now they’ve already penetrated into politics, thanks to rotten takrima law. They live in government houses whilst its workers make do on the outskirts of the city. They’ve remained holier than us since they were brought in by colonialists.

We well know. Indian business moguls are almost behind every stinking lucrative government tender. Refer to the radar, presidential jet purchase, NSSF, Richmond, EPA and what not.

Many will wonder why. It is simple. Corrupt government officials prefer to do dirty business with Indians. They can not divulge their secrets. They’re easy to intimidate and repatriate when things go wrong as it happened in Chavda scam. So indigenous ’fisadis’ are left out of the big picture.

And if you look at whom Tanzania prefers to award citizenship to, you’ll find that Indians outsmart others. They still do the same- being middlemen-the job for which colonialists brought them. When white colonialists left and black ones took over, the role of Indians remained the same almost everywhere in Africa. Go to Kenya, Malawi, South Africa and elsewhere. Indians are still doing the same job-weakening the indigenous for the good of corrupt rulers.

So to avert wasting time, if Kikwete could take a leaf from Mengi, our war on corruption would make more sense than it is today when it is but white washing.

In other words, corruption in Tanzania is like ’mduara’ dance. It’s conspiracy between venal rulers and their corrupt guests. It’s time to rally behind Mengi to see to it that those ’fisadis’ are not harming him. Shall they, Mtikila’s gabacholi era will be latched onto. And the government must stop its indifference. The ’isadis’ it has been asking for are now given pro bono.
FOR MORE,VISIT HIM AT freethinking unabii



YAH,WANASEMA NI SUALA LA MTIZAMO: KUSEMA GLASI IKO HALF EMPTY AU HALF FULL.HABARI MBILI ZIFUATAZO ZINADHIHIRISHA MANTIKI YA MSEMO HUO.

Na Boniface Meena

UMAARUFU wa Rais Jakaya Kikwete unaonyesha kuendelea kuporomoka, kwa mujibu wa ripoti ya matokeo ya utafiti uliofanywa na taasisi ya Mpango wa Utafiti wa Elimu ya Demokrasia nchini (Redet).

Ripoti hiyo pia inaonyesha kuwa utendaji kazi wa Rais Kikwete, ambaye aliingia madarakani mwaka 2005 kuongoza serikali ya awamu ya nne, umeshuka kwa asilimia 28 mwaka jana ukilinganisha na matokeo ya utafiti ya mwaka 2006.

Pamoja na kushuka kwa asilimia hiyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi waliohojiwa wanaridhika zaidi na utendaji wa Rais Kikwete, kuliko wanavyoridhishwa na utendaji kazi wa baraza lake la mawaziri ambalo utendaji wake umekubaliwa na asilimia 18 tu.

Kwa mujibu wa utafiti huo, watu wanaoridhika sana na utendaji kazi wa Kikwete ni asilimia 39.5 tu kulinganisha na asilimia 69 iliyoonyesha kuridhika naye sana mwaka 2006.

Akitoa taarifa ya utafiti huo jana kwa waandishi wa habari, mtafiti mkuu wa Redet, Dk Benadetha Killian alisema kuwa ukilinganisha takwimu za Oktoba 2006 na Oktoba 2007, asilimia ya wale wahojiwa ambao wanasema wanaridhika sana na utendaji kazi wa Rais Kikwete imepungua kutoka asilimia 69 Oktoba 2006 hadi asilimia 44 mwezi Oktoba 2007 na sasa imefikia asilimia 39.5 hadi Novemba mwaka jana.

Dk. Killian alisema kuwa ukichambua undani wa mwenendo huo utaona kwamba wakati idadi ya wanaosema wanaridhika sana iliteremka kwa tofauti ya asilimia 23, kati ya mwaka 2006 na 2007, kasi ya kutoridhika sana imepungua ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2007/08 wakati idadi ya wahojiwa ambao walisema wanaridhika sana ilipungua kwa tofauti ya asilimia 4.5 tu.

Kwa mujibu wa Dk. Killian, ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya utafiti huo ulifanyika katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na sampuli ilichaguliwa katika ngazi tatu ambazo ni wilaya na vijiji/mitaa na katika kila ngazi sampuli ilipatikana kwa kutumia mtindo wa sampuli nasibu.

"Katika kila wilaya, watafiti walitakiwa kuchagua vijiji viwili (kwa maeneo ya shamba) au mitaa miwili (kwa maeneo ya mjini) kwa kutumia njia ya sampuli nasibu. Katika kila wilaya, jumla ya watu 50 walichaguliwa kwa ajili ya kuhojiwa, 25 kutoka kila kijiji/mtaa," alisema.

"Na kati ya watu 50 waliohojiwa katika kila wilaya, 25 walitakiwa wawe wanawake na wengine 25 wawe wanaume na uchaguzi wote wa wahojiwa ulifanyika kwa kutumia njia ya sampuli nasibu."

Alisema ukiacha masuala mengine ya utendaji wa mawaziri, waliohojiwa walitakiwa kutoa tathimini yao kuhusu utendaji kazi wa Rais Kikwete katika kipindi cha takriban miaka mitatu ya utawala wake kwa kutoa maoni yao kama wanaridhika sana, wanaridhika kiasi au hawaridhiki.

Dk. Killian alisema kati ya wote waliohojiwa, asilimia 39.5 walisema wanaridhishwa sana na utendaji wa Rais Kikwete, asilimia 39.0 walisema wanaridhika kiasi na asilimia 19.3 walisema hawaridhiki na utendaji kazi wa mkuu huyo wa nchi.

Alisema hata hivyo kwa ujumla, matokeo ya utafiti wa Novemba mwaka jana yanaashiria kwamba, utendaji kazi wa Rais Kikwete bado unaonekana kuridhisha idadi kubwa ya watu pale ambapo makundi mawili ya wahojiwa yanapojumlishwa pamoja yaani wale wanaosema wanaridhika sana asilimia 39.5 na wale wanaosema wanaridhika kiasi asilimia 39 ikiwa inafanya idadi hiyo ya wahojiwa wote kufikia asilimia 78.5.

Dk Killian alisema sababu za kuridhika au kutoridhika na utendaji kazi wa serikali ya Rais Kikwete ni kutoridhishwa na ahadi yake ya kuboresha hali ya maisha. Asilimia 31.0 ya waliohojiwa walisema ameshindwa kuboresha hali ya maisha, wakati asilimia 24 walisema hajatimiza ahadi na asilimia 12.2 walisema hafuatilii utekelezaji wa ahadi zake.

"Sababu nyingine zilizotolewa na wahojiwa ni kuchagua viongozi wasiofaa asilimia 10.8, ameshindwa kupambana na rushwa asilimia 8.0, lakini pamoja na kwamba utafiti huu ulifanywa kipindi ambacho "vigogo" walikuwa wanapelekwa mahakamani kuhusiana na tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na wengine kutuhumiwa na wizi wa fedha za akaunti ya madeni ya nje (EPA), ni asilimia 6 tu ndiyo waliotaja moja kwa moja suala hili kama sababu ya kutoridhishwa au kuridhishwa kiasi na utendaji kazi wa rais," alisema.

Alisema sababu za wananchi kutoridhika na utendaji wa serikali iliyo madarakani ni kutofuatilia utekelezaji asilimia 30.7, serikali kujihusisha na rushwa asilimia 29 na inapitisha mikataba mibovu asilimia 10.0.

Utafiti huo pia unaonyesha kuwa bunge ndio linaongoza kwa kutoridhisha wananchi baada ya asilimia kubwa ya waliohojiwa kueleza kuwa hawaridhishwi na taasisi hiyo ya kutunga sheria.

Bunge limeonekana kutoridhisha wengi tofauti na taasisi za serikali kama polisi, taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini, serikali za mitaa na kadhalika.

Dk. Killian alisema bunge linaongoza kwa kuwa na asilimia kubwa ya kiwango cha kutoridhika ambacho ni asilimia 77.4, ikifuatiwa na serikali za mitaa asilimia 75.6 wakati baraza la mawaziri linashika nafasi ya tatu kwa asilimia 63.

Kwa upande wa utendaji kazi wa Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar, utafiti unaonyesha kuwa asilimia 44 tu ya wote waliohojiwa wanaridhika sana, wakati asilimia 24 wanaridhika kiasi na asilimia 26 walisema hawaridhiki.

Alisema kiwango cha utendaji wa Rais Karume kimeonekana kupanda kwa asilimia 9 ukilinganisha na utafiti wa Oktoba 2007 wakati asilimia 35.5 tu ilimkubali baada ya kuporomoka kutoka asilimia 47.8 aliyopata kipindi cha hadi Oktoba 2006 na baadaye kupanda kutoka asilimia 35.5 Oktoba 2007.

CHANZO: Mwananchi



Nyota ya Kikwete Bado Yang'ara
na mwandishi Wetu


Watanzania walio wengi, zaidi ya asilimia 80, bado wana imani na Rais Jakaya Kikwete, kuliko miaka minne iliyopita alipochaguliwa kuwa Rais. Pia asilimia kubwa ya Watanzania inaridhishwa na utendaji kazi wa Rais na Serikali yake.

Kura ya maoni iliyoendeshwa na taasisi ya uchunguzi inayojitegemea ya REDET kuhusu utendaji wa Serikali ya Kikwete katika miaka mitatu iliyopita ya uongozi wake, inaonyesha kuwa asilimia 83.7 ya Watanzania wana imani naye.

Kundi hilo la Watanzania wanaothibitisha kuwa na imani na Rais Kikwete likigawanywa katika makundi ya ulinganisho wa imani, asilimia 50 inasema ina imani sana kwa kiongozi huyo, asilimia 33.7 inasema ina imani kiasi cha kutosha kwake.

Asilimia hiyo ni kubwa kuliko ile ya ushindi wa urais mwaka 2005, alipochaguliwa kwa kishindo ambapo alichaguliwa kwa asilimia 82. Hakuna mwanataaluma yeyote wa REDET ambaye alikubali kuzungumza na gazeti hili kuhusu kura hiyo ya maoni licha ya kupatikana kwa nakala ya matokeo ya utafiti huo.

Lakini habari zinasema matokeo kamili ya kura hiyo yanatarajiwa kutangazwa rasmi wiki ijayo na uongozi wa REDET. Kubwa zaidi katika ripoti hiyo, ni ukweli kuwa asilimia ya Watanzania wenye kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Kikwete bado iko juu.

Utafiti huo wa kisayansi na wa kina uliofanyika katika sehemu mbalimbali za nchi mijini na vijijini unaonyesha kuwa asilimia 78 ya Watanzania wanaridhishwa na utendaji kazi wake. Matokeo ya kura hizo yamethibisha kwa mara nyingine, ukweli ambao umebakia bila kubadilika kuhusu imani ya wananchi kwa Rais Kikwete na utendaji wake tangu alipoingia madarakani.

Kura zote za maoni ambazo zimefanyika tangu wakati huo, zimekuwa zikionyesha kuwa kiwango cha imani ya wananchi wake na kwa utendaji kazi wake kimebakia kwenye eneo la asilimia 80. Kura hizo pia zinaonyesha kuwa imani ya wananchi kwa wasaidizi wake wakuu ni ya juu.

Zinaonyesha pia kuwa asilimia 82.7 wana imani na Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein akiwa nyuma ya Rais kwa asilimia moja, wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda anavutia asilimia 84. Utafiti huo pia unathibitisha kuwa wananchi kiasi cha asilimia 70 wana imani na Baraza la Mawaziri, wakati asilimia 66 wana imani na wakuu wa mikoa. Imani ya wananchi inashuka kidogo kwa Bunge ambalo lina asilimia 65.

Katika namna ambayo pia itakipa nguvu na kuifurahisha CCM, asilimia ya Watanzania ambao wanasema wanaridhishwa na utendaji kazi wa chama hicho ni 72.8 wakati asilimia 75.6 wanasema wana imani na chama hicho. Matokeo hayo yatakifurahisha chama hicho kwa sababu asilimia hiyo kubwa ya kukubaliwa na Watanzania imebakia ya kiwango hicho hicho kwa karibu miaka 17 tangu kuanzishwa kwa vyama vya upinzani nchini.

Mwaka 1992 wakati CCM na serikali zilipoongoza mageuzi ya kuingia katika mfumo wa vyama vingi, ilikuwa baada ya uchunguzi uliothibitisha kuwa ni asilimia 20 tu ya Watanzania waliokuwa wanataka mfumo wa vyama vingi. Kwa namna moja au nyingine, asilimia hiyo imebakia na kujithibitisha mara nyingi kupitia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupitia uchaguzi mkuu ambao umefanyika tangu wakati huo na hasa uliopita uliomwingiza Rais Kikwete madarakani mwaka 2005. Kwa upande wa vyama vya upinzani, asilimia ya Watanzania ambayo inasema haina imani na vyama hivyo inabakia juu kwa asilimia zaidi ya 31.



CHANZO: HabariLeo



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































27 Apr 2009


KUNA MAMBO YANAYOTOKEA HUKO NYUMBANI YANAKERA KUPITA MFANO.HIVI HAWA WATANZANIA WENZETU WALIOKABIDHIWA DHAMANA YA KUTUONGOZA (TUKIAMINI KABISA KUWA WANA UPEO MZURI TU WA KUTAFAKARI MAMBO) WANAWEZAJE KUONGEA MAMBO YA AJABU NAMNA HII?ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA KISHA TUENDELEE KUJADILI



* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza

Ramadhan Semtawa na Leon Bahati

MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.

Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".

Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.

Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.

Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.

Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"

Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.

"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."

Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.

"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."

Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.

Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.

Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi
.

Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.

"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.

Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.

Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.

Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.

Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.

Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.


CHANZO: Mwananchi


HALAFU TUKISEMA UFISADI NI MIONGONI MWA SERA ZA CCM TUTAITWA WACHOCHEZI?CHADEMA WALIPOTOA LIST OF SHAME CCM,KAMA KAWAIDA YAKE,IKAJA JUU KUDAI HIZO NI POROJO ZA KISIASA.WENGINE WAKAENDA MBALI ZAIDI NA KUTISHIA KUWAPELEKA AKINA SLAA MAHAKAMANI KWA MADAI YA "KASHFA".HADI LEO HAKUNA HATA MMOJA WAO ALIYEKWENDA MAHAKAMANI,NA SANASANA BAADHI YA WATUHUMIWA HAO KWA SASA WAKO MAHAKAMANI WAKITUHUMIWA KUHUSU YALEYALE YALOTAJWA KWENYE LIST OF SHAME.


TATIZO LA MAWAZIRI WOTE WAWILI SIO MANJI AU THE PATELS.NI MR UNTOUCHABLE.HUYU AKIGUSWA BASI NDIO KAMA UMEPIGA LUMUMBA,HQ YA CCM.HAIHITAJI UPEO WA JUU KUBAINI KUWA WANACHOONGEA MAWAZIRI HAO WAWILI NI SAWA NA SELF-DENIAL.YAANI TUKIMJUA MWIZI TUSIMUITE MWIZI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI?TUTAMFIKISHAJE HUKO PASIPO KUMTUHUMU IN THE FIRST PLACE?


NA KWANINI ALALAMIKE WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA NA SIO HAO WALIOTAJWA NA MENGI?WAMETUMWA AU WANATUMIWA?WASITUFANYE WATOTO KUHUSU HABARI ZA HAO MAPAPA WA UFISADI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA VILE HILO HALIWEZEKANI.KWANI KUNA SABABU NYINGINE INAYOSABABISHA KUSUASUA KUWATAJA WAMILIKI WA KAGODA ZAIDI YA UKWELI KUWA AMONG THE WAMILIKI NI MR UNTOUCHABLE?


AH,SIJUI MAMBO HAYA YATAENDELEA HADI LINI!

Neighbours of a woman who ended up in court for her noisy love-making were savouring peace and quiet today after she was locked up accused of breaking her anti-social behaviour order.

Caroline Cartwright, 48, was remanded in custody until May 5 charged with three breaches of her Asbo in just 10 days. The four-year order was imposed by magistrates in Sunderland on April 17 and prevented Cartwright 'making excessive noise' anywhere in England
...continue


Judges could be forced to bow to Sharia law in some divorce cases heard in Britain.

An EU plan calls for family courts across Europe to hear cases using the laws of whichever country the couple involved have close links to. That could mean a court in England handling a case within the French legal framework,or even applying the laws of Saudi Arabia to a husband and wife living in Britain...
continue

As many as one in five British couples sleep in separate beds. According to a recent survey, snoring, tossing and turning, and talking in your sleep were cited as the main irritants, with ever more stressful careers and lives that demand a good night's rest making us increasingly reluctant to put up with them. But does choosing to sleep apart sound the death knell of intimacy? ...continue

Facebook messages, texts and internet addresses will all be logged and stored under new laws proposed by the Home Secretary today.Jacqui Smith said phone and internet providers would be legally obliged to retain records of customers' calls and internet usage.

However, the proposed plans fell short of a widely-predicted centralised database containing email, phone and web data.The information, to be stored for a year at a cost of £2bn, would be available to police in the event of criminal investigations...continue

MOJA YA MAENEO KOROFI KATIKA BARABARA KUU WILAYANI KILOMBERO.UNGETEGEMEA VIONGOZI WA WILAYA HIYO WAELEKEZE NGUVU ZAO KWENYE KU-ADDRESS SHIDA ZA WANANCHI (KAMA HIYO YA BARABARA) BADALA YA KUTAKA KUUZA ARDHI YAO.HUU NI UNYAMA USIOKUBALIKA HATA CHEMBE.ANYWAY,2010 IS COMING.I HOPE UKATILI HUU WA VIONGOZI WABABAISHAJI UTAKUWA SABABU TOSHA YA KUWAPIGA CHINI KWENYE UCHAGUZI.

na Mwandishi Wetu, Kilombero

KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.

Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.

Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.

Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.

“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.

“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.

Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.

Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.

Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.

“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.

Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.

Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.

“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.

Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.


THIS IS BECOMING PERSONAL!TATIZO LA WILAYA YETU (NA JIMBO LA KILOMBERO KWA UJUMLA) NI KAMA HATUNA MBUNGE.KUNA JAMAA ANAITWA LIGALAMA.I JUST CANT UNDERSTAND WHAT THIS GUY HAS BEEN DOING!BADALA YA VIONGOZI KUWEKEZA NGUVU ZAO KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO WAO WANAENDEKEZA USHKAJI NA WAWEKEZAJI....NA HAIHITAJI UTAFITI KUFAHAMU KUWA KICHOCHEO KIKUBWA HAPO NI RUSHWA NA UFISADI KWA UJUMLA.

26 Apr 2009


KUNA kila dalili kuwa taifa halielekei pazuri hasa baada ya siku za hivi karibuni kuibuka matukio kadhaa ambayo kwa kiasi kikubwa yameishtua jamii kiasi cha kuhoji taifa linakoelekea.

Matukio ya kiongozi wa nchi kudhalilishwa kwenye mtandao wa kompyuta, malumbano ya wabunge juu ya kuvuja kwa siri za serikali na kuanikwa kwa mishahara yao pamoja na hatua ya Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kutaja majina ya watu anaowatuhumu kuwa mafisadi ‘papa’ hadharani.

Kutokea kwa matukio hayo katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwakani kumeelezwa ni mambo ambayo kwa kiasi kikubwa yanaweza kuliyumbisha taifa.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii wanayaona matukio hayo kama ni mapambano ya hatari yanayowahusisha baadhi ya wafanyabiashara na vigogo wa siasa ambao katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakitumia njia mbalimbali kuhakikisha wanafanikisha mikakati ya kuongoza.

Tukio la Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kuwataja baadhi ya wafanyabiashara na wanasiasa maarufu hapa nchini kuhusika na kashfa za ufisadi limezua mtafaruku miongoni mwa jamii ambapo baadhi ya watu wanaiona hatua hiyo ni mapambano ya hadharani baina ya pande hizo mbili.

Mapambano hayo ambayo katika siku za hivi karibuni yamefikia hatua mbaya kiasi cha kuanza kuhusisha uandishi wa habari usiozingatia maadili ya fani ya habari umeonekana kutumika kwa ajili ya kukashfu na kudhalilisha utu wa baadhi ya walengwa.

Vita ya pande hizo mbili vinaonekana kuanza kushika kasi na kuna habari kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi wamejipanga kujibu mashambulizi hayo kwa gharama zozote zile.

Wakati mapambano hayo yakionekana ni ya pande mbili wanasiasa, wafanyabiashara na wananchi mbalimbali wamejikuta ama wanaunga mkono upande mmoja au mwingine hali inayozidisha utete wa vita hivyo.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii wamebainisha kuwa hali hii ya sasa imekuja hasa baada ya ufisadi wa EPA, Meremeta, Richmond na kadhalika ambao ulisababisha baadhi ya viongozi akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa kujiuzulu.

Kujiuzulu kwa viongozi hao na kufikishwa mahakamani kwa baadhi ya watuhumiwa walioshiriki katika kashfa hizo na za matumizi mabaya ya madaraka kumechochea vita dhidi ya ufisadi huku baadhi ya wananchi wakitaka pia Rais wa mstaafu, Benjamini Mkapa, naye aondolewe kinga ili aweze kujibu tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.

Hatua ya Mengi kujitokeza hadharani na kutaka majina ya watu anaowatuhumu kwa kashfa za ufisadi na baadhi ya wabunge kuwachachamalia watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi nako kumezidisha joto na hofu ya mapambano hayo.

Wakati mawazo ya watu yakiwa bado katika mzozo huo, limetokea tukio jingine la kusikitisha katika mtandao ambapo kiongozi wa nchi amejikuta akidhalilishwa kwa picha zisizofaa mbele ya jamii.

Tukio hilo kwa kiasi kikubwa linaonyesha ukosefu wa ustaarabu na maadili kwa baadhi ya watu ambao wameamua kutumia vibaya teknolojia ya kisasa hususan upashanaji habari kwa kutumia mtandao.

Jambo hilo kwa kiasi kikubwa limekuwa likihusishwa na mbinu za kuchafuliana majina hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi na kubainishwa kuwa kama hatua za haraka za kuwakamata wanaohusika na mitandao hiyo zisipochukuliwa kuna hatari ya viongozi wengi zaidi kudhalilishwa kupitia mambo mbalimbali.

Moja kati ya tukio la udhalilishaji wa viongozi ni hatua ya kijana mmoja kuamua kumpiga kofi Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, katika sherehe za Maulid zilizofanyika kwenye Ukumbi wa Daimond Jubilee, Dar es salaam.

Sakata jingine ambalo limeonekana kuwagawa zaidi Watanzania na wanasiasa ni kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma, kuwa kuanzia sasa wabunge na watendaji wote watakaovujisha siri za serikali watashughulikiwa ipasavyo.

Kauli hiyo ambayo ilionekana kumlenga Mbunge wa Karatu Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA) na baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakitumia nyaraka mbalimbali zinazodaiwa kuwa za siri kuiumbua serikali sasa watakumbana na mikono ya sheria endapo watakutwa na nyaraka hizo.

Kauli hiyo imeonekana kupingwa na wananchi wengi kwa madai kuwa sasa serikali inataka kuwa ya kidikteta hasa kwa kuficha nyaraka za ufisadi uliofanywa au unaofanywa na viongozi waliopo na waliomaliza muda wao madarakani.

Baadhi ya wananchi wamekuwa wakiihusisha kauli hiyo kama ni njama za kuficha uovu ambao umekuwa ukipoteza fedha nyingi za Watanzania kupitia rasilimali mbalimbali.

Mshangao huo wa wananchi uliongezeka zaidi pale baadhi ya wabunge walimshutumu hadharani Dk. Slaa kwa kubainisha vipato wanavyovipata wabunge na kutaka fedha hizo zipunguzwe ili zitumike kwa maendeleo ya wananchi.

Baadhi ya wabunge walimtuhumu Dk. Slaa kwa kutaka kujitafutia umaarufu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu ujao jambo ambalo limepingwa vikali na wananchi wanaoonekana kukubaliana na ushauri wa Dk. Slaa.

Matukio haya kwa kiasi kikubwa kwa namna moja au nyingine yanaonyesha kuliweka taifa katika sehemu mbaya na iwapo kama hatua za kurekebisha baadhi ya mambo hazitachukuliwa kuna kila dalili za kutokea mpasuko mkubwa miongoni mwa jamii.

Naye Rahel Chizoza anaripoti kutoka Dodoma kuwa sakata la wizi wa nyaraka za serikali na kuwekwa hadharani kwa mishahara minono na marupurupu wanayopata wabunge kulikoibuliwa na Mbunge wa Karatu Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA), hivi karibuni limechukua sura mpya baada ya baadhi ya wabunge kuonyesha kumchukia mbunge huyo.

Hali hiyo imejitokeza jana kwenye semina ya maboresho ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma iliyoendeshwa kwa wabunge ambao baadhi yao walionyesha hali ya kumbeza mbunge huyo aliposimama kwa ajili ya kuchangia hoja.

Hali hiyo ilisababisha mwenyekiti wa semina hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje, kuingilia kati na kuwasihi wabunge kupunguza minong’ono.

“Hivi hizi nyaraka zinazodaiwa kuwa ni za siri, kwa nini zinawekwa kwenye makabati ya serikali, naomba Katibu Mkuu aniambie kama ni halali kwa nyaraka za wizi kuwepo katika kabati za serikali,” alihoji Dk. Slaa

CHANZO:Tanzania Daima

25 Apr 2009


DECI....DECI...DECI.NDIO GUMZO HUKO NYUMBANI.LAKINI KUNA MENGI YANAYOHITAJI TAFAKURI PANA KUHUSU SUALA HILO.TRULY YOURS NIMEJARIBU KUCHANGANUA SUALA HILO KWA UNDANI KIDOGO.ANGALIA HAPO JUU KULIA KWENYE SECTION YA AUDIO USIKIE UCHAMBUZI HUO.NIRUSHIE BARUA-PEPE TUENDELEZE MJADALA KWA MANUFAA YA TAIFA.NA KAMA NIMECHEMSHA,USISITE KUNIKOSOA.
KARIBUNI SANA!!!



MZALENDO MMOJA AMENITUMIA UJUMBE UFUATO KWENYE E-MAIL,NAMI NAOMBA KUUWASILISHA KAMA ULIVYO:


Kuna habari kwamba mmoja wa wafanyabiashara aliyetajwa na Mkurugenzi wa IPP Bwana Reginald Mengi amenunua hisa nyingi za umiliki wa kituo cha kurusha matangazo ya Television.

Mfanya biashara huyo inasemekana ni yule aliyetumia mtindo huohuo kununua hisa za kampuni iliyokuwa inatoa gazeti lilikuwa maarufu kabla ya mwaka 2005 na sasa si maarufu tena.

Mfanyabiashara huyo ambaye ana hisa kwenye kampuni moja ya simu za mikononi inasemekana ana mpango wa kutumia minara ya kampuni hiyo ya simu ili kusambaza matangazo ya kituo hicho nchi nzima kwa urahisi na bila gharama kubwa.

Kwa vile kampuni yake ndiyo yenye mtandao mkubwa hapa nchini basi itakuwa ni rahisi kwake kusikika nchi nzima kuzidi vyombo vyote vya habari.

Iwapo mpango huo utatekelezwa basi mfanyabiashara huyo atakuwa anaongoza kusikika eneo kubwa nchini.

Bwana Mengi ina ITV na Redio zake tabidi avute bidii ya kasi kwa sababu yeye hataweza kuwa na mtandao mkubwa kama hiyo TV.

Wenu mtafuta habari

24 Apr 2009


Boniface Meena na Mkinga Mkinga

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.
>
Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".

Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. " Biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ovyo." Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

“Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.>
"Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi."

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.

CHANZO:Mwananchi

22 Apr 2009


Na Waandishi Wetu

VURUGU kubwa zimeibuka katika Makao Makuu ya taasisi ya Development of Entrepreneurship for Community Initiative (Deci), wanachama wake walipokuwa wakigombea kuingia ndani ya ofisi hizo kuorodhoresha majina yao kwa ajili ya kung’oa mbegu walizopanda.

Kati msongamano wa wanachama waliokuwa wakigombea kuingia ndani ya ofisi za taasisi hiyo jana; baadhi ya watu walianguka chini, kumi kati yao walipoteza fahamu na saba walinusurika kufa baada ya kutumbukia kwenye kisima cha maji kilichopo katika eneo hilo.

Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa watu hao walianza kusukumana kwenye lango la kuingilia ndani ya ofisi hizo, muda mfupi baada ya kufunguliwa na kukaidi amri ya kufuata foleni iliyotolewa na muhudumu wa Deci.

Walisema baada ya wanachama hao kukaidi amri hiyo, walijazana kwenye mlango wa kuingilia ndani ya ofisi hizo na ndipo walinzi wa kampuni binafsi wanaolinda ofisi hizo walitumia nguvu kuwarudisha nyuma wanachama hao bila mafanikio.

“Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya walifunga mlango wa kuingilia na shughuli za taasisi hiyo kusimamishwa kwa muda,” alisema mmoja wa mashuhuda.

Alisema ofisi zilisitishwa kuanzia saa 3:00 hadi saa 4:05 zilipofunguliwa baada ya kuwasili kwa askari polisi kutoka Kituo cha Magomeni.

Polisi hao wakiwa na silaha waliwasili kwenye ofisi hizo na kuingia ndani kupitia katika mlango uliokuwa umezingirwa na umati wa watu, ili waweze kuwalazimisha kufuata foleni.

Hata hivyo, zoezi hilo lilizidi kuwa gumu bada ya watu hao kuendelea kusukumana mlangoni hapo licha ya polisi kuingia ndani ya ofisi hizo na wahudumu wa Deci kutangaza kuwa wanachama waliopanda mbegu zao Machi mosi hadi 10, mwaka huu kuwa ndio wanatakiwa kuingia kupata huduma.

Kutokana na vurugu kuongezeka, ofisi hizo zilifungwa tena saa 7:45 mchana na kuwataka wanachama waondoke hadi kesho saa 2:00 asubuhi.

Hata hivyo muhudumu aliyekuwa anatoa taarifa kwa wanachama hao aliwataka kutofuata ratiba iliyoandaliwa na taasisi hiyo awali ya kuwahudumia waliopanda mbegu zao Februari. Badala yake aliwataka waliopanda mbegu zao kuanzia Machi mosi hadi 5, mwaka huu ndio watatakiwa kwenda kujiorodhesha leo.

Mmoja wa wanachama waliotumbikia kwenye kisima, Getruda Moto aliliambia Mwananchi kuwa akiwa na wenzake, alishituka baada ya mbao alizokuwa amesimamia juu yake zikizama.

“Mimi nilikuwa nimesimama pembeni, lakini kuna watu walikuja na kukanyaga mbao iliyogusa kwenye mgomba, ndipo ikatengua mbao zilizoegeshwa kwenye kisima hiki na mimi pamoja na wenzangu kutumbukia,” alisema Moto.

Hata hivyo alisema mara baada ya kuokolewa alifarijiwa na wanachama wenzake, wakimtaka asiilaumu Deci, bali serikali ambayo ndiyo chanzo cha yote hayo.

“Usiilaumu Deci hii haikudhamiria kufanya haya bali ni serikali iliyoifunga na kusababisha yote haya” alisema mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana.


Mchungaji wa Kanisa la Sharoom Gospel la Yombo Buza, Kamiliusi Macha ambaye ni mmoja wa wanachama wa Deci aliilalamikia serikali kwa kutoweka ulinzi wa kutosha katika eneo hilo linalokusanya umati mkubwa wa watu.

“Hapa walitakiwa kuwepo askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU), ndiyo wangeweza kuwalazimisha wanachi kupanga foleni na hali hii ya wanachama ya kujazana mlangoni isingekuwapo,” alisema Macha.

Akizungumzia kampuni hiyo alisema kwa sasa inakatisha tamaa kwani taarifa zake ni za kutatanisha. Ofisi hizo pia ziligubikwa na kila aina ya vituko baada ya vibaka kuibuka na kuwaibia watu simu za mkononi pamoja na risiti zao za Deci.

Mwanachama mmoja aliporwa risiti zote za Deci zenye thamani ya Sh 200,000 akiwa nje ya makao makuu ya ofisi hizo. Mwanachama huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema aliporwa karatasi hizo alizokuwa amezishika mkononi na kuachiwa karatasi ya ratiba.

Alisema mara baada ya kuporwa stakabadhi hizo alikwenda kituo cha polisi cha Urafiki kutoa taarifa, lakini alipofika huko aliambiwa arudi katika ofisi za Deci ambako angepewa barua ya utambulisho.

Hata hivyo juhudi za kupata barua hiyo zilishindikana baada ya watendaji wa Deci kukataa kufungua mlango wa ofisi hizo kwa madai kuwa muda wa kufanya kazi ulikuwa umemalizika.

“Nifungulieni mimi nimeibiwa naomba mnisaidie, nimeshaenda polisi nimeambiwa nije huku mniandikie barua,” alilalamika bila mafanikio baada ya sauti kutoka ndani ya ofisi hizo ikidai muda wa kazi umeisha.

Mwenyekiti wa kamati ya dharura ya wanachama wa Deci, Mchungaji Isaack Kalenge alifika katika ofisi hizo na kuwatangazia wanachama juu ya mkutano wao utakofanyika Jumamosi wiki hii kuanzia saa 7:00 katika viwanja vya Jangwani na kuwataka wanachama wote kufika bila kukosa.

Kabla ya kufika katika ofisi hizo mkutano aliokuwa ameuitisha na waandishi wa habari Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, ulivunjwa na maofisa wa maelezo kwa kushirikiana na maafisa usalama, baada ya mchungaji huyo kutoa kauli iliyodaiwa kumdhihaki Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Mkutano huo ulivunjwa baada ya mchungaji huyo kusema kuwa kauli ya Waziri Mkuu kuwa Deci ina Sh1.8 bilioni katika akaunti yake badala ya 54bilioni zilizotajwa na viongozi wa taasisi hiyo, ni ya kuropoka na kupotosha umma.

Kauli hiyo iliwaudhi maofisa wa maelezo hivyo kumtaka aache kuongea habari za viongozi wa taasisi hiyo, hata wa serikali badala yake kusoma maandishi aliyoyaandika katika karatasi yake.

“Wewe siyo kiongozi wa Deci hivyo unatakiwa kuzungumzia masuala yako binafsi kwa kuwa ni mwanachama wa taasisi hiyo, si kumdhihaki na kumtukana Waziri Mkuu,” alisikika kiongozi mmoja wa maelezo na kuamsha kelele kutoka kwa waandishi waliokuwepo katika mkutano huo.

Hata hivyo mchungaji huyo aliitaka serikali kupitia Wizara ya Fedha kuwajengea wananchi mazingira ya kupata fedha zao.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alimtaka mchungaji huyo kufuata utaratibu uliowekwa na jeshi hilo kabla ya kufanya mkutano wake Jumamosi ijayo kwa kuwa kufanya hivyo bila kibali ni kukiuka Sheria namba 322 ya Jeshi la Polisi iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002.

Katika tawi la Deci lililopo maeneo ya Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam umati mkubwa wa wanachama ulikusanyika huku ukiulalamikia utaratibu wa kujiandikisha majina na kuacha risiti mpaka siku ya kurudishiwa fedha zao.

Mwananchi lilishuhudia washiriki hao wakizozana na baadhi ya viongozi wa tawi hilo na kuwalazimu kubadili uamuzi huo kwa kubandika tangazo ambalo lilikuwa linaonyesha utaratibu wa malipo kwa waliopanda mbegu kuanzia Oktoba mwaka jana mpaka Aprili, mwaka huu.

“Hatutaki kabisa kuacha risiti hapa kwani ikifika siku ya malipo mtaturuka. Tunasema hatutaki, nyie tuambieni siku ya kuja kuchukua fedha zetu, tutakuja na risiti zetu,” walisema washiriki hao.

Wakati hayo yakiendelea Deci katika taasisi nyingine ya Malingumu Investment iliyopo maeneo ya Ukonga karibia na lilipo tawi la Deci wanachama wake walionekana wakiendelea kupanda kama kawaida.

Mwananchi lilifika eneo hilo saa tisa alasiri ilikuta wanachama wa taasisi hiyo wakigombania kuingia ndani, huku wakiwa wanazuiwa na walinzi wa kampuni binafsi waliokuwa wakilinda eneo hilo.

CHANZO: Mwananchi
Baadhi ya washiriki hao walikuwa na nia ya kung’oa mbegu zao kwa kuhofia taasisi hiyo kufungiwa kama ilivyofungiwa Deci.



KWA MFANO KATINA GAZETI LA SANI KUNA HABARI KWAMBA MWANANCHI MMOJA ALIYEPANDA MBEGU ZENYE THAMANI YA SHS MILIONI 20 "AMEPARALAIZI" (AMEPOOZA)UPANDE MMOJA WA MWILI WAKE BAADA YA HABARI KUWA HUENDA MBEGU YAKE HIYO IKAWA "IMEOZA ARDHINI".....KIBAYA ZAIDI NI KWAMBA MBEGU HIZO (SHS MILIONI 20) ZILIKUWA NI FEDHA ZA URITHI WA FAMILIA,NA "MPANDA MBEGU" HUYU ALITUMIA TU NAFASI YAKE KAMA MWEKA HAZINA WA FUNGU HILO AKIAMINI MBEGU ZINGEZAA FAIDA NA KISHA ANGEREJESHA KIWANGO HICHO......




Captured Somali pirates,like Abduwali Abdukhadir Muse (pictured above,smiling as he arrives on the U.S soil) are most likely to seek for asylum in the U.S. upon completion of their jail terms.Compared to the current situation in Somalia,life in a U.S. prison could most probably be perceived as a once-in-lifetime-luxury many Somalis could only imagine.Couldn't this encourage even more pirate attacks in the future?



May be that's why the captured pirate is all smiles....

1 When presidents get invited to the annual Gridiron Dinner for a night of political skits among the Washington press corps, they always go. Not this one, who became the first sitting President politely to decline.

2 We have had lots of canine companions on the rugs of the Oval Office, but Obama's is the first first whose name, Bo, is also his master's initials. Better still, Portuguese water dogs come with fine Democrat credentials – Senator Ted Kennedy has litters of them

3 Americans have become accustomed to knowing that the so-called "enemy combatants" were being held at a safe distance – at Guantanamo Bay. But BO comes into office and instantly declares he will close it within a year.

4 Never mind the Bush policy of hostility to Iran, BO has been making tentative overtures, asking Tehran to cooperate on Afghanistan and edging towards face-to-face talks on its nuclear programme without preconditions.

5 In his first formal press conference, BO took a question from a correspondent of The Huffington Post, the political blog site. In this White House, old journalism must compete with new journalism.

6 As soon as the first cherry buds were bursting in Washington, Michelle Obama, accompanied by local school children, was breaking sod for the First Family's organic vegetable patch.

7 America is no longer shrugging its shoulders at the drug cartel violence shaking Mexico. BO and Secretary of State Hillary Clinton acknowledged that the US is fueling the problem, supplying guns and consuming the drugs.

8 The Beast. The new first limousine – a Cadillac with more armour than your average tank and bullet-proof windows – has already prowled the streets of London, Strasbourg, Prague and Istanbul. And Pennsylvania Avenue on Inauguration Day.

9 Rush Limbaugh is the conservative blowhard on the radio who millions of Americans long ago learned to love or hate. But now his visibility, ratings and influence have soared. Some even tag him the unofficial head of the Republican opposition.

10 When Nato fed live footage of Barack and Michelle arriving for a dinner hosted by Angela Merkel into a packed press room, scores of normally cynical reporters rose to their feet to clap...CONTINUE

SOURCE: The Independent


21 Apr 2009

Shule ya Sekondari ya kutwa ya Marambo yenye wanafunzi 253 ya kidato cha Kwanza hadi cha Nne , iliyopo Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi ina mwalimu mmoja. Mkuu wa shule hiyo, Saidi Mbutuka ndiye pekee aliye shuleni hapo anayelazimika kushika nyadhifa zote.

Mbutuka aliliambia gazeti hili kuwa hali hiyo inatishia mustakabali wa elimu kwa wanafunzi shuleni hapo kwa kukosa elimu inayostahili. ''Mimi ndiye mkuu wa shule, ndiye mwalimu wa zamu, mwalimu wa taaluma, kila siku za kazi natakiwa kuingia katika madarasa yote manne, kwa siku ninakuwa na vipindi zaidi ya 10'', alisema.

Aliongeza, ''kwa hali hiyo hata kama ningekuwa mwalimu mzuri, kuna kila sababu ya kutilia mashaka na ubora wa elimu, mimi ni mwalimu wa masomo ya Sanaa, lakini nalazimika kufundisha Sayansi,'' alisema Mbutuka.

Alifafanua kuwa tatizo hilo limejitokeza mwaka huu baada ya walimu wanne waliokuwa shuleni hapo kwenda kusoma. 'Tunao wanafunzi wa kidato cha Nne ambao wanahitaji wafanye mtihani wa kuhitimu elimu yao, hivi tujiulize nini watavuna wanafunzi hawa kwa kufundishwa na mwalimu mmoja ambaye pia ndiyo nguzo kwa wanafunzi wa vidato vingine,'' alihoji.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo, akiondoka kwenda mjini hulazimika kuwatawanya wanafunzi au kuwaacha chini ya uangalizi wa wanafunzi wenzao ambao ni viongozi.
Mbutuka alibainisha kuwa pamoja na tatizo hilo shule hiyo inakabiliwa na tatizo sugu la mdondoko wa wanafunzi unaotokana na wanafunzi hao kukimbilia katika machimbo ya madini ya Miruwi, Nachianji na Mituguru yaliyopo jirani na shule hiyo.

Alisema mwaka 2006, wanafunzi 53 waliripoti shuleni hapo hata hivyo waliobakia ni 31, wakati mwaka 2007 wanafunzi walioripoti walikuwa 111 waliopo 73. Mwaka 2008 wanafunzi 80 waliripoti na waliopo ni 50. Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Nachingwea, Bakari Mussa, alikiri kuwapo kwa tatizo hilo na kuongeza kuwa halmashauri inashindwa kuwahamishia walimu shuleni hapo kutoka shule zingine ili kupunguza ukubwa wa tatizo kutokana na kukosa fedha za uhamisho.

''Kuna waraka wa serikali unaomtaka mwajiri kutomhamisha mtumishi yeyote bila kumlipa stahiki zake, kwa sababu halmashauri haina pesa tunashindwa namna ya kuiisaidia shule hiyo, lakini uwapo wa tatizo hilo sote tunautambua'' alisema Mussa.

CHANZO:Habarileo


HALAFU 2010 CCM WATAKUJA KUTUIMBIA MAFANIKIO KATIKA SEKTA YA ELIMU,NA KUDAI WAPEWE TENA MUDA WA KUIPELEKA NCHI YETU WANAKUJUA WAO.MIAKA ZAIDI YA 40 BAADA YA UHURU BADO TUNAKUWA NA SHULE YENYE MWALIMU MMOJA?WATETEZI WATASEMA SIE MASIKINI.MASIKINI GANI ANAYEWALIPA WABUNGE ZAIDI YA 300 SHS MILIONI 7 KWA MWEZI?MASIKINI GANI ALIEIBIWA BILIONI 40 NA KAGODA LAKINI ANAMWONEA AIBU HATA KUMTAJA HADHARANI?






Baraza la Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) limepitisha uamuzi wa kuishirikisha Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuhakiki vyeti vya wote wanaoomba kuwania nafasi za kisiasa ili sifa zao kielimu zitambulike.

Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya, aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, TCU imewasiliana na NEC kwa barua, ili utaratibu huo uanze kutumika katika uchaguzi mkuu ujao mwakani.

Nkunya alitoa taarifa hiyo wakati akizungumzia maonyesho ya vyuo vikuu yaliyoandaliwa na TCU yatakayoanza kesho hadi Aprili 24, mwaka huu. “Baraza letu limepitisha uamuzi ili watu wanaotaka kugombea nafasi za kisiasa, vyeti vyao vihakikiwe, ili akipita sifa ijulikane rasmi kama ni daktari basi awe daktari na si daktari feki,” alisema Profesa Nkunya.

Hatua hiyo ya tume inatokana na kilichoelezwa na Nkunya kuwa ni kukithiri kwa vyuo na vyeti bandia nchini, jambo ambalo alisema wamejipanga kulivalia njuga kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha Tanzania haiangamii kitaalamu na kitaaluma.

Alisema orodha ya vyuo visivyotambulika vya nje ambavyo Watanzania wengi wakiwamo mawaziri na wabunge wamesoma, ni ya kweli na kwamba kama kuna mtu anahisi kuonewa ruhusa kwenda mahakamani...ENDELEA

CHANZO: Habarileo.

TAMKO ZURI LAKINI LINALOSTAHILI UMAKINI KATIKA KULIAMINI.HAWA TCU WAKATI WANAZUNGUMZIA UCHAGUZI WA 2010,WANATAKA KUTUMBIA HAWAKUWEPO 2005?AU WATAPATA NGUVU HIYO 2010?JE KAMA SASA WANASHINDWA KUWASHUGHULIKIA HAO "MADAKTARI WA FALSAFA" WALIOKWAA SHAHADA ZAO MTANDAONI TUTAAMINI VIPI KUWA WATAWEZA HIYO 2010?
TATIZO LA NCHI YETU SIO SHERIA,KWANI ZIMEKUWEPO TANGU TUNAKABIDHIWA UHURU NA MKOLONI.TATIZO NI UTEKELEZAJI WA SHERIA HIZO.KUNA MBUNGE ALIKUWA NA TUHUMA ZA KUFOJI ELIMU (SIO YA CHUO KIKUU) BALI YA SEKONDARI.CHA AJABU HADI LEO "ANAPETA".JE HII HAILETI USHAWISHI KWA VIHIYO WENGINE KUJARIBU BAHATI ZAO?

TATIZO LA PILI LA NCHI YETU SIO SHERIA BALI UTEKELEZAJI WAKE UNAOELEMEA ZAIDI AINA YA MKOSAJI.YALEYALE YA ANAEIBA KUKU KWA NJAA KUITWA MWIZI LAKINI ANAYEFUJA MABILIONI ANAOTWA M-BADHIRIFU (NA SANASANA BADALA YA KWENDA JELA ATAHAMISHWA KITUO CHA KAZI).KUNA SHERIA KWA AJILI YA VIGOGO (KAMA AKINA CHEYO WANAOUA KWENYE AJALI LAKINI WANAUNDIWA TUME BADALA YA SHERIA KUCHUKUA MKONDO WAKE) NA SHERIA NYINGINE NI KWA AJILI YA MAKABWELA.


SAKATA la mgodi wa Kiwira kufikishwa bungeni, limeendelea kugubikwa na wingu zito, kutokana na ratiba za bunge kutoonyesha kama serikali itatoa ripoti.

Mgodi wa Kiwira, ambao unamuhusisha Rais wa Serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati, Daniel Yona umejaa utata kutokana na madai kuwa kampuni ya Tan Power Resources Limited iliununua kwa Sh70 milioni badala ya thamani yake halisi ya Sh4 bilioni.

Hadi sasa serikali haijatoa ufafanuzi wowote kuhusu utata huo licha ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuahidi katika mkutano wa 13 wa bunge kwamba,ingetoa taarifa bungeni.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alisema tu kwa kifupi "vuta subira".

Iwapo serikali haitatoa ripoti hiyo katika mkutano unaoendelea itakuwa ni mara ya tatu kupigwa tarehe suala hilo.

Katika mkutano wa 13, wakati mjadala wa mgodi wa Kiwira na Meremeta ukiwa umepamba moto, Pinda alisema serikali ilikuwa ikiandaa taarifa lakini akasema ni bora asulubiwe kuliko kutaja wamiliki wa Meremeta kwa maelezo kuwa inahusu usalama wa taifa.

Lakini, hadi mkutano huo unamalizika hakukuwa na ripoti yoyote ya serikali na hata ulivyokuja mkutano wa 14 hakukuwa na ripoti kama hiyo.

Tayari ratiba ya bunge imetoka na kuonyesha kwamba, hoja nzito inayotarajiwa kutikisa bunge hadi sasa ni ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo imepangwa kuwasilishwa bungeni Aprili

20 Apr 2009



Mie adhabu zangu HUKO O'level zilikuwa kwenye namba (HISABATI) ambayo kwa miujiza mikubwa nillibuka na D (japo ilikuwa dhaifu mno,na chupchup iwe F) na FIZIKIA ambayo sikuwa na ujanja nayo na nikaambulia F.

18 Apr 2009


Na Leon Bahati

SAKATA la Halmashauri ya Karatu, kugomea kulipia malazi ya Makamu wa Rais, Dk Ali Mohamed Shein na ujumbe wake limechukuwa sura mpya, baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Celina Kombani kuunga mkono uamuzi wa halmashauri ni sahihi.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili, Kombani alisema halmashauri za wilaya haziwajibiki kuchangia ziara za mawaziri, rais au makamu wake, wanapotembelea katika maeneo yao.

Kombani alibainisha kuwa kama ingekuwa utaratibu huo upo, halmashauri nyingi zingefilisika hasa ambazo mawaziri wanatoka, kwa sababu wana utaratibu maalumu wa kutembelea zaidi ya mara tano kwenye maeneo yao, kwa mwaka.

"Kwa mfano kwa mwaka mimi hufanya ziara mara sita katika wilaya yangu ya Ulanga (Morogoro). Tukisema wanigharamie basi ingefilisika pamoja na halmashauri nyingine ambazo zina mawaziri," alisema Kombani ambaye ni Mbunge wa Ulanga Mashariki.

Akielezea kuhusu taratibu za matumizi ya fedha kwenye halmashauri, alisema kwa kawaida matumizi yote hupitishwa kwenye vikao vya madiwani.

Alibainisha kuwa gharama za msafara wa rais, makamu wa rais na mawaziri hugharamiwa na serikali kuu, kulingana na taratibu zilizowekwa.

"Ndiyo maana rais anapokuwa kwenye ziara huenda na vyakula vyake," alisema Kombani lakini akafahamisha kuwa halmashauri zinaweza kutenga fungu kwa ajili ya kuuandalia ugeni kwenye maeneo yao chakula cha jioni.

Iwapo halmashauri itaamua kufanya hivyo, alisema kuwa ni lazima fungu hilo liwe limepitishwa na halmashauri kupitia vikao vyake halali na si mkurugenzi na watendaji wake.

Alipoulizwa juu ya adhabu ya kiongozi wa halmashauri atakayetoa fedha pasipokufuata taratibu; alisema kila halmashauri ina taratibu zake za kuwajadili viongozi au maofisa waliokiuka taratibu na kuwachukulia hatua.

Suala la Halmashauri ya Karatu, kugomea kulipia malazi ya Makamu wa Rais pamoja na ujumbe wake liliripotiwa na gazeti la Mwananchi Jumatano iliyopita likionyesha kuwa Mkuu wa wilaya hiyo, Mathew Sedoyeka alimjia juu na kumtaka aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Majid Myao, aandike barua ya kujieleza kwanini alikataa kutoa fedha za kulipia ziara ya makamu wa rais wilayani humo.

Sedoyeka hakufurahishwa na kitendo cha halmashauri hiyo kugoma kulipa kiasi cha Sh2 milioni ambazo ni malipo ya kulala siku moja pamoja na chakula kwa ujumbe huo wa makamu wa rais, katika hoteli ya Bougain Villea ya mjini Karatu.

Kwenye barua ya kujieleza iliyoandikwa Machi 3, 2009 yenye kumbukumbu namba kdc/ded/cv.3/1/121, Myao amejitetea kuwa uamuzi wa kutolipiwa ziara hiyo, umetokana na kamati ya fedha ya madiwani kukataa kuidhinisha fedha hizo.

Alisema kutokana na kutoidhinishwa malipo hayo, aliona angekiuka Sheria namba tisa ya mwaka 1982 ambayo inahusu masuala ya matumizi ya fedha za halmashauri na maamuzi ya kamati ya fedha.

“Kama mimi ningetoa malipo hayo ni wazi ningekiuka sheria za serikali za mitaa hasa ikizingatiwa madiwani katika kikao chao halali ndio waligomea,” alieleza Myao.

Akizungumzia sakata hilo, Mbunge wa Jimbo la Karatu, Dk Willibrod Slaa alisema alichofanya ofisa huyo wa serikali ilikuwa halali kwa sababu walikuwa hawana bajeti ya malipo hayo.

Dk Slaa alitoa wito kwa serikali kutomuadhibu mtendaji yoyote wa halmashauri hiyo kutokana na uamuzi uliochukuliwa, ambao ulizingatia maadili ya kazi na utekelezaji wa utawala bora.
CHANZO: Mwananchi


Riyadh, April 16 - Saudi investors have asked Tanzania if they can lease 500,000 hectares of farmland mainly for rice and wheat farming as part of a plan to secure food supplies for the desert kingdom, officials said.

Senior officials from the Saudi capital's chamber of commerce made the request on the sidelines of a meeting with visiting Tanzanian President Jakaya Kikwete.

"Tanzania is ready to do business with you ... There is 100 million acres (40.5 million hectares) of good arable land," Kikwete told Saudi businessmen.

Samir Ali Kabbani, head of the chamber's agriculture committee, said: "We had very positive feedback."

"He (Kikwete) told us that Tanzanian authorities can lease us plots each of which covers up to 10,000 hectares for a 99-year period," he told Reuters after the meeting.

The Saudi government has joined private operators to invest in farm projects abroad after a long and costly food sufficiency plan threatened to deplete the desert kingdom's water supplies.

Saudi businessmen and officials will visit Tanzania in the next few weeks.

"They can lease the land from the government," January Makamba, an aide to President Kikwete, told Reuters.

"But we have to make sure we don't end up in a situation similar to that of Nigeria: Huge oil reserves but long queues in front of petrol stations," Makamba said.

Saudi officials are particularly interested in Tanzania because of its geographic proximity, political stability and the availability of water resources and farmland.

Several Saudi firms have already started investing in agricultural projects from Indonesia to Ethiopia.

Indonesia said in August that Saudi BinLadin Group would invest $4.3 billion on 500,000 hectares for rice farming.

Saudi Arabia's annual wheat needs are estimated at about 2.5 million tonnes and it imported a little over 1 million tonnes of rice in 2008, according to the U.S. Department of Agriculture.


SOURCE: Reuters

"TANZANIAN AUTHORITIES CAN LEASE THE SAUDIS PLOTS EACH OF WHICH COVERS UP TO 10K HECTARES FOR A 99-YEAR PERIOD!?"

DID I QUOTE THAT RIGHT? YES I DID.

CALL ME ONE OF THE DOUBTING THOMASES BUT IF THIS STORY IS TRUE,THEN PERHAPS THE LIKE OF CHIEF MANGUNGO WERE NOT SO DUMB WHEN THEY WERE DUPPED INTO SIGNING SOME CRAZY LAND CONTACT WITH KARL PETERS&co..AT LEAST THE CHIEFS COULD HAVE AN EXCUSE...IT'S DURING THE "DARK AGES" AND THE FORE-RUNNERS OF COLONIALISM TOOK OF ADVANTAGE OF THE CHIEFS' ILLITERACY AND LACK OF SUFFICIENT KNOWLEDGE IN GOVARNANCE OF THEIR PEOPLE AND PROPERTY.

BY THE WAY,INSTEAD OF BEGGING THE SAUDIS,WHY SHOULDNT THE PRIORITY BE IN EMPOWERING THE LOCAL FARMERS IN A COUNTRY WHERE THE ECONOMY DEPENDES HEAVILY ON AGRICULTURE THAT ACCOUNTS FOR MORE THAN 40% OF GDP?


HIVI HAWA WAHINDI WAMETUROGA HADI KUFIKIA HATUA YA KUBADILISHA MAJINA YA MITAA YETU KWA MINAJILI TU YA KUKIDHI LADHA ZAO!HUYU ABUU JUMA,MEYA WA MANISPAA YA ILALA SI ALIAHIDI KUFANYIA KAZI TABIA HII CHAFU YA KUBADILISHA MITAA PASIPO KIBALI?FOR THAT MATTER,INAELEKEA CITY FATHERS WAMEAMUA "KUKUBALI MATOKEO" NA HATIMAYE KUWAACHA HAO WAHINDI WAJIBADILISHIE MAJINA YA MITAA KWA NAMNA WANAVYOTAKA!

NA KAMA DESTURI ILIVYO,YAYUMKINIKA KUAMINI KWAMBA "KUKUBALI MATOKEO" HUKO HAKUKUFANYIKA HIVI HIVI TU,KUNA FISADI "KADIKISHWA KITU" KURIDHIA UCHAFUZI WA HISTORIA.OLE WAO WANAOENDEKEZA TAMAA ZAO ZA FEDHA NA KUPUUZA URITHI WETU WA KIHISTORIA.IPO SIKU MAKABURI YAO YATABOMOLEWA KWA HASIRA YA VIZAZI VIJAVYO.WHY NOT?MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU ANAPASWA KUKASIRISHWA NA UPUUZI WA NAMNA HII.

17 Apr 2009

KWA MUJIBU WA GAZETI LA Uhuru,KATIBU MKUU WA CCM,YUSUPH MAKAMBA,AMEAGIZA UONGOZI WA CCM NA JUMUIYA ZAKE NGAZI ZA MIKOA KUANDAA MAPAMBANO YA KUMPONGEZA JK NA SERIKALI KWA KAZI NZURI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA.....
Nadhani muda si mrefu kutakuwa na tangazo jingine la kuagiza maandamano ya kupongeza mafanikio ya kutimizwa kwa ahadi ya MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA sambamba na pongezi za kuwabainisha wamiliki wa Kagoda.
CCM HOYEEEE!!!!!

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!!!!

That's all I can say!

Habari nyingine ndani ya gazeti hilo ni pamoja na "UFISADI MALIASILI:Sh Bil 2.4 zayeyuka kiutatanishi;Mil 790 zatumika kununua pikipiki hewa;Watumishi watimuliwa,wachunguzwa"






Queen Elizabeth II is Britain's most trusted public figure, leaving Prime Minister Gordon Brown and other politicians trailing in her wake, a new survey revealed on Friday...CONTINUE


A total of US$30 million (over 36bn/-) given to Tanzania as aid by the Norwegian government in the past 12 years may have been squandered through corruption and mismanagement, an independent report has revealed.

The just-released Anti-corruption Resource Centre Report entitled `Does Aid work?`, which considers the challenges to aid effectiveness in major natural resources programmes, says half of the US$60 million did not make it to the primary targets and ended up lost.

The report is authored by Erik Jansen, a senior advisor at NORAD Evaluation Department.

A former programme officer at the Norwegian Embassy in Tanzania quotes in the report an evaluation by independent consultants in 2006 as having established these facts.

``Those who have control over the natural resources are in a powerful position and usually have easy access to money... Tanzania has not been successful in managing its natural resources in a sustainable and equitable manner, nor has the country been able to achieve significant economic growth in its utilisation of these resources,`` notes the report.

Norway financed the Management of Natural Resources Programme (MNRP) in Tanzania from 1994 to 2006 and the report names the Natural Resources and Tourism ministry as being in charge of managing the forestry, fisheries and wildlife resources.

``The Ministry had three separate divisions, each dealing with one of these resources. MNRP had projects in the forestry, fisheries, and wildlife sectors that were closely connected to these three divisions of the Ministry. In all of the three sectors there has been pervasive corruption during the last decades. Management and staff in the Ministry, together with politicians and people from the local population, have plundered the resources and exploited the resources in a way that is not sustainable. Often this has been in collaboration with foreign investors,`` writes Jansen.

The example is given of assistance from the Kuwait Fund for Arab Economic Development, the OPEC Fund for International Development, and the Saudi Fund for Development, which resulted in one of the largest bridges in Africa. It was built over the Rufiji River in 2003.

``The bridge led straight into a natural forest of about 20,000 square kilometres that had remained fairly unexploited until then. A comprehensive study conducted after the completion of the bridge showed extensive illegal exploitation of the forest,`` says the report.

It adds: ``Logs worth tens of million of US dollars were exported illegally to China and other countries in Asia. Taxes and royalties were paid for only four per cent of the forests that were harvested.``

According to the study, illegal logging cost Tanzania about US$ 52 million of its potential revenue annually.

The reports further notes that corrupt politicians and representatives of the fisheries and wildlife sectors allowed these resources to be plundered by national and international companies, provided they themselves obtained a share of the resultant profit.

``Both in the fisheries and wildlife sectors, licences are allocated to investors at a price that is only a fraction of the market price. Corrupt representatives of the Government earn huge amounts of money that should have gone into the Treasury,`` the report states.

``The development partners in Dar es Salaam recently notified the Government that the fees which the Government received from the wildlife sector were minimal. The Government only charged US$ 8,000 for hunting blocks that had a much higher market value.

``The Government accepted the complaint by the development partners and increased the fees to US$ 40,000 for each block. However, many of the politicians and ministers who controlled these hunting blocks complained that the increased fees would lower their profit and therefore demanded that fees should remain at the old levels,`` it adds.

Some 150 trawlers from EU member countries and the Far East operating within Tanzania`s Exclusive Economic Zone in the Indian Ocean are said to have been paying a paltry US$18,000 annually to obtain a licence. But on a good day of fishing, the trawlers are able to catch fish of the same value.

The report says that, if the Government had charged market value for these licences, the Treasury could have collected US$20 million annually for the trawlers` licences.

``It is also well known that the export of Nile perch from Lake Victoria has been underreported for many years in order to avoid taxation. There is much money to be earned by government officials and politicians who contribute to increased export of natural resources without it being taxed,`` it adds.

The Natural Resources and Tourism ministry is viewed as being in a special position in the government set-up because of its opportunity to generate its own resources from taxes, fees and royalties. It also receives allocations from the Treasury.

``It is difficult to estimate how much money the Ministry transfers to the Treasury and how much disappears due to corruption. With all the potential income from natural resources, the Government of Tanzania should have been able to manage its own natural resources without depending on funds from development partners,`` notes the report further.

A report from the World Bank enforces this view, saying: ``Because of policy failures, Tanzania’s natural resource endowments are not harnessed in an optimal way to achieve both economic growth and poverty reduction. On the contrary, owing to weak governance regimes in revenue-generating sectors, resources are offered below market price to the benefit of a few powerful winners and the loss of the majority of the rural population.``

It adds: ``Yet these natural resources provide substantive potential for income to communities in the rural areas. The weakness in governance regimes in forestry, wildlife and fisheries include primarily the lack of transparency and accountability in issuing rights to extract resources and accrue revenues from them, inequitable sharing of benefits with communities, and monitoring and surveillance of stocks.

``In all four principal sectors providing natural capital in the growth equation – forestry, wildlife, fisheries, and mining – royalties are set arbitrarily and do not reflect scarcity. Royalties are hence not used as a policy instrument of intertemporal resource pricing and sustained yield management (Pfliegner 2008).``

The World Bank report stresses that the problem is not lack of legal acts and instruments, policies, strategies and plans that explains the mismanagement and corruption in the natural resources sector but lack of the political will to follow up on the adopted instruments.

``The Government of Tanzania has a complicated relationship to its task of managing the natural resources. On the one hand the government has, with the support of its development partners, spent much time and resources in developing legal acts, policies, strategies, national plans, and sector strategies for its forestry, fisheries, and wildlife resources which are compatible with those of the international community.

No doubt many government officials in Tanzania do their utmost to comply with and follow up these adopted plans and strategies.`

``On the other hand, there are also many government officials and politicians who undermine the policies they themselves have been central in having Parliament adopt.

Many of these politicians and government officials have held high positions in the Ministry. These leaders can force honest government officials to adopt corrupt practices,`` it adds.

Published as part of the project named `Corruption in Natural Resource Management`, the paper suggests a more sophisticated approach to budget and programme support.

``If we are to improve and understand the relationships between a plan and the reality, it is important that we are open and share experiences made in development aid.

It is therefore a good thing that the political leadership in the Ministry of Foreign Affairs and Norad welcomes a broader and more open debate on development aid,`` writes Jansen.

Renewable natural resources in Tanzania play an important role both for the population in rural areas of the country and for the economy as a whole.

Of Tanzania`s total population of about 40 million people, 75 per cent live in rural areas.

Most of the rural population has access to forestry, fish and/or wildlife resources.

It is estimated that on average 40 per cent of the income in rural households comes from one of these three natural resources.

Agriculture is the main economic sector in the rural areas but most people living off the land use simple technology and land productivity is very low.

Efforts to improve the agricultural sector are slow and income and food from forests, fisheries and wildlife will for many years continue to play an important role for the rural population.

Natural resources are important at the national level too. Timber from the forests is important for economic activities in the country and it is also a major source of foreign exchange.

The country also receives substantial foreign exchange from the export of Nile perch from Lake Victoria and shellfish from the coastal areas. Wildlife brings income from tourism and hunting licences.

Traditionally, local people have used their own rules of management for the various natural resources they have found of interest. But this has changed during the last few decades.

A new set of actors, very often foreign investors, have discovered the value of Tanzania`s natural resources and stiff competition for scarce natural resources has changed the constellation among the actors.

SOURCE: Ippmedia

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.